Condoms au Dawa za kuzuia Mimba

"Mke wangu anataka tutumie kondom, hiyo ni kweli? Nimeoa miaka 6 iliyopita, tumejaliwa watoto wawili wa miaka 4.5 na mwingine ni mwaka Mmoja.

Tangu tumepa mtoto wa pili, Mke wangu alianza visingizio kuwa yeye hatatumia njia nyingine za Uzazi tofauti na Condom kwani njia zingine zinamsababishia kuumwa Mgongo, Joto kali na mengine mengi.


Mie kutumia Condom najiona kana kwamba nipo na Changudoa, sipati raha hata tone, nimemueleza haelewi, nishauri nifanyeje?"

***********


Dinah anasema: Hello there! Ahsante kwa Ushirikiano.


Kabla ya yote unapaswa kutambua kuwa Raha/Utamu wa Ngono upo Akili(kichwani) na sio kwenye Uume, Uume ni kitendea kazi.


Suala la kuona kama upo na Changudoa kwasababu ya kutumia Condom ni Dharau kuu kwa Mkeo! Inamaana ukivaa Condom unapoteza mapenzi na hisia zote za Huba kwa Mkeo na hivyo unafanya tu ili kuji-relief?

Ikiwa Mkeo anasumbuliwa na Dawa za kuzia Mimba na kumfanya aumwe kama alivyokuambia hakika hawezi kukuelewa. Wewe kama mumewe ulipaswa kumuelewa na kumpa-support na kwa pamoja ama kukubaliana na matumzi ya Condom au kutafuta/jaribu aina nyingine ya Dawa za kuzuia Mimba.


Ikiwa kila dawa anazojaribu zinamsababishia matati kiafya ni vema kutotumia na badala yake mtumie Condom kama alivyo-suggest, kama hutaki na Nyama to Nyama ni muhimu kuliko Afya ya Mkeo basi kazibwe Mirija ili usiwezi kumtia Mimba.

Unapaswa kutambua Dawa hizo (baadhi) zinahomono na huwafanya wanawake wengi wapate "side effects" mbaya sana.

Wengine huwa wakali, wakatili, wazembe/wachafu, wanapoteza hamu ya kufanya mapenzi, wanapoteza hali ya kukupenda wewe, kujipenda wao au watoto, maumivu ya Kichwa yasiyoisha, kupata Hedhi kwa muda mrefu (miezi 3-9), Unene/Kujaa maji, Mapigo ya Moyo kuwa juu n.k.


Wanaume wengi (hasa Waafrika) mpo nyuma sana kwenye ku-support Wake zao kwenye matumizi ya Condom kwa kuamini kuwa Condom inazuia raha na "nimemuoa hivyo hakuna kutumia Condom"...Condom ni njia nzuri sana ya Kuzuia Mimba ikiwa njia nyingine zinasumbua.

Techology ya Condom imekuwa sana na mengi yamebadilika, kuna Condom nyepesi kama ngozi lakini Imara(hazipasuki)....explore aina za Condom Mwanaume, za bure waachie Wanafunzi na watu wasio na Uwezo.

Condom za leo haziwashi, sio nzito(lakini Imara), hazinukii kama mpira....nunua kulingana na mahitaji yako.

Wekeza kwenye Condom Mwanaume sio unashupalia Nyama to Nyama na kutojali matatizo ya Kiafya ya Mkeo utadhali Uhai wapo depends on Nyama to Nyama!


Mapendo tele kwako...

Comments

Kirungu said…
Dahhh mwanaume mwenzangu hapo umechemka mkuu.Katika vitu unavyo paswa kua makini navyo ndani ya ndoa yako ni pamoja na kujali afya ya mkeo.Kwanza hio condom huvai miaka yote ni kwa muda tu.na i get the feeling kwamba Mkeo pia kakushitukia sio mwaminifu ndio maana kakomalia uvae ndom, ask yourself why mtoto wa pili ndio uvae ndom?.Tena una bahati hata amekubali uvae ndom kwahio kama unaheshimu feelings za mkeo basi kubali tu.Nimeshitushwa na lugha mbovu uliyotumia kua ukivaa ndom unaona kama unatomba changudoa, yaelekea ndio michezo yako kununua dada poa.Nakushauri ukitaka kufaidi penzi la mkeo pamoja yuko bize kulea mtoto msaidie.wahi kurudi nyumbani, shirikiana nae mambo ya msingi,msindikize kama kuna sehemu unayotaka kwenda.Sio unakaaaa bar unarudi usiku unataka tu kutomba kavu wakati ushatia michangudoa yako thts is not accepatble.Hebu jaribu kumpa support atakuheshimu na kama ilikua tu uoga wa kupata magonjwa kutokana kutotulia kwako atakupa tu kavu au nyamanyama.Wake zetu wana hurumu sana, sisi tunachukulia poa tu hata kwenye serious issues acha kua selfish bro uta enjoy kwa mkeo , kwa ushauri zaidi check me up via kirungu6.7@gmail.com