Mwili unafanya nisijiamini...

Dada/Mama shkamoo mimi ni kijana umri wa kwenye early 20s urefu 6ft  naitwa junior naishi arusha nimekuwa nikiambiwa na my friends kuwa mimi ni handsome na vitu vingine ila sijui tatizo liko wapi.

Nashkuru sana kwa Blog yako ambayo nimekuwa nikijifunza mambo mengi kuhusiana na Mahusiano na vitu vingine vingi.


Nilikuwa naomba ushauri sana sana kutokana na tatizo langu la kutokuwa na self confidence na sometimes nakuwa insecure about my body.


Wakati wa kum-face msichana naeza nkamuona msichana 4 the 1st time na kupenda kujuana nae ama kumuomba no zake lakini nashindwa.

Mimi ni mkimya na mara nyingi huwa naogopa sana kutoswa na msichana kuhofia aibu na pia ninapokuwa katika approaching phase huwa najiona kama sina quality za msichana kunikubalia sababu maybe kwa ajili ya body yangu ama other negative reasons na kwamba siwezi kukubaliwa.

So kutokana na mimi kufikiria hivyo nimekuwa si-participate kwenye relationships meaning I don't care, no feelings no emotions stuffs like that.


Naomba sana ushauri wako kwa kuniambia tatizo langu hasa ni nini? na unanishaurije? Asante.
 
***********

Dinah anasema: Aiii Mama tena?!! Mwanangu mkubwa anamiaka 3 sio 20+....Mdogo wangu wa mwisho anamiaka 21 so yeah I am your Dada hehehehe nani ataka uzee hapa! Ahsante sana na shukurani kwa Ushirikiano wako.


Kama Mwanaume umekuwa "programed" ku-handle kukataliwa bila aibu wala nini....piga kifua jiambie umejiamini na umeweza kutongoza (Baba yako anapaswa kukusaida kwenye hili, mie mkimama hata sijui mambo yenu wakibaba).

Kwenye Maisha yako utakataliwa mara nyingi zaidi kuliko kukubaliwa....ili kupunguza uwezekano wa kukataliwa unapaswa kuwa na uhakika kuwa msichana husika anapendezwa na wewe angalau kwa mbaaali. Jaribu kutengeneza mazingira ya kirafiki zaidi kuliko Mapenzi.

Kuna u-handsome ambao ni Universal (Kama yule Lil Romeo wa MasterP) kwamba kila mtu anakuona "handisamu" alafu kuna ule u-handsome unaotokana au kutegemea na mtazamaji au jinsi mhusika anavyojiweka/jibeba.

U-handsome universal sio kigezo cha kupendwa au kukimbiliwa na wanawake, u-handsome can be boring kwamba mhusika haweki effort maeneo mengine kwavile anajijua yeye yupo "fresh" maeneo ya Usoni.


Alafu kuna wale watu ka' Ali Kiba kwa mfano(I just like the Kid)....sio handsome lakini ni attractive(which can be handsome kwa mtazamaji husika lakini sio kwa kila mtu).


...anajua "kujibeba"....anajua mwili wake ulivyo, anautunza ubaki vile ulivyo na anajua kuuvika/Pendezesha.....anaweza kutoka bila kuchana nywele na kavaa Ndala bado akavutia....haitaji huge effort kuvutia....sijui unanielewa?

Umegusia zaidi ya mara mbili kuwa unadhani tatizo ni mwili wako je, mwili wako ukoje? Urefu wako mbona ni wa kujivunia kabisa!!


Je, unadhani mwili wa aina gani utakufanya ujiamini? Au unadhani wasichana wanavutiwa nao na hivyo kukupa hali ya kujiamini?


Hayo mambo ya Ubora wa kupendwa au kuvutia watu huwa tunajiwekea tu kuvuta muda....Muda ukifika tunajikuta tumedondokea kimapenzi watu tofauti kabisa.....kati ya vibox 10 anaTick kimoja tu hehehehehe Nomaaa! My point is hakuna viwango wala ubora linapokuja suala la Kupenda.

Kuwa na uhusiano wa kimapenzi katika Umri wako sio muhimu kiviiile hivyo badala ya kupoteza muda kutafuta namna ya kuwa na Msichana ni vema kuwekeza Muda wako kwenye kujifunza kujipenda, kujikubali ili upate hali ya kujiamini.

Usipojipenda wewe mwenyewe na kujiweka katika hali ya kuvutia ni vingumu kwa watu wengine kukupenda ama kuvutiwa nawe.

Sote huwa tunavitu viwili-vitatu ambavyo huwa tunakuwa insecure about, haijalishi ni Mzuri kiasi gani, unapesa kiasi gani, akili (academically) kiasi gani au umeumbika vizuri kiasi gani lazima kuna siku utahisi some sort of insecurity. Nadhani ni sehemu ya Ubinaadamu (hakuna aliekamilika).

Utapata vipi hali ya kujiamini?

Tuanze na tatizo kuu hapa ambalo ni "body"....iwe ni mwembamba au Mnene, mazoezi ni muhimu. Mwembamba unahitaji kujaza Misuli na Mnene unahitaji kupunguza Mwili (fat) na kujaza Misuli hivyo fanya mazoezi kulingana na Mahitaji yako.

Kujaza Misuli sio kama Mabaunsa hapana, hiyo wala sio attractive....Misuli kiasi tu ili upate ile V-shape ambayo ukitupia kafulana size ya kati kanakaa vizuri maeneo ya mabegani na kifuani....sio inateremka ka' Blauzi.

Nadhani kuna Blog ya Kibongo
kuhusiana na Mazoezi inaitwa Bryan or something au yeyote unayodhani itasaidia kukupa maelezo muhimu kuhusu Mazoezi kulingana na mahitaji yako.

Muonekano; Hakikisha kichwani ni kusafi....kama ni nywele ndefu basi zipunguze kiasi. Sijui wanawake wangapi wanavutiwa na mwanaume kusuka au rasta....kama unasuka au una rasta hebu badilisha hilo(new start eti).

Mavazi: Badilisha mtindo wa uvaaji wako(style), nenda zaidi kwenye mavazi ya kawaida (casual) lakini yanavutia....achana na trends (Dar combine a.k.a Midosho sort of things). Usivae ili kupata attention(na wewe umo kwenye fashion), vaa ili kuwa Msafi, Uvutie na uwe comfortable.

Vaa Suruali ya kitambaa (nyepesi) only kama unaenda kwenye Mahojiano ya kazi/masomo/kuchumbia vinginevyo wekeza kwenye Suruali "nzito".

Mie sio mtaalam wa Mavazi, nikikushauri kuhusu hilo hapa nitakuwa nakuambia uvae nipendavyo mimi kitu ambacho sio sahihi.

Sasa zoezi hili la kupata hali ya kujiamini likikamilika na ukaanza kujipenda na kuvutiwa na muonekano wako then njoo tuangalie namna ya kunasa wasichana.

Unasoma au kufanya kazi? Kama upo upo tu mtaani basi tafuta mahali pa kujishikiza ili kipato au kujitolea(kusaidia) lakini muhimu ni kupata uzoefu na kuongeza hali ya kujiamini kutokana na kukutana na watu wapya/tofauti na wale uliowazoea kwenye mzunguuko wako (ndugu, jamaa na marafiki).


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments