Penzi kwa Simu, Nikimuona Penzi Nywiii...

Habari dada dinah, natumai umzima na pole na kazi. Kwanza napenda kukupongeza kwa hii blog yako kwa kweli tunafaidika sana na tunajifunza mengi kutoka kwako nakupenda sana.


Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 24 naishi Dubai. Nimepata Mchumba ana umri wa miaka 37 na kakubalika nyumbani na tuko kwenye harakati za kufunga Ndoa.


Kwakweli huyu bwana ananipenda sana kupita kiasi . Ananijali na kunithamini na kuniongoza katika kila jambo na kunishauri mambo yake yote kuhusu maisha yake na kwa kila kitu kiasi ambacho kanisubiri muda wa Miaka mitano ili nimalize masomo ili anioe.

Kwakweli miaka yote hatuna tabia ya kutoka pamoja wala kuonana ila nimazungumzo kwenye simu tu kwa muda wa miaka miwili.

Anakuja kwetu kawaida na mie kwakweli namempenda huyu kwa jinsi anavyonipenda na kunijali na navutiwa naye sana nikiwa naongea kwa simu kiasi ambacho siwezi kukaa siku bila kuongea nae na siwezi kufanya jambo bila kumshauri yeye tu.


Lakini cha kunishangaza akija kwetu kuonana na mie Moyo wangu unabadilika nahisi kuwa kama sijampendaa huyu mtu!

Naomba usinielewe vibaya dada dinah kusema kweli dada dinah nikikaa nikifikiria kiakili nahisi  sijaimpenda sura yake kwakweli na kwajinsi nilivyo huwa inanijia kama tukitoka wote itakuwa vipi?


Ila moyoni nampenda sana na siwezi kumkosa kabisa. Kwakweli dada dinah nahisi nachanganyikiwa sijui nijiamulie vipi niufate moyo wangu au akili yangu?

Naogopa sana ikaja ikawa tatizo kwenye ndoa yangu na kutompa furaha anayoitarajia au je hili halitokuwa tatizo nikioana nae kwa vile Moyoni nampenda ntakuja kumpenda na kutojali sura yake.


Naombaa unisaidie dadaa dinah, nakupenda sana. Asante sana.


*********


Dinah anasema: Habari ni njema tu Mrembo, ahsante. Aah! Nakupenda pia kwa kunipenda sana.....shukurani kwa ushirikiano.

Hapo ni Je, kufuata Moyo wako au Macho yako?....Akili haihusiki.


Binaadamu tupo tofauti na tunapendezwa na mambo tofauti na wakati mwingine pia umuhimu wa vitu/mambo maishani ni tofauti.

Kuna ambao hawajali sura ya mtu bali tabia, wapo wanajali Mali/Pesa tu....wengine hujali Umbo zuri sio sura wala tabia, wachache hujali Umaarufu/mtindo wa Maisha....alafu kuna wengine ka' Dinah hapa ambapo vyote ni muhimu isipokuwa Umaarufu/Pesa/Mali!


Kama unahisi Sura yake inabadilisha upendo ulionao kutoka Mpenzi kuwa jamaa tu wa kushauriana nae basi ni vema kutafuta namna ya Kuizoea sura yake.

Kwa maana kwamba tumia muda wako mwingi kuongea nae ana kwa ana, tokeni pamoja na mfanye mambo pamoja mara kadhaa kwa Wiki halafu uone kama utaendelea kumuona "mbaya".

Kama baada ya mwezi, miezi 3 bado unajisikia kutokumpenda kila unapomuona basi ujue kuwa humpendi kweli bali unapenda Msimamo wake kimaisha, unapenda anavyozungumza na wewe, unapenda anavyoshauriana na wewe, unavutiwa na sauti yake n.k.


Yeye kukusubiri wewe kwa Miaka Mitano ili umalize Masomo ilikuwa Choice yake wala usihisi Hatia kabisa na wala isikusukume kwenda kufunga Ndoa nae ambapo unajua wazi hautokuwa na furaha kila ukimuona (yeye na sura yake).


Ndoa sio "kitu" cha kuingia na kutoka kama unavyotaka.....kama haupo tayari ni vema kusubiri kuliko kuingia kwa ajili ya sababu nyingine na sio Mapenzi.

Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
Amakweli mapenzi upofu