Wivu na kutoaminiwa

Habari da Dinah, Mimi na mke wangu tumekuwa tukiishi maisha ya amani, Furaha na Upendo.


Kwa muda sasa mambo hayapo kama yalivyokuwa miaka ya nyuma. Mke wangu amekuwa na wivu sana na haniamini tena kama alivyokuwa akiniamini zamani.

Siku hizi tunapitisha hata miezi miwili, hajishughulishi wala kuonyesha kutaka kuwa karibu nami.

Mabadiliko ya tabia yamenifanya nihisi kuwa labda yeye sio muaminifu na anapata hisia mbaya juu yangu kutokana na Maovu anayoyafanya yeye.


Je, unanishauri nichukue hatua gani ili kuokoa ndoa yetu?

***************


Dinah anasema: Habari ni njema kabisa, ahsante kwa ushirikiano.


Umenikumbusha "ukiona kaanza wivu au hakuamini ujue yeye ndio anafanya maaovu nje ya ndoa na guilt ndio inamfanya ajisikie wivu/asikuamini"....wanaoamini hiyo ni ama wapuuzi....au hawajahi kupenda.


Wivu na Uaminifu ni vitu viwili tofauti lakini kimoja kinasababisha kingine hivyo naweza kusema vinategemeana.


Wivu ni hisia kama ilivyo hisia ya kumpenda mtu. Ikiwa unampenda mtu kimapenzi hutotaka kuona "tishio" la yeye kuwa na mtu mwingine kimapenzi bali wewe na hapo ndio Wivu unapojitokeza.


Kutokumuamini mtu kunatokana na issues za Wivu ambazo hazijafanyiwa kazi(kurekebishwa).

Nitakupa Mfano wa upande wa pili ili unielewe vema na mfano huu utakusaidia kuchukua hatua madhubuti kuokoa Ndoa yako.


Mf; mwenza wako anamazoea ya karibu na wanaume ambao wewe huwajui(marafiki zake) au hata kama unawajua(marafiki zenu).


Inafikia mahali mazoea hayo yanafikia hatua mbaya ya kuitana honey, sweet, Mpenzi, laazizi "kiutani" na kutumiana "visual" hugs, mabusu na emotions nyingine ambazo sio sahihi kwa watu ambao sio wapenzi.


Wao wanakua wa kwanza kusalimiwa asubuhi pale akiamka tu na hupewa "usiku mwema" kiss visually(wewe hupewi, yaani haipo siku hizi kwa sababu haupo kwenye Simu/Tablets).


Mkeo anawatembelea wao na kula nao chakula au kunywa nao (wewe na yeye hamfanyi hivyo siku hizi) kwasababu muda unatofautiana na hata ikitokea mpo pamoja bado hilo halitokei.


Unajaribu kuweka hisia zako wazi kwake kuwa hupendezwi na tabia hiyo ya mkeo, lakini badala ya mkeo kuomba radhi kwa kukuumiza hisia zako na kukuhakikishia mapenzi yake kwako kwa vitendo (sio Ngono bali affection, attention etc). Yeye anakuambia "acha wivu hao ni marafiki tu".


Au badala ya kuahidi kuachana na hao watu (kuwafuta/zuia) kimawasiliano na kuonyesha angalau dalili ya kubadilisha tabia yake hiyo mbaya....anajitetea au anawatetea "watu wake" au ana-justify kwa kusema "mbona wewe na akina blablabla siwaingilii".


Hapo ndipo kutomuamini Mkeo "kutazaliwa"....na kusipokuwa na kuaminiana kwenye uhusiano wowote basi ujue kuna tatizo kubwa na tatizo hilo litaingilia uhusiano wenu wa Kingono na hivyo kuhatarisha Uimara wake.

******Mwisho wa Mfano.

Katika hali halisi hatupaswi kuwaamini wenzetu kwa asilimia zote lakini huwa tunaongeza asilimia kubwa sana ya uaminifu kwa watu tunaowapa Mioyo na miili yetu.


Mkeo alipoanza kuhisi Wivu na kukueleza ulipaswa kuchukua hatua za kurekebisha kama ni tabia au matendo unayoyafanya na kupelekea Mkeo kupata wivu.


Sasa, kwasababu hakuna lililofanyika na labda ukategemea mkeo kuzoea au kuacha wivu bila wewe kutoa ushirikiano lakini haikuwa hivyo na badala yake sasa hakuamini tena.


Wivu hauwezi kuondoka wakati "chanzo" cha wivu bado kipo.....na hapo ndio tatizo la kutoaminiwa na mkeo lilipojitokeza.


Wanawake tunatofautiana na wanaume linapokuja suala la ngono, kwa mwanaume anaweza kuwa na wivu na akaweza kuendelea na tendo la ndoa kama ifuatavyo.


Lakini kwa mwanamke anaekupenda huwa ngumu kiasi kwani kwake tendo hilo ni sehemu ya mapenzi yake kwako na ukaribu wa muungano wenu kama wanandoa....sio ngono ili kumaliza hamu ya mwili.



Hatua gani uchukue: Mawasiliano.....weka issue Mezani na mizungumze kwa upendo, yeye akueleze hofu zake na wewe weka zako (umegusia kuwa unahisi yeye ndio Mkosaji na guilt inamfanya akuhisi wewe) mezani kisha muelewane na Mkubaliane kufanya mabadiliko..

Ushirikiano....badala ya kufananisha au kutetea "chanzo cha Wivu" jiweke kwenye "receiving end" wakati anajieleza ili upate kujua anavyojisikia kisha rekebisha lolote linalosababisha ajisikie anavyojisikia ili muungano wenu uwe na amani.

Kumbuka Ndoa ni safari yenye mabadiliko mengi, hivyo ni vema "kutozoea" mabadiliko au "kuyavumilia" na badala yake kwa pamoja fanyia kazi lolote linalijitokeza ambalo linatishia kuharibu kile mlicho nacho.


Rejeeni nyuma, awali mlikuwa mnafanya nini kama wapenzi? Fanyeni yale na kuongeza mapya na yale ya kati....


Unapofundwa, unaambiwa "usisahau ulikotoka....usiache kilichokufiikisha hapo ulipo"......hivyo kurejea mwanzo kimapenzi husaidia kuwakumbusha ni kiasi gani mnapendana.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments