Nini cha kufanya Mumeo akipoteza Kipato/Kazi?

 

Enzi nafundwa, hakuwa kuhusu kufanya tendo la mikao/mitindo yake tu bali pia ilikuwa kuhusu Maisha ya ndoa kwa ujumla (Uzazi,malezi ya Watoto,Vifo na jinsi ya kukabiliana na maombolezo). Unaambiwa wazi kabisa kuna wakati Mumeo atakosa pesa, mtafiwa na unatakiwa kufanya  nini  wewe kama mke ikiwa hayo yatatokea.

 

Kulingana na urefu wa Ndoa yetu nimekabiliana nayo yote hayo, hivyo nikalazimika kufanyia kazi kwa vitendo yale ambayo nilifunzwa awali, kwasababu sikuolewa mara tu baada ya mafunzo, kuna makosa mengi nimefanya. Baadhi ya mafunzo niliyokuwa nayakumbuka niliyaandika na kuyatunza ki-eletronic (Unaikumbuka Dinahicious ya 2007/8?) hivyo ilikuwa rahisi kurudi  kwenye files nakujikumbusha.

 

Turudi kwenye Topic ambayo ni Mwanaume na Pesa; Kwa kawaida Mwanamke anaekupenda kiukweli huwa haonyeshi kujali wala kutaka pesa zako (kama unazo). Mara zote anakuwa amekwishaona kuwa una potential ya kuwa na kipato cha uhakika kwa sababu wewe ni ambitious (inategemea na unavyojibeba/jieleza). Anajua kabisa bila kipato itakuwa ngumu kwake kuvutiwa nawe kwa muda mrefu(maisha ya ndoa), inakuwa kana vile huna “UANAUME” kwamba hujakamilika kusimamia na kuilinda familia ikitokea mmeamua kufunga Ndoa.

 



 

Ukianza uhusiano na Mwanamke huyu atakusukuma ili kujiboresha na hivyo kukua kiuchumi kwa kupendekeza mf uangalie uwezekano wa kubadilisha kazi, kujiendeleza kielimu ili kuongeza uwezekano wa kufanikiwa na anapofanya hayo anakua very loving, hakusukumi na harudii mara kwa mara…unaweza hata kusahau. Mtakapofunga ndoa nakuanza kuishi pamoja kama Mke na Mume na sasa mna watoto. 


Gharama zimeongezeka lakini anaona unachelewa kufanya mabadiliko, anaweza kujiweka yeye mbele na kukuambia kuwa anataka kurudi Shule ile kuboresha/ongeza kipato(anakukumbusha kwa kinyume)….hapo kwa kawaida kama mwanaume utachukua uamuzi wa kufanya hivyo  kwasababu yeye ana majukumu mengine na muhimu kwa Watoto wenu. Utajitahidi kumpunguzia Mzigo, vinginevyo si atakuwa single mother with a husband? No...yes.

 

 

Kwa kawaida(asilia) mwanamke havutiwi kabisa na mwanaume ambae hana pesa/kipato….huitaji kuwa Milionea isipokuwa uwe na uwezo wa kurekebisha mambo na kusimama ikiwa yeye hana Kipato au Ikitokea kaamua kuwa Mama wa nyumbani uweze kusimamia Majukumu yako kama Mume  vema wakati yeye ana-focus kwenye malezi ya Watoto wenu na kutunza nyumba yenu. Kiasilia Mkeo anahitaji uhakika na ulinzi wa kipato kama vile wewe unavyohitaji “umiliki”, Tendo la ndoa kwa uhakika, Heshima na Amani kutoka kwake.

 

 Unatakiwa kufanya nini ikiwa Mumeo kapoteza Kazi?

Unatakiwa kumpoza na kumpa Moyo/matumaini na kumhakikishia kuwa unaamini anaweza na kuongezea  mengine ya kiimani kulingana na mnachoamini kama familia. Kamwe usimshushe kwa kumwambia “usijali nitaenda kuongea na Fulani atusaidie” au “usijali naenda kutafuta kazi” na wala  usi-panic na usimpe presha ya kutafuta kipato. Jukumu lako ni kusimama nae, kumpa support na kumpa muda(kaa kimya kuhusu issue hii nzima), kama mwanaume anajua nini cha kufanya. Atajipa siku kadhaa au Wiki then atatoka humo ndani na akifanikisha atakujuza.

 

Hivi, mnapokwenda nje for dinner na mumeo  ndiye alieandaa na kulipia, unahisi nyenyere za ajabu hata kama circle yako ipo ukavuni(baada ya kupevusha pale njia panda ya kuelekea siku Salama na Hedhini)mkifika home huwa mnakuwa na a very hot tendo tofauti na wewe ukiandaa/lipia dinner date? Ukute ni mimi tu.

Haya bwana, takuona wiki ijayo.

Bai.

Comments