Mpenzi haniamini, nifanyeje....

Habari Dada Dinah,

Naomba ushauri wako nifanye nini katika hili! Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 27 na nina mpenzi ambae tumetokea kupendana sana kwa muda wa mwaka mmoja sasa.


Niseme tu ananipenda nami nampenda sana katika swala la tabia sio muhuni kabisa! Niko free na simu yake muda wote ni msikivu na tumepanga kufanya mambo mengi sana.


Tatizo kubwa lililopo hajiamini hata kidogo kutokana na historia ya
mahusiano aliyokuwa nayo huko nyuma kwani alitendwa sana.

Nimejaribu kumuweka chini na kumuelewesha na kujaribu njia mbali mbali za kumfanya awe na amani na mimi lakini naona bado tatizo liko pale pale, kiasi kwamba nakosa raha kabisa.

Mfano naweza chukua simu yangu labda nikamjibu Dada angu msg yeye anakasirika kiasi cha kupoteza maelewano kwa muda wa dakika kadhaa! Hili linanifanya mpaka nikiwa nae niweke simu mbali kwa kuhofia kutoelewana.

Dada Dinah tafadhali nisaidie katika hili sitamani kumpoteza na mimi
wala sio muhuni kabisa, akitaka simu yangu anapata muda wote tatizo bado
haniamini.


Anasema hawezi muamini mwanamke katika maisha yake! kauli hii huwa inanisononesha sana mpaka kuna muda nafikiria kuachana nae.


**********

Dinah anasema: Habari ni nzuri sana, ahsante na shukurani kwa ushirikiano.


Bila shaka kutendwa huwa kunampotezea mtu hali ya kuamini tena na humchukua mhusika muda mrefu sana (inategemea na mtu).

Wengi huwa hawajiingizi kwenye Mahusiano ya kimapenzi mpaka watakaporudisha hali ya kuamini mwanamke/mwanaume tena.

Baadhi hujiingiza kwenye mahusiano tena wakitegemea wapenzi wao kuwarudishia hali ya kuamini kwavile wanahisi wao peke yao hawawezi. Huyu mpenzi wako inawezekana kabisa ni mmoja wao.


Ni vema amekuwa wazi kwako kwa kusema kuwa hatomuamini tena mwanamke hivyo kama unampenda kweli na hutaki kumpoteza basi ajira ndio hiyo, fanya yote ambayo unadhani yatamrudishia hali ya kuamini tena, na zaidi kukuamini wewe.

Unajua unapokuwa na Mpenzi mpya mara zote unakuwa hujui Uzoefu wake hivyo unajaribu "kumfanya" asahau alikotoka incase aliepita alikuwa "Mkali" kwa kuwa mbunifu au kufanya mambo ambayo unadhani hajawahi kufanyiwa au kama aliwahi kufanyiwa basi sio kama unavyofanya wewe....yaani unaweka "Ustadi" wa hali ya juu ili apagawe!

Unabadilisha ufanyaji mpaka siku aseme "sijawahi kupata uzoefu huu" au "ktk maisha yangu hakuna aliewahi kunifanyia hivi" au "duh wee ni kiboko".....ukipata hiyo ndio unaanza kupunguza speed na kumpa mambo makali once a week au mwezi(inategemea na ujisikiavyo)....


Sasa basi hata kwenye kumrudishia mwanaume hali ya kuamini na kukuamini wewe unapaswa kutumia mbinu kama hivyo.....badala ya matendo kingono, fanya kitabia, onyesha kumjali, mshirikishe, onyesha kuwa unajivunia yeye unapokuwa na watu wengine, toka nae na uonyeshe affection kwake....sio lambanana ndimi na sura bali unaweza tu kumshika mkono, bega au kumpa nusu kumbato huku mnatembea, kaa nae 0-destance mnapokuwa nje n.k.


Punguza au acha mazoea yasiyo ya lazima na Wanaume(rafiki zake wakiwemo) via Simu au Mitandao ya Kijamii.


Pia tambua kuwa baadhi ya wanaume ni sensitive na wanaweza kuwa emotional at times(sio Ushoga) ndivyo walivyo tu. Wanaume kama hawa wakitendwa huwa wanahitaji kuhakikishiwa kuwa unawapenda, hutowatenda kamwe, uaminifu wako kwao n.k.

Yaani mara kwa mara wanahitaji kuwa reassured japo hawasemi, sasa tangu unajua tatizo liko wapi Mrembo jaribu niliyosema alafu uone kama kutakuwa na mabadiliko.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments