Pale Mume anapoweka Password kwenye Simu yake....

Hi Dinah,
Kwanza kabisa nikupongeze kwa kazi nzuri. Mie binafsi blog yako imenibamba kweli na imenitowa kimasomaso kwa mambo mengi.


Nimepata elimu na nimnefurahia sana.
Mpendwa naomba kuuliza! Mie ni mwanamke mwenye Ndoa ya miaka Sita. Tulipo oana na mume wangu mwaka wa kwanza wa Ndoa yetu tulikuwa tunakaa Mikoa mbalimbali, yeye akikaa Lindi na mie Dar kwa sababu za kikazi.

Mungu alijalia mwaka wa pili akapata kazi Dar akahamia Dar, tuliishi vizuri na sikuwa na wasiwasi naye maanake niliona kama mwanzo wa maisha mapya kwa pamoja tukiwa chini ya dali moja.

Baada ya miezi kama Sita hivi mume wangu alibadilika na style yake ya maisha ikabadilika ikiwa hata marafiki. Hapo ndipo nilipo anza kutafuta kushika simu yake ili kujua kinachoendelea.

Duh amakweli usilolijua nikama usiku wa giza, nilipoanza kushika simu yake nilikuta ni kiwembe cha kutupa! Alikuwa na mademu wasiopungua 10 wengine amewasave kwa majina ya magari, hotels na kwa majina ya marafiki zake wa kiume.


Dinah niliunia sana nikakaa chini nikaongea naye nikamwambia madhara ya Umalaya ni nini? athali zake kwa watoto wetu akasema atajirekebisha.

Nikampatia muda akabadilisha namba kwa malengo ya kupoteza mawasiliano na wao, ila baada ya muda mfupi hali ile ilijirudia.

Kweli nilipitia kipindi kigumu sana kwa miaka yote hiyo. Mwaka jana nikamwambia kama simfai mie naondika na watoto wetu 2 ili yeye afaidi maisha anayoyataka .

Akapiga magoti akalia akaomba msamaha akasema ni company mbaya za shetani akaahidi ku cut-off marafiki na kubadilika kwa mambo yote niliyo mweleza.

Nikampatia nafasi aniambie kama kuna mapungufu kwangu aniambie nijirekebishe akasema tatizo ni yeye na nimpe muda.


Hivi sasa simu zake zote ameweka password, Airtel na Tigo na ameongeza line nyingine ya Airtel sasa dinah sina amani na simuamini kwani amekosa uaminifu kwa muda mlefu.


Nashindwa elewa kama ana-improve makosa yake kwa sababu ya password kwenye simu na naomba nielimishwe kuhusu matumizi ya simu ya mwenza ni mwiko kushika?


Au anafanya hivyo ili nisione kinachoendelea? Naipenda Ndoa yangu na na muomba sana Mungu anisaidie. Sipendi Talaka na kuachana imani yangu ya Dini hainiruhusu.

Nahitaji elimu jinsi ya ku- overcome haya maumivu na stress.
Natanguliza shukrani.

************


Dinah anasema: Ahsante na shukurani kwa Ushirikiano.


Sometimes watu wanamsingizia Shetani! Hapo Shetani hausiki kabisa ni yeye mwenyewe amejiachia kwa sababu ambazo anazijua mwenyewe.


Sasa hapa mie ndio huwa napata Hasira!!! Mumeo ni Malaya na umethibitisha lakini hutaki kuachana nae bali unataka to overcome Maumivu na stress za Umalaya wake. MWANAMKE mwenzangu!!!! Kweli?!! Kivipi(maana mie sijui)?


Kama Dini yako hairuhusu basi Sheria inaruhusu mkimama....Miaka Sita ya Kunyanyaswa Kihisia, Kimapenzi, Kimwili na Kisaikolojia juu ya Umalaya wa Mumeo kwenye ndoa haijakutosha tu....usije zeeka au kufa bila kujua nini raha ya Maisha.


Huwezi ku-overcome Umalaya wa mtu kwa kuendelea kuishi nae na kumuacha aendeleze Umalaya wake na kum-treat as if wewe ndio mwenye Makosa!


Huyo ni mumeo, sio boyfriend....baada ya kugundua Usaliti wake ungemuweka Chini ukiwa firm (sio unalia-lia), ungempa msimamo wako kwenye Ndoa yenu na unge-Demand kupima afya zenu na mabadiliko ya kudumu haraka sana or else!! Hakuna kumpa Muda.


Kama kweli anakupenda na anaitaka Ndoa basi angekuomba msamaha na angebadilisha tabia yake, SIO kubadilisha namba ya Simu na kuweka password.

Huyo mumeo hafai, hakuheshimu, hakuthamini na wala hakupendi.....yupo na wewe possibly kwasababu ya watoto au mambo mengine lakini sio Mapenzi.


Watu wanakaa kwenye Ndoa kwa sababu za Kikazi (status), wengine kwasaabu ya Miradi n.k.


Sasa usijedhania unapendwa sana na mumeo pale anaposhupaa na kulia kabisa usimuache....usikute analilia "mkate" kwamba Kazi yake inamlazimisha awe na Mke (kazi nyingi za serikalini).


Kuhusu Mumeo kuwa na line nyingi za Simu na kuweka "kiingilio" cha siri ni wazi kuwa anakuficha Mengi ambayo anajua ukiyajua basi utamkimbia.


Unapaswa kuhoji kwanini hasa anakuwa na line nyingi za Simu na kwanini anaweka "neno la siri"?....ni mumeo na unahaki ya kujua kila akifanyacho....hii ni 2014 sio 1994!!


Wengine huweka "neno la Siri" ili simu zao zisitumiwe na watu wengine hasa Makazini, wanaweza kuiba details za kibiashara au hata Picha binafsi na kuzisambaza Mitandaoni.


Hii isikupe matumaini, tayari unajua Mumeo ni Mshenzi hivyo uaminifu haupo so ni vema kupata ukweli kutoka kwake.

Kwa kawaida hakuna mipaka kati ya Mume na Mke linapokuja suala la simu ya Mkononi, kama mna-share kila kitu kama familia kwanini simu ya Mkononi iwe tofauti?!!

Tatizo lako ni kwamba humuamini tena Mumeo na kama hakuna Uaminifu kwenye Ndoa ni wazi hakutakuwa na Amani.

Mumeo anahitaji kubadilika na kukuhakikishia kuwa kabadilika kwa vitendo ili akusaidie kurudisha hali ya kumuamini tena.

Lakini Mumeo hawezi kubadilika ikiwa unam-treat unavyom-treat sasa(kutokana na maelezo yako).....anafanya atakavyo kisha anaomba msamaha....anapewa muda....anarudia tena mzunguuko uleule.

Nasikitika kuwa sina mbinu ya kukushauri ili ku-overcome Umalaya ya mumeo ambao ni very active.....kwamba sio alifanya miaka 2 iliyopita bali nafanya sasa hivi.
Labda wasomaji wasaidie.

Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
POLE bt mapenzi kwangu mie hayanipi shda kbsa kwa hpo nyuma yalinipa shda lkn sasahv mtu akileta upuuuzi n kibuti kwa kwenda mbele nilkuwa n boyfriend nkackia anacheat nikamuuliza akakana nksma potea hko sisamehe mtu msaliti mimi huo muda cna niwe nimeolewa cjaolewa nikijua unanisaliti kibuti fasta......unaumia lkn utazoea tu trust meeeeeee
Anonymous said…
mmh mimi nina shinda kama ya huyo dada na nimevumilia nimechoka nimehamua kila mtu awe na mambo yake ila bado tunaishi pamoja na kwa sababu ya watoto ila akilini napanga mambo yangu yakiwa vizuri nitamkimbia tu sitaweza kuteseka hivi.