Mapenzi na Kazi, unakabiliana vipi?

"Mimi ni msichana wa miaka 24, nimekua na mahusiano na boyfriend wangu miaka mitatu sasa mwaka wa kwanza tulikua na matatizo kutokana na Ex wake aliyekua anamng'ang'ania na kuwashirikisha ndugu wa mwanaume ili wamsaidie arudiane nae.


Bahati nzuri mpenzi wangu ni mtu mwenye msimamo kidogo haku-fall kwa hilo na yote niliyavumilia..kama wapenzi tumekua na ups and down na tumevumiliana nimeshafanya makosa sana lakini bado ameendelea kuwa na mimi.

Tatizo linapokuja hapa, mpenzi wangu ameajiriwa na mimi bado nipo Chuo ila Ofisi yao ilitangaza nafasi za kazi za muda mfupi akani recomend nikapata kazi ila akasema tuseme sisi ni marafiki maanake Ofisi itaona amemtafutia kazi mpenzi wake kitu ambacho sio kizuri.


Nikakubali manake kazi yenyewe ilikua ya muda, kuanza kazi pale nikakutana ma mdada ambaye anampenda boyfriend wangu though my boyfriend anamchukulia kama rafiki. Yupo nae close and all that.


Siku moja tukatoka Out kama Ofisi, kwa vile tumeamua kufanya mahusiano yetu yawe siri hata siku hiyo tukashindwa kuwa pamoja matokeo yake akawa karibu na wadada wengne wa Ofisini mmoja wapo akiwa huyo anayempenda my bf.

Kwa hasira nikaishia kunywa pombe hadi nikapoteza kumbukumbu kabisa nikarudishwa nyumbani na my bf na he took care of me. Nikajisikia vibaya mno kwa nilichokifanya.


Kesho yake akanambia nililewa nikafanya ujinga kitu ambacho sikumbuki, akasema nimemuumiza sana na kwa mara ya kwanza akalia. Najua nilifanya makosa na hiyo ikawa mwisho wa kunywa pombe!


Siku hiyo tukaamua kuachana ila tukawa tunaendelea na mawasiliano, ikapita kama Mwenzi tukaanza tena kulala pamoja but kipindi hiko haikua serious sana.

Nikawaza vile mimi ndio nilikua responsible kwa uhusiano wetu kuvunjika basi ntavumilia tu ikapita kama three months tukawa sawa and tokea hiyo incident ni mwaka sasa.


Tatizo ni lile lile hataki watu wa ofisini wajue uhusiano wetu japo ndugu zake wote na marafiki zake wote wanajua uhusiano wetu. Kipindi hiki nimerudi tena kufanya hapo kazi anadai wanawake wa pale Ofisini anawajua vizuri wakijua sisi ni wapenzi sitafanya kazi kwa amani, kwamba kutakua na maneno sana ila siku itafika watajua tu ukweli.

Nampenda mno namuamini pia ila kwenye hilo suala linakua chanzo cha ugomvi kati yetu wakati mwingine. Nakua njia panda

Nishauri dada yangu. And sorry kwa maelezo marefu."


*******

Hello there, usijali maelezo marefu yaliyokamilika nayapenda na ndio huyafanyia kazi. Shukurani sana kwa ushirikiano.

Hapo kuna mawili-matatu! Moja inawezekana Mpenzi wako alikuwa na Uhusiano na mtu ambae bado yupo hapo Ofisini au Mkubwa wake wa Kazi hapendi wafanya kazi wawe na wapenzi wao mahali pa kazi(kuepusha uzembe na kupendeleana) na mpenzi wako hataki upoteze kazi.....(Fanya uchunguzi hapa, usikurupuke ukakosa vyote).

Pili, Mpenzi wako hataki ijulikane kuwa wewe ni mpenzi wake na hivyo kasaidia au alisaidia wewe kupata kazi pale ofisini kwake....kasema ni marafiki na labda baadae ukipata ajira ya moja kwa moja atajifanya amekudondokea na hapo kuanzisha uhusiano(wakati ukweli mnaujua wenyewe).

Ni vema mpenzi wako atambue kuwa kufanya uhusiano Siri wakati yeye anakuwa karibu na Wanawake wengine huku wewe ukishuhudia ni ngumu na inaumiza sana (anakunyanyasa Kiakili na Kihisia).


Kufanya kazi hapo ni muhimu kwako kwa ajili ya uzoefu na pengine ajira ya kudumu hapo baadae hivyo usilazimishe sana kujulikana na watu wengine hapo Ofisini (hawana umuhimu sana kama Ndugu zake) na hakika unaweza kupewa Ukweli(umbea) wa nini mpenzi wako alikuwa akifanya na mtu fulani hapo ofisini(tuseme ni Ex) na hapo kukawa na ugomvi au makundi na kufanya maisha ya kikazi Jehanam.


Muhimu ni kuzungumza na mpenzio na kumueleza unavyojisikia bila hasira, kisha wote kwa pamoja muelewane kuwa yeye apunguze au aache kabisa ukaribu na wanawake wote hasa yule ambae unadhani kuwa anampenda mpenzi wako.

Kama yupo serious na uhusiano wenu na mnapendana (mwambie) basi ni vema tukaweka Mipaka dhidi ya watu wa jinsia tofauti wanaotukaribia ili kusiwe na maumivu Kihisia na Kiakili.

Inawezekana kabisa kuwa na uhusiano Kazini kama Wafanyakazi na Wapenzi mkiwa nje ya Kazi ikiwa mtafuata hayo hapo juu.

Hili likishindikana basi ni vema mmoja wenu aombe uhamisho au abadilishe kazi.


Kila lililo Jema.
Mapendo tele kwako...

Comments