Kumuendekeza mwenza(wa Kiume)!

Unajua tunapoanza mahusiano huwa tunajitahidi kufahamiana na kujuana zaidi kabla hatujaamua kuwa -serious(Ku-ndoa-na).





Baadhi yetu hujitolea "Mhanga" na kwenda kujuana na kufahamiana baada ya kuwa serious(Ndoa-na kwanza mengine yanafuata).





Wachache huamua kuichukulia kila siku kama inavyokuja(hawa bado wanakua au wanaogopa kuji-commite baada ya kutendwa).





Jinsi siku zinavyokwenda ndivyo ambavyo kila mmoja wenu anajifunza jambo au mambo kuhusu mwenzie. Ukigundua kuwa mambo au jambo fulani linaweza kuwa Mzigo huko mbeleni ni vema kuliweka wazi na kulizungumzia kisha kutafuta Mbadala.





Baadhi huamua kuendekeza tabia za mwenza wakitegemea kuwa watabadilika....bila kujua huko mbeleni inaweza kuwa Mzigo. Mfano Uvivu ambao hupelekea mtu kuwa tegemezi, Ulevi au Uchafu n.k.





Baadae mnapokuwa na familia utajikuta unakuwa Single-mother with a husband, kwamba unafanya kila kitu kuanzia kazi za ndani mpaka kutafuta pesa ya Chakula na Matumizi mengine kwa Familia......ukidhani kuwa huko ndio kuwa "independent".





Nimelenga wanaume kwasababu ndio ambao huwa wagumu "kubadilika" kutokana na ile imani kuwa "mwanamke hawezi kunibadilisha" au "usikubali kubadilishwa na mwanamke".




Hakikisha unakuwa Msaada kwa mwenza wako ili awe kwenye mstari na msaidiane, kama hakueleweki....Mpige Mkwara.



Feels great to be Back!
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
Bora umerudi mwaya blog ilipwaya kweli