Mimi;Nakupena..Yeye;Usijali

Shikamoo dada dinah! Mimi ni mwanamke na nilikuwa ktk mahusiano for 4years but nikaachana na ex wangu sababu alikuwa ananicheat sana.

Sasa kuna mkaka ambaye nilikuwa namjua na tulikuwa tunasoma Chuo kimoja japo yeye alikuwa amenizidi na alikuwa anachukua Masters.


Alikuwa ananifatilia wakati wote huo lakini mimi sikuwahi mkubalia kwasababu nilikuwa kwenye mahusiano na yule Ex, baada ya kuachana nae tukaanza kuwasiliana serious kama mwezi mmoja hivi.


Siku moja akaniambia niende kwake, nilipofka akataka tufanye mapenzi mimi nikamwambia nahitaji kumjua zaidi na japo kucheck afya! Akataka tufanye kwa kutumia Condom but mimi nilikataa.


Sina nia mbaya na yeye ni kweli nampenda halafu dada mimi ni muaminifu sana kwenye mahusiano. Nilivyokataa ku do naye akasema sawa, tulikiss na kunishika shika.

Toka siku ile hapokei simu zangu na msg hajibu. Kuna siku nikamtext kumueleza kuwa nampenda sana akajibu in short akasema usijali!

Kiukweli naumia sana na mimi nampenda huyu kijana sasa simuelewi nimemuomba tuonane tuongee hajajibu chochote.

Dada chonde nisaidie nimekosa raha kabisa sielewi nia yake ni kunichezea au? Na mimi sio kwamba siko tayari kushiriki penzi naye but nahitaji nimjue vizuri then mengine yafuate.
Asante.


******

Dinah anasema: Marhabaa mrembo, ahsante kwa ushirikiano.


Mmeanza kuwasiliana kwa umakini kwa mwezi mmoja....unauhakika kweli unampenda huyo Mr Masters au ume-miss tu kuwa na mpenzi baada ya kuachana na Ex na huyo jamaa akawa easy target kwasababu alionyesha kukutaka?


Miaka minne ni mingi sana kuwa kwenye uhusiano wa Kimapenzi na ku-get over uhusiano wa muda mrefu hivyo huchukua Muda zaidi ya mwaka! Haya ni muda gani umepita tangu umeachana na the cheater one?


Pamoja na kuwa unasababu nzuri sana ya kukataa Ngono (hongera kwa Msimamo Mzuri) bado inaonyesha upo needy na unaharaka ya commitment kwa sababu umemwambia unampenda mapema sana, huwezi mpenda mtu ndani ya mwezi mmoja tena baada ya kutoka kwenye uhusiano wa muda mrefu.


Sio tu inauma kumwambia mtu unampenda alafu yeye anakujibu "usijali" au "ahsante" inakufanya ujihisi aibu mbele yake na pengine kujiamini kunaweza kupungua kimtindo!


Ni wazi kuwa jamaa hajaanza kujisikia "anakupenda" as in "I love you" yaani penzi halijamvaa kama unavyodhani ila anapendezwa au kuvutiwa na wewe as in "I like you a lot".


Kiswahili hakina maneno mbadala ya kuwakilisha hisia kabla, labda napendezwa nawe ilikuwa sahihi zaidi ya "nakupenda".

Tangu kaamua kukuchunia basi ni vema na wewe kuuchuna na kuangalia ustaarabu mwingine.

Kuwa cheated on alafu kujibiwa hivyo hakika inaweza kukukatisha tamaa kabisa na suala zima la Wanaume au unaweza kuamua "liwalo na liwe" kwamba unakubali mwanume yeyote atakaejitokeza ili kujihisi vema moyoni na kujirudishia kujiamini.....(Utajiumiza zaidi).


Unahitaji muda kupumzika kabla ya kuingia tena kwenye mahusiano ya Kimapenzi. Achana na huyo Mr masters.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments