Mume Mbishi au apenda Changamoto?

Hongera kwa kuokoa Ndoa za walio wengi mimi ni mfuatiliaji wa blog yako kwa muda sasa na ninapenda saaana kazi zako. 

Kiufupi mimi ni mwanamke nimeolewa miaka miwili iliyopita na nimebahatika kuwa na mtoto mmoja. Naomba ushauri ambapo sijui tatizo ni la kwangu au ni la mume wangu au ndio kukosa hisia!

Ni kwamba nahisi Mume wangu hana hisia nami kwa sababu zifuatazo;

1. Huwa hanisikilizi kama zamani na amekuwa mbishi kupindukia anaweza kubishana na hata mtu mzima kumzidi, mimi ndio usiseme.

***********

Dinah anasema: Mumeo amekuwa na huenda Upeo wake umepanuka kwamba anauelewa wa mambo mengi kwa undani kuliko ilivyokuwa awali (mlipokutana).


Kubishana sio tatizo kwani inakusaidia kuweka wazi Mawazo yako wazi kuhusu issue inayozungumziwa, muhimu ni yeye kutoa nafasi ya kukusikiliza na wewe umpe nafasi ya kujieleza(weka mawazo yako wazi).

Kuhusu kubishana na mtu mzima kuliko yeye ni dalili kuwa anajitegemea kiakili na anajua kuwa anahaki ya kusikilizwa na kuweka maoni yake wazi....kuna watu wanapenda "debate"....ni sehemu ya "character" yake kama yeye.

Jaribu kuzungumza nae na kumuambia tabia yake ya kubishana kuhusu kila jambo haikupendezi na inakunyima amani, ni vema mjifunze kuzungumza (kuwasiliana) kama Wenza.
*************

Anaweza kuondoka na asiseme anakwenda wapi kwa kweli mimi huwa ananiudhi inafikia hata kipindi namchukia.

**********


Dinah anasema: Hili pia ni suala la kuzungumza na Mumeo na kumuambia kuwa ni muhimu kuanga na kukuambia anakwenda wapi na kwasababu gani ili kukuondolea hofu na usumbufu wa akili kwani Dunia inamengi na lolote linaweza kutokea muda wowote na wewe usijue kama Victim ni Mumeo au la!
***********


2. Hana shukrani hata upike vizuri kiasi gani, upambe chumba au hata nijipambe mwenyewe hawezi kunisifia sasa huwa sijisikii vizuri pale ninaposifiwa na watu wengine wakati wa kunipa faraja ni yeye....ila utamsikia mmh leo mmmh leo. 

*********

Dinah anasema: Huenda alipata Malezi mabaya, hakufundishwa manners nzuri(na muhimu Maishani) ambazo kila Mzazi anapaswa kumfunza mwanae tangu akiwa Mdogo nazo ni Kushukuru, Kuomba, Kusalimia, Kuaga, Kubisha(Hodi) n.k.


Kwenye kukusifia kuhusu Muonekano wako sio muhimu ailimradi tu mwenyewe unajijua umependeza, lakini kama kwako ni Muhimu na inakufanya ujisikie vizuri au kukufanya ujiamini basi weka wazi kwake mnapozungumza au mkumbushe(kama anajua anapaswa kukusifia ukipendeza).

**************


3. Hanifikishi kama zamani, siku hizi akipiga kimoja hoi ndio nitolee hiyo wakati mwanzo alikua anaenda hata round nne kwa siku na si za masihara ni za ukweli!


**********


Dinah anasema: Jinsi siku zinavyokwenda Mwili wa mwanadamu hubadilika! Hivyo inawezekana mwili wake hauwezi tena au anahitaji "kuhamasishwa" zaidi baada ya hicho kimoja. 

Halafu pia Wanaume wengine huwa Hodari wa Mizunguuko pale mwanzo wa uhusiano ili mwanamke usikimbie....na vile mnaonana mara chache basi "anajitunza" mwenyewe ili akija au ukienda mfanye mapenzi kufidia siku Saba zijazo na Saba zilizopita!

Lakini baada ya ndoa anakuwa na uhakika wa kukupata muda wowote hivyo haitaji ku-show off "uhodari" wake ana-relax a bit. AGAIN....zungumzeni kuhusu hili pia na mkubaliane kurudisha "moto" kwenye uhusiano wenu.
************

4. K yangu ni ndogo sana inanifanya hadi niumie kila wakati hata kama mume wangu ataniandaa kwa masaa matano mwisho wa mchezo naambulia maumivi sasa tatizo sijui nini? 


***********

Dinah anasema: Sasa mrembo walalama Mizunguuko Michache, hapa unasema unaambulia Kuumia, huoni hicho kimoja ni afadhali kuliko viTano eti?!!


Hakuna Uke Mdogo linapokuja suala la kufanya Ngono ailimdari kuna Ute wa kutosha Nje (mwanzo wa Uke) na ndani kusaidia Uume kuingia na Misuli ya Uke ku-relax jinsi anavyoingia taratibu(hatua kwa hatua).

Lakini kutokana na yote uliyoelezea hapo juu ni wazi kuwa unapoteza hamu ya Tendo hivyo hata akikuandaa kwa muda mrefu Misuli ya Uke wako inashindwa ku-relax kwasababu wewe huja-relax akilini kutokana na maudhi ya Mumeo.

Kumbuka kupata Ute sio kielelezo kwamba upo tayari kwa Tendo (kuingiliwa)....jaribu kumaliza issues zenu kwa kuzungumza na kuelewana ili wote kwa pamoja muweze kufurahia Ndoa yenu.
**************

Kiufupi da dinah nampenda sana mume wangu na sitamani kumkosa ila kwa tabia sijui hata nitamrekebisha vipi.

Na nikimkubaria kila kitu anasema simpendi kwa nini niwe namkubalia kila nachosema na nikimkatalia pia  ni hivyo hivyo nifanye nini jamani au mimi ndio namkosea sijui jinsi ya kuishi nae?!!

**********

Dinah anasema: Ahsante Mrembo, shukurani sana kwa ushirikiano.


Nimejitahidi kujibu kila swali papo kwa hapo ili nisikuchanganye.


Hilo la mwisho nitalijibu hivi:- Wanaume wa Kisasa wanapenda Changamoto, hawapendi ile "ndio bwana" kwenye kila jambo kwani haiwasaidiii.


Kama nilivyogusia awali, inaonyesha Mumeo amepanuka kiupeo na ana-enjoy changamoto au anataka kupata Maoni yako kuhusu jambo analokuambia.

Hategemei kukubaliwa au kataliwa moja kwa moja/haraka hali ambayo wewe unadhani ni "umbishi".


Ndoa yenu haina Mawasiliano na inaelekea hamkujipa nafasi ya kujuana zaidi kabla ya Ndoa, matokeo yake kila jambo unaona "jipya".

Kuwa pamoja kwa Muda mrefu kabla ya Ndoa sio kithibitisho cha kujuana zaidi (usichanganye), bali Uwazi kwenye kujieleza kuhusu Malezi yenu, Wepesi wa kuhoji, Uhuru wa kuweka wazi au kuonyesha "good manners" n.k.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments