Heshima kwa mumeo(Nguzo tano za Ndoa bora)

 Natumai upo salama,..mie mzima kabisa ahsante kwa kujali.


Bila shaka unewahi kuona/soma/sikia watu wakisema "Mwanaume haitaji kupendwa bali kuheshiniwa", kwamba Heshima kwake ndio kupendwa...lies the Internet tells. Mwanaume anahitaji vyote, Heshima na kupendwa....ila ukifikiria kiundani(inategemea na situation iliyokufanya ushushe heshima kwake ) kumpenda Mume wako bila kumheshimu ni ngumu. Acha kufikiria kiundani.


Pengine Mumeo amewahi kukuambia kuwa anahisi kuwa huna heshima kwake...halafu ukang'aka na kudai sio kweli, kwamba mbona unamheshimu sana tu! Heshima kwa Mwanaume(Mumeo) ni tofauti na vile unamuacha anajiachia kwenye Internet/Bar na wadada wengine, kutopinga maamuzi yake hata kama ni mabaya/hatarishi, kutokuvaa mavazi fulani n.k.



Hivi ndio unavyopaswa kumheshimu Mumeo ukiachilia mbali kumsikiliza pia usizungumzie mapungufu yake kwa watu wengine hata kama ni Mama yako.


Thamini Ndoa yenu (sio kuishi kwa mazoea) na ikitoke mmepishana na kugongana/zozana chunga Ulimi wako na usitumie Lugha/maneno ya kudhalilisha.


Ikitokea amekushirikisha kwenye jambo la familia na akakupa nafasi ya kufanya uamuzi....onyesha kumuamini yeye kufanya uamuzi huo kisha subiri majibu, sio kurudi na kuanza kumbugudhi na maswali.


Badala ya kwenda kwenye Social media/kwa Rafikizo/Wazazi kuomba Ushauri, omba ushauri kwa Mumeo. Pengine Mumeo sio mshauri mzuri kwenye baadhi ya mambo(inategemea na Upeo/Elimu/Uzoefu) bado mmpe hiyo heshima.


Akiamua kusaidia kwenye suala fulani hapo nyumbani muamini na muache afanye mpaka mwisho....unless otherwise atakuomba msaada, usiingilie au kukosoa akifanyacho. Ni kawaida kwa Mumeo kukataa adharani kuwa ahitaji kusifiwa, kupewa attention au kuhakikishiwa Penzi ulilo nalo kwao. Ukweli ni kwamba hawa viumbe wanahitaji kusifiwa kama vile sisi tunavyopenda tofauti wqo hawahitaji mara nyingi kama sisi.



Sifia mumeo akitokelezea(pendeza), akikamilisha jambo(kubwa au dogo),  mhakikishie kuwa unampenda na hakuna mtu atachukua nafasi yake(kwa vitendo pia). Je unajiheshimu na unamheshimu Mkeo ili akuheshimu au nikukumbushe pia?

Muda wako hapa ni thamani kubwa kwangu, ahsante.

Comments