Nilimuacha, sasa namtaka tena...

Natumaini umzima bukheri wa afya, dada Dinah mimi ni kijana ambae
nilikua na mpenzi na tulipendana sana ila nilimuacha kutokana na
Wivu wangu wa kijinga.






Sasa nina mawazo sana kwasababu bado nampenda kiasi cha kunifanya nisongwe na mawazo mpaka kufikia kuumwa.





Bado namuhitaji mpenzi wangu ila sijui nianzie wapi maana alinivumilia
kwa visa vingi nilivyomtendea na sasa ameamua kunisahau kabisa.




Tafadhali dada dinah naomba unishauri nifanyaje maana naumia sana na
nahitaji turudiane.


***********


Dinah anasema: Namshukuru Mungu, ansante kwa ushirikiano.



Kuna msemo huku unaenda hivi "She will love you, she will cry, she will ask why, she will hate you, she will forgive you, she will love you again.....but one day she'll go and never come back".





Mtu anaweza kuvumilia visa na vituko lakini ipo siku moja akipata "akili" ya kuondoka au kwa bahati nzuri akaachwa kama ulivyofanya wewe inakuwa ngumu sana kurudi(anagundua kuwa alivaba/kosea).....inakuwa lucky escape!





Kwasababu sijui nini hasa kilipelekea wivu wako wa kijinga na hata kumfanyia visa na hatimae kumpiga buti itakuwa ngumu sana kukupa ushauri wa nini cha "kujaribu" kufanya ili umshawishi akubali kurudi kwako.




Kabla hujaanza harakati za kuenda "kumuimbia" misamaha ya kamosa(vile Visa) ni vema kuhakikisha kuwa umebadilika na kujiamini moyoni(na akilini) kuwa hutorudia tena makosa yako kwake (akikubali) au mwanamke mwingine hapo baadae(akikukataa).





Kama unampenda kweli basi pigania penzi lako kwake haraka kabla mwingine hajawahi akamsahaulisha wewe.




Akikataa kubali kuwa sio mwisho wa Maisha yako(huitaji mtu, unahitaji hewa/chakula na maji), ipo siku nyingine utakutana na mwingine na kutokana na ulichojifunza huenda utam-treat vema zaidi huyo Mpenzi Mpya mtarajiwa.



Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments