Anajua nina Familia lakini anataka nimuoe.

Pole na majukumu ya kazi Dinah
Mm ni kijana wa miaka 33 na nimeoa na nina mtoto mmoja

Awali nilikuwa na msichana kama friend chat wa kwenye mtandao na baadae tukapanga tuwe wapenzi but mwemzangu alikuwa bado anasoma. Kwahiyo kwa kipindi chote hatukuwahi kukutana kimwili.


Mwaka 2010 tulipoteza mawasiliano, mwaka jana alinipigia simu na kunieleza kwamba amesha maliza masomo na yupo tayari kuoana na mimi.


Ndipo nilimwambia ukweli kuwa mimi nina familia lakini yeye aliomba tuonane. Kusema kweli nampenda but ni Mkristo na siwezi kuvunja kanuni ya mke zaidi ya mmoja.

Yeye amekubali kuwa hata mke wa pili maana ananipenda je? nifanyeje na bado tunapendana?


***********


Dinah anasema: Ahsante na shukurani kwa Ushirikiano.


Watu kwa ku-complicate maisha ya wenzenu khaaa! Kama kweli mlikuwa mnapendana kitu gani kilikufanya uendelee na maisha mengine na hata kuanzisha familia?

Si ungesubiri "sikumoja atarudi", actually ungemtafuta kwa hali na mali huyo mwanamke wa mtandaoni na kurudisha mawasiliano kabla hujaongeza another life(mtoto) Duniani.


Umewahi kusikia kitu inaitwa "second best"...nitakupa a little real story ili yakuingie vema.

Kuna mdada alikuwa na bf Tz, yeye alikuwa akiishi Ulaya. Huko Ulaya akawa anakula maisha na wanaumbe mbalimbali yaani alikuwa akifanya umalaya.

Jamaa wa bongo akachumbia, Mdada akakataa kuolewa nae akidai bado yupo shule hivyo bora waendelee tu kuwa wapenzi wa mbali, mwanamke akapunguza mawasiliano na baadae kukata kabisa.

Jamaa kwavile alikuwa akimpenda aliendelea kuvumilia akiamini siku akirudi watafunga ndoa.

Miaka ikapita, umri wa mdada ukaenda akaanza kuwa desperate kuolewa lakini mwanaume aliekuwa nae Ulaya hakutaka kumuoa kutokana na sifa mbaya alizozisikia kuhusu huyo Mdada.

With desperation ya kuolewa na aibu ya wanaume wa Ulaya kumgwaya...akakumbuka kuna Bwege linampenda Bongo Tanzania.

Akarudisha na kukoleza mawasiliano na ku declare mapenzi kwa yule wa Bongo, akarudi Tz wakafunga ndoa na kwenda Ulaya kuanzisha familia.

Hana mapenzi na yule mwanaume lakini kwa vile alitaka kuolewa na kuzaa akaamua kuolewa na mwanaume ambae awali alimkataa na kukata mawasiliano.

Faida kwake ni kuwa Mwanaume hajui maisha ya yakimalaya aliyokuwa akiishi Ulaya na hafahamiani na watu wa huko hivyo chance ya kuyajua ni ndogo na hata akija kuyajua baadae atakuwa tayari kaolewa na anawatoto so itakuwa win win situation.


Miaka 12 baadae ndoa imekuwa ndoano, Mume keshajuana na watu na wanampa stori kuhusu Mkewe....jamaa kuuliza mkewe...mke akakubali kwa dharau na kumwambia ukweli kuwa ulikuwa "Second best"

.....mwanamke kabadilika (well karudia tabia yake), sasa wanaishi nyumba moja ili kukuza watoto wao lakini hawana mapenzi hata yale ya awali ya kuigiza kutoka kwa Mke mtu.

The end.****

Kama ungekuwa unamapenzi ya dhati kwa mkeo na mwanao usingeenda kukutana na huyo mwanamke pale alipoomba mkutane.

Baada ya kumuambia hali halisi ya maisha yako ya sasa na kuweka Msimamo wako wazi kuwa huna mpango wa kuwa nae achilia mbali kumuoa asingeshupalia kuwa Mke wa pili.

Inaonyesha ulitoa mwanya wa yeye kuolewa na wewe, maana umesema "amekubali kuwa mke wa pili", hukupaswa kutoa mwanya wowote wa kutaka uhusiano na huyo Mwanamke.


Nia yake hapo sio kuwa mke wa pili kwani anajua haiwezekani, "anachomaanisha ni kuwa iterekeze familia yako unioe mimi".


Wanaume mjifunze kuwa na msimamo, sidhani kama kuna mapenzi hapo kama kungekuwa na mapenzi juu ya huyo mwanamke ungepigana na kufanya lolote ili "asipotee" kwenye 18 zako, ungeenda hata kwao.... lakini you moved on quiet kirahisi na kuanzisha familia.


Futa mawasiliano na huyo mharibifu wa familia za watu (wapo wengi kama yeye) focus kwenye familia yako, ipende, itunze, ithamini na kuijali ili uishi maisha marefu.


Fainali uzeeni, unamiaka 33, mke na mtoto bado unahaha na kupoteza muda na hizi mambo za "mapenzi ya mtandaoni" hebu piga kazi ili kuwekeza kwenye Elimu ya mwanao.


Kesho-keshokutwa umerudisha namba, nani atamsomesha mwanao? Ona mbele sio umbali wa Miguu yako ukiwa umesimama.

Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments