Hanitaki kwake kisa Ex ni rafiki wa Dada'ke!

Habari za kazi pia pole na majukumu, hongera kwa kazi nzuri ya kutushauri wadau, mimi nikiwa mmoja wao!

Dada dinahicious mimi ni mwanamke umri wangu ni miaka 30 kwanza napenda kukufahamisha kuwa nimepitia mahusiano kadhaa ingawa sio mengi kihivo!

Tatizo langu linalo nisumbua sasa kwa huyu bwana niliyenae ni hili, nimeanza mahusiano nae ya kimapenzi mwezi wa Kwanza mwaka huu 2014 hadi leo hii tarehe 18.8.2014 ninavyoandika mail hii tuna miezi 7 na wiki kadhaa ingawa tumefahamiana tangu mwaka 2009.


Mwenzangu ana umri wa miaka 38, wakati tunaanza mahusiano alinieleza kuwa alikua na mke na akabahatika kuzaa nae watoto 2. Waliacha kutokana na sababu zao ambazo alinieleza nikaridhia ingawa kwa maelezo yake ni kwamba sababu za kuachana ni Usaliti wa mkewe.

Kabla ya kuanzisha mahusiano na mimi tulika tukiheshimiana sana mwisho wa siku tukaamua kuwa wapenzi kwa kifupi historia yake ni hiyo na hakunieleza kitu kingine zaidi ya suala la kuachana na aliyekua mke na mama wa watoto wake.


Nami pia nilikua nimeachana na mpenzi wangu takribani mwaka na miezi kadhaa nilikua naishi mwenyewe, ila tatizo linalonisumbua ni kutopajua anapoishi hadi hivi ninavyo andika email hii kwako!

Tulienda na hali hiyo baada kufikisha miezi 2 nilishindwa kuvumilia maana nilistaajabu kuona hakuna siku aliyoniambia karibu nyumbani kwangu na hali yeye anafika nyumbani kwangu na yupo huru sana.


Nikamwambia naomba nipajue unapoishi akasema utapajua usiwe na shaka na akaniambia kupajua anapoishi sio defence ya mahusiano yetu natakiwa kuangalia moyo wangu unasema nini kwake na moyo wake unasema nini kwangu na kusisitiza kua ananipenda na anamalengo.


Baada ya hapo alinifahamisha jambo linalomfanya ashindwe kunipeleka kuwa baada ya kuachana na mkewe alijikuta anaanzisha mahusiano na msichana ambaye hakutaraji pia hakua na malengo nae msichana huyo.

Aliniomba msamaha kwa kutonifahamisha hilo, alinisihi sana nisimwache pia akaniomba nitulie anitengenezee mazingira salama na akadai pale nyumbani anaishi yeye na wadogo zake 2 moja wa kiume na mwingine ni wakike hivyo binti aliyeanzisha mahusiano nae anaurafiki sana na mdogo wake wa kike hivyo mara nyingi huyo binti amekua akipendelea kwenda pale nyumbani kwa sababu hawakai mbali sana.

Yeye kuishi na wadogo zake aliniambia mapema pia akasema anawaheshimu wadogo zake hivyo nimpe muda asitishe mahusiano na yule bila kutumia nguvu nyingi.


Kiukweli nilimwelewa sikuendelea tena kumuhoji kuhusu hilo, tumeendelea na mapenzi hadi mwanzoni mwa mwezi wa 8 mwaka huu nikaona suala hili linaniumiza sana kichwa pia nimejikuta natawaliwa na hasira sana wakati mwingine.


Nikamkumbushia tena kuhusu kupajua anapoishi bado akanisihi niwe na subra na kwamba amejitolea kua nami hakuisha maneno akaniambia mapenzi ni ghalama na amejitoa sadaka kwangu na kauli hiyo alikua anapenda kuitumia toka tunaanza mahusiano mara ya kwanza nilikua simwelewi mara nyingi alikua akiniambia unajua nimejitoa sadaka kwako kwa lolote.


Wakati mwingine ananiambia unajua mapenzi ni ghalama sana kwa siku hizo nilikua simuelewi ila nikaja kumuelewa alichokua akimaanisha kiukweli inaniuma sana na nimekua nikitawaliwa na hasira kila ninapolifikiria suala hili. Nimekua nikijiuliza maswali mengi sipati majibu.


Ingawa nakiri kwa kipindi chooote ambacho nipo nae kama mpenzi wangu amekua karibu na mimi sana ananijali na haijawahi pita siku bila kuonana usiku kabla ya kulala tunawasiliana.

Yeye ni mtu ambae amejiari anaofisi yake na mimi pia ninafanya kazi katika kampuni moja ambayo haipo mbali sana na ofisi yake hivyo kwa kipindi chote hicho nimekua nikitoka ofisini kwangu napitia ofisini kwake nakaa then naondoka zangu pia huwa hasiti kunitambulisha kwa watu wake wa karibu hususani marafiki zake.


Huwa tunatoka mara nyingi hasa siku za Jumamosi na Jumapili baada ya kutoka Ibadani kuanzia saa 3 huwa tunakua pamoja hadi usiku saa 5 ndio ananiaga anaenda zake kwake.

Ananipa treatment kama mke na kila anaponiona nimebadilika na kua na hasira hua haishi kunisihi nimvumilie hatanitenda kama nilivyo kueleza hapo juu kua suala la kutopajua anapoishi linaniuma hivyo nimejikuta nikiwa mtu wa kutawaliwa na hasira hasira hasa nikikumbuka.


Tafadhali naomba ushauri wako dada dinahicious pamoja na wadau kulingana na jinsi nilivyo jieleza kichwa kinaniuma stress tupuuu,


Samahani kwa maelezo marefu.


***********


Dinah anasema: Habari ni njema, ahsante na shukurani kwa Ushirikiano.


Ni rahisi sana kwa mwanaume (mume) kusema "nimeachana na mke wangu kwasababu alinitenda" lakini ukweli ukawa yeye ndio Msaliti mkuu na wewe ndio unaefanikisha Usaliti huo....Kwamba hajaachana na mkewe as in kupeana Talaka.

Ndoa yake ni ya Kikristo? Ndoa za Kikristo huwa hazivunjiki kutokana na "Maandiko" yao hivyo utakuta Mke/Mume anaendelea kuishi tu na Mume/Mke ambaye ni Msaliti.

Sioni umuhimu wala sababu ya wewe kupata hasira kwasababu hukujui nyumbani kwake....,adhani ungepata hasira kwanini yule binti (ex) bado anauhusiano na Jamaa na anaendelea kwenda kwake kwa kisingizio cha Urafiki na Mdogo wake!!

Tena kakuambia kabisa anataka "kumalizana" nae taratibu na wewe ukamuelewa REALLY?!!! Moja haku-declare kuwa na ka-ex (baada ya Mke) THEN I mean pili anakuambia "anataka kumuacha tataribu" kwa kigezo cha " "uwifi" kati ya mdogo wake na ex.


Kuna mawili nayaona hapa: Mosi, hajaachana na Mkewe ila anampango huo(wana issues zao kwenye Ndoa yao). Anashindwa kukupeleka kwake kwasababu hataki Ugomvi na Mkewe na hataki kuwachanganya na kuwaumiza watoto wake kihisia.


Hivyo anatafuta visingizio kila leo kwani hataki kuwa mkweli kuhusu familia yake, hasa watoto wake kwako kwasababu anahofia kuachwa. Ukimuacha wakati hana maelewano na Mkewe atakuwa kakosa kote.

Ujue, kuna baadhi ya wanaume waoga sana kuachwa hivyo akiona dalili za kuachwa na Mke, huwa anatafuta mtu pembeni just in case..... Ndoa ikibuma anaendeleza huko nje bila ku experience upweke(sijui unanielewa?).

Pili, anauhusiano na huyo Binti rafiki wa dada yake na wakati huohuo anauhusiano na wewe.....aka Malaya!


Suala la kukaa na wewe mpaka Late usiku na kuondoka sio kielelezo cha Upendo au Uaminifu! Anaweza kutoka kwako muda huo na kwenda kwa Mkewe au yule rafiki wa dada yake pale Nyumbani kwake.


Kuwa treated kama Mke ndio kukoje kwani? Ikiwa Mkewe anam-treat kwa kutokuwa nae muda wote anapokuwa na wewe....utasemaje anaku-treat kama Mke?

Sasa Mwanamke, ili kujua ukweli wa nini ni nini hasa ni vema kufanya Uchunguzi bila yeye kujua.

Mfuatilie nyendo zake anapokwenda kwake ili ujue nyumbani kwake ni wapi hasa, kisha kuwa Detective.... Siku nenda pale kwako ukijua hayupo na ukajitambulishe kama Mfanya biashara mwenzie au rafiki yake na una-deals au mmepanga kukutana hapo kwake!

Ukipata nafasi (ukikaribishwa ndani) au hata kwa nje, jaribu kuwa Mcheshi na kuhoji uliowakuta kiujanja....Mf: kama kuna binti na kijana unaweza kusema "wewe na huyu nani Mkubwa?"...."Baba yenu anapenda sana kuwazungumzia, anajivunia sana watoto wake"

Maelezo hayo (sio lazima yale kama yalivyo, tafuta ujanja wako mwenyewe wa kupata ukweli) yatawafanya au kumfanya mwenyeji wako kuwa comfortable na wewe.


Ana/wanaweza kusema Fulani(mpenzi wako) hana watoto au sisi sio watoto wake au watoto wake wapo blablah...


Kumbuka unachokifanya kinaweza kumpunguzia mpenzi wako Uaminifu kwako lakini unaweza kujitetea kwa kitendo chako (ikitokea umebambwa na alikuwa Mkweli).


Wewe ndio mwenye Mamlaka na furaha yako, mwenye uwezo wa kuchagua aina gani ya maisha unataka kuishi.....kama mtu mwingine anakusababishia usumbufu wa akili na haonyeshi kukuelewa au hamuelewani basi huna haja ya kupoteza Muda.

Wengine wataongezea....
Kila la kheli.
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
Pole kwanza.ila huyo bwana anaonekana ni muongo si mkweli na bado anaishi na mkewe..kukutambulisha kwa marafiki zake haimaanishi kua ni mkweli big NOoo hata hao marafiki zake nahis wanaku enjoy tu hakuna watu wanaofichiana sir km wanaume hasa hao marafiki aka Mashemeji...na pia isitoshe yy ndio chanzo cha matatizo na mke wake kisa tamaa zake.i had the same scenario nikaja jua na mke na mtt na bado anakaa na mkewe wanaume ni waongo mnooo.kua makini mfatilie utajua ukweli.
Anonymous said…
Huyo anatafuta sehemu ya kupooza stress zake hana mpago wowote na wewe. Kama angekuwa mtu mwema angekupeleka nyumbani ufahamiane na ndugu zake, kutambulishwa kwa marafiki ni jambo la kawaida kwa kila mwanaume kutambulisha michepuko yako jamani nani hawajui wanaume wanavyojuana kwa vilemba? dada mwenzangu angalia maisha yako huyo jamaa anatafuta kipoozeo tu mpendwa.
Anonymous said…
Rafiki kimbia mbio ndefu kweli maana huyo mpenzio huko nyumbani ana mke au mwandani mwingine. Ngoja nikupe kisa changu kifupi.
Nilienda kwenye sherehe moja nikakutana na mwanaume mmoja alivyoniona akawa kama amepagawa vile maana aliniuliza how are you na swali la pili likawa je umeolewa? Sherehe ikaisha kila mtu akashika ustaarabu wake. Siku si siku naona jamaa anagonga hodi kwetu.. mmh nikashtuka kapajuaje? Kumbe amenifuatilia wee kwa mwezi mzima.
Akajieleza akanipeleka kwake nikapaone.. akadai anaishi na dada ake ambaye amesafiri atarudi baada ya miezi miwili. Namshukuru Mungu mi si mkurupukaji sikuwa na boyfriend (mjane) na sikutaka boyfriend kwa wakati huo. Tukawa tu marafiki wa kawaida. Siku isiyo na jina mdada mmoja akanambia nimekuona na fulani jana 'mke wake' mshari sana. Nilishtuka kindani ndani nikasema ni rafiki wa kawaida. Akanisohi niwe makini.
Aisee kumbe dada alonambia kasafiri ni mkewe wa ndoa ya kanisani mpendwa.. ndo huyo kasafiri yeye ananambia ni dadaake.
Hata sikujisumbua kumuuliza.. nikamblock kila mahali na nikampiga marufuku kukanyaga kwetu la sivyo ntamshtaki.
Kuwa makini sana.
Anonymous said…
Tena isitoshe ni tamaa zake tu mke wake hana tatizo nae...kukupigia sim kabla hajalala saa tano obvious kwa mkewe hua anadanganya labda yupo ofisin anafanya kazi na hivi kajiajiri mke anaamini...na mpaka unakua huru kwenda hapo ofisin kwake ashajua mkewe kuja hapo ni mpaka kuwe na issue muhimu na hua anamwambia mume nakuja...huyo anakudanganya zaidi kutokana na mazingira ya kaz ya kujiajir hata hyo jumapili baada ya ibada atakua anamwambia mkewe nitakua ofisini namalizia kazi mbili tatu...km anakupenda kweli sikuvmsuprise mwambie hukubali unataka ukalale kwake uone atakavyoloa...mimi kuna mmoja alikua anadanganya hatak nipeleka kwake etu nitajisikia vibaya cz bado mke wake tangu wameachana hajachukua vitu vyake so ntajisikia vibya siku ya siku mke wake akanitafuta akaniuliza kiustaarab kweli nikamuelezea cz hakuaja kishar nae akanielezea kuabado anakaa na mumewe na hua akichelewa rudi anasema yipo kazini..huyoo ana mkeeee...
Anonymous said…
Jamani si kila NYOKA UMUONAYE NDIYE ALIYEKUUMA WEWE!! MIFANO YA YALIYOWATOKEA UNAZIBUZ MASIKIO NA MACHO ILI MWENZETU HUYU AJARIBU KUWA MCHUNGUZI ZAIDI KULIKO KUENDELEA KUDANGANYWA. MDADA UMEISHAPEWA VISA VYA YALIYOWATOKEA WENZAKO HIVYO NA WEWE ANZA KUWEKA MASPY ILI UCHUNGUZE MINAJIRI YA HUYO DUME WAKO USIJEINGIZWA MITINI.ILA UMENISHANGAZA ETI MNATOKA KANISANI NA MNAENDELEA KUBANJUANA SASA HUKO KANISANI HAKUNA HATA MNACHOJIFUNZA JUU YA MNAYOENDELEA KUYAFANYA GIZANI KUWA SI VIZURI.
Anonymous said…
pole sana my dia kwanza huyo jamaa ni mwongo na anakupotezea muda wako, pili inaelekea ww ni mvivu wa kuchunguza unakuwa na mahusiano na mwanaume muda wote huo hupajui anapoishi na anakupooza kwa kukuahidi kila cku then umeendelea kukaa kimya u cnt b serious aisee ebu anza kufanya uchunguzi kimya2 bila yy kujua utajua mengi na yaliokuwa chn ya kapeti ila utakavyokuwa unachunguza itabidi uwe mvumilivu kutokana na maelezo yako huyu mwanaume anakuficha mengi sana so utayajua ukianza kuwa mchunguzi wa kimya2 ila pole hayo yanatukuta wengi kikubwa ni kuwa makini tu