Misamaha Lukuki lakini wapi!

Hi dada,
Mimi ni binti wa miaka 25 na mfuatiliaji wa blog yako japo si sana. Nahitaji msaada.

Nilikuwa na mpenzi wangu miezi kadhaa imepita sasa, hatuwasiliani coz tuligombana. Nilijaribu kumuuliza tatizo la yeye kunichunia (maana yeye ndio aliacha kunitafuta ghafla) anasema hamna shida.

Nikajitahidi mtoto wa kike nikamwomba misamaha lukuki kwa kosa ambalo halijulikani,lakini wapi!. Nikashirikisha baadhi ya ndugu zake na marafiki....hamna kitu.


Mwisho nikaona ya nini nifeli Chuo mie nikakaa kimya. Lakini Moyoni bado nampenda sana, taratibu upendo ukaanza kupotea.


Juzi kati akanitafuta akiniambia kwamba "unajua kazi nyingi" nikaona huyu asinizingue, basi nikawa namsikiliza anavyonipa kesi ya kunitenga mara huyo akapotea.

Sasa tatizo ni kwamba kila ninapopata hisia za mapenzi nakimbilia kwenye Mtandao nasoma au naangalia picha za mapenzi basi nakuwa sawa kiasi, na hii tabia naona inakua na mimi sipendi mchezo huo. Ukizingatia kwa sasa Ex wangu wa ananisumbua sana na nahisi
nahitaji mapenzi .


Sasa ndio sijui nifanye nini. Naomba unisaidie.

*********


Dinah anasema: Hello there, shukurani kwa ushirikiano.


Hako kaeksi kako nako hakakuwa tayari na Uhusiano. Kutokana na maelezo yako nadhani "Ex" wako hakuwa anachukulia muungano wenu kama Uhusiano wa kimapenzi bali "company" kwamba mnatoka na pengine kufanya ngono....nothing serious yaani hakuenda mbali huko kwenye Uhusiano ambako wewe ndio ulikuwepo.

Unajua ni vigumu kwa mwanaume kueleweka kwa binti wa miaka 20nakitu akisema wazi "nataka niwe na wewe kwa ajili ya kutoka kila ninapokuhitaji, sitaki uhusiano".

Ila ni rahisi kumtongoza mwanamke kumapata kisha kuingia mtini kila anapohisi hakuhitaji.....siku akikuhitaji anakutafuta tena na kuomba msamaha au kukupa hadithi.


Kama unahitaji uhusiano serious basi achana nae na songa mbele na Maisha yako mpaka utakapopenda tena.


Kuhusu kukimbilia kwenye Mitandao kila unapojisikia Nyege sio kitu kibaya ailimradi unajua "limit" yako.....kuna wanawake wengi hufurahia Porn pia sema huona haya kusema.


Ila nadhani itakua vema kama utakuwa unajipa Mkono kuliko kutegemea Picha za X. Sio mbaya kujisaidia mara mbili-tatu kwa mwezi, inasaidia kukuweka vema Kingono na pia kuujua mwili wako zaidi kama mwanamke.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments