Mke wangu na Jamaa, siwaelewi....

Dinah pole na majukumu pia usituchoke mimi ninamatatizo na Mke wangu ambayo yamepelekea kuwa Mlaji wa Milungi maana silali.

Inshu na Mke wangu ilianzia pale alipokuwa hanipi ushirikiano Kitandani na kila nilipo mwambia anasema kachoka. Nikahisi kunajamaa anamazoea nae yamepita kiasi, nikaanza kufuatilia mara nikakuta Vidonge vya kuzuia mimba.

Nilipomuuliza akaniambia havitumii vilikuepo kwa muda, mie sikuridhika na maelezo yake. Basi nikamwambia twende kweo lakini akataa, ikabidi niondoke pale kwenye ile nyumba nikarudi kwetu.

Mara akaja na yule jamaa niliekua namhisi na Mke wangu eti kaja kuchukua kifaa chake so jamaa kaja kumsaidia, wakachuka hao wameondoka sasa dada dinah hii inshu imeniathiri sana kwani nimetokea kumchikia sana mke wangu.


Hivi muda wowote namuacha coz kila nikimfikiria jamaa na Mke wangu nakosa hamu yakufanya Mapenzi, hata awe mwanake mwingine sitamani.


Mimi na Mke wangu tumezaa mtoto mmoja wa kike naomba ushauri wako please!


*************

Dinah anasema:Ahsante na shukurani kwa ushirikiano. Walaa sichoki, nikichoka nitafunga Blog.


Inshu yako imechichanganya....pale uliposema ukamwambia mkeo arudi kwao, akakataa kisha wewe ukatudi kwenu.....kwani mlikuwa mnaishi wapi? Hotelini au Mkeo anaishi na huyo Jamaa?....hata hivyo nitakujibu kama ifuatavyo.


Kutumia Vidonge vya kuzuia Mimba sio kosa kama Mkeo hataki kuzaa tena, haina maana kuwa anatoka na mtu mwingine.....inawezekana kweli ni vya zamani, kwani baadhi ya wanawake hubadilisha Vidonge pale wanapohisi kuwa haviwafai....Vidonge sio kielelezo cha kucheat.

Kutokukupa ushirikiano kitandani inategemea na shughuli zake za kutwa nzima, pia sio sababu kuwa anaridhishwa huko nje. Kuna wanaotoka nje na bado wanatoa ushirikiano wa kutosha na kuonyesha mapenzi tele kwa waume zao.

Nadhani kwenye uhusiano wenu kuna ukosefu wa Nguzo muhimu iitwayo MAWASILIANO. Unahitaji kuongea na Mkeo, sio kumuambia. Kaeni chini na mzungumzie issue ya Uaminifu na unavyojisikia kuhusu huyo Jamaa, uhusiano wenu, mapenzi yenu na Mtoto wenu.

Siamini kuwa humpendi Mkeo, ila unahasira ambazo zinapelekea kuhisi kuwa "humpendi" lakini ukweli ni kuwa humuamini tena kwa vile unahisi kuwa anatoka na Mwanaume mwingine. Hali hiyo inapelekea kupoteza hamu ya kuwa nae karibu kimapenzi....

Issue yako haina ushahidi wa kutosha kuwa Mkeo anatoka na huyo jamaa ila inaonyesha unampa nafasi(unamsukuma) ili atoke na huyo jamaa.

Zungumzeni....vyovyote itakavyokuwa rudi tena na ujibu maswali yangu hapo juu.


Uliuliza via Comment ndio maana sikuweza kurudisha mail ili ufafanue kuhusi maswali yangu pale juu.


Tafadhali tumia Email kuuliza na sio comments.

Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments