Ukaribu na Mpenzi...

Halo! vipi mzima dada?

Mimi ni mdada ambae nahangaika sana mwenziko, sina hata raha. Kuna mkaka ambaye mwanzo alinipenda sana, ki ukweli nami nilimpenda kwani ni Mstarabu sana na kila nimuombacho hunipa.

Ila sasa hanitafuti mara kwa mara yaani labda baada ya wiki kama mbili hivi ndio huwa ananitafuta. Nikimpigia na kumwambia anadai kazi nyingi na huko yupo kijijini.


Sometimes akija weekend ananiambia to meet but ni wa kwanza kubreak hiyo promise yaani ni Mr promiseless!!


Pamoja na kuwa ananipa chochote nitakacho bado nahitaji ukaribu wake kwangu sasa sijui hata nifanyajee please help
me.


Najua nakusumbua ila I know unajua more na unaweza nisaidia vizuri tu.

**********

Dinah anasema: Hello! Namshukuru Mungu mie ni Mzima. Ahsante kwa ushirikiano.


Kwanini uhangaike Mrembo wakati unajua kabisa mwenzio anahangaikia Maisha ambayo wewe pia unafaidika(anakupa kila umuombacho).


Natambua kuwa ukaribu na mpenzi umpendae ni muhimu na it feels GOOOOOOD lakini kuna kitu kinaitwa Compromises.....wakati mwingine kwenye maisha ya kimapenzi inabidi tujaribu kuwaelewa wenzetu na kukubali ku-compromise so long as Mpenzi alie busy hafanyi Ushenzi nje ya Uhusiano husika.....sio kulalamika na kufikiria na kujali hisia zetu pekee.

Kutokana na maelezo yako inaonyesha wazi kuwa Mpenzi wako anabanwa sana na shughuli zake na pengine anapokuwa mbali na Mji(kijijini) labda network inasumbua na anashindwa kuwasiliana nawe(umewahi kufikiria hili?).


Pia ni vema utambue kuwa kuna Umri fulani ambapo baadhi ya Wanaume hu-focus zaidi kwenye kuweka Maisha sawa alafu mapenzi ndio hufuata. Huenda Mpenzi wako ni mmoja wao.

Nadhani anadhani kuwa ni rahisi kwako kumuelewa akivunja promise kuliko Boss au Mama/Baba yake na hii inatokana na "priorities" zake.

Inawezekana kwenye priorities zake za maisha wewe unachukua nafasi ya 2 au tatu, kwamba kazi yake kwanza, familia yake pili na wewe tatu....au Kazi kwanza(Pesa), wewe pili kisha familia yake. Hii haina maana kuwa hakupendi bali umuhimu wako na kazi kwenye maisha yake vinatofauti(kwa sasa).

Pamoja na kusema hivyo ni vema mkipata nafasi mzungumze kuhusu hili, Mawasiliano yenu yatasaidia kila mmoja wenu kutambua umuhimu wake kwa mwenzie.


Wakati huohuo mkubaliane namna ya kuwasiliana, kwa kumwambia Mf; "sio vema kukaa kimya kwa Wiki mbili, tujaribu kuwasiliana mara kwa mara ili kuondoa hofu kwani siku moja ni ndefu sana kwa uhai wa mtu umpendae".


Uhusiano ukikomaa(kama bado) au mkiwa tayari kwenda "level" nyingine basi ukaribu utakuwepo bila kuuomba...namaanisha Ndoa au Kuishi pamoja kama "Trial" kabla ya Ndoa.


Badala ya kukosa raha kutokana na umbali (anapokuwa kazini) jaribu kufanya mambo mengine ambayo yatakufanya ufurahie maisha yako kama Mwanamke. Ikiwa huna Kazi/Shughuli basi tumia muda mwingi na familia yako, ndugu, jamaa na marafiki....hii itasaidia kukimbiza masaa na siku.

Kamwe usifananishe maisha yako ya kimapenzi na yale ya watu wengine au uyaonayo kwenye TV au usomayo kwenye Magazeti.

Kila uhusiano wa kimapenzi ni tofauti kwasababu wahusika wake ni watu tofauti hivyo hakuna uhusiano ambao ni sawa na mwingine na pia hakuna uhusiano ambao ni perfect kama uonavyo kwenye TV progs.

Usiizoeshe akili yako kukosa raha kwani itapelekea Depression na hivyo kuwa mtu wa huzuni(kukosa raha) tu kila kukicha.


Ni bahati kuwa na Mwanaume anaekupenda, Mstaarabu, Mchapa kazi na anaekujali(kukupa chochote utakacho)......Most men wana moja au mawili kati ya hayo.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
Thanks dada Dina ushauri wako mzuri unanisaidia hata mimi