Ubora na Viwango vya Mpenzi!

Hi dada dinah, i have been your follower for quite some time now, though ukaja potea kidogo, naona umerudi and you are doing a good job. I would like to congratulate you for that.


Nina umri wa miaka 26 single and lonely, naomba ushuri kwa hili, nimekua napata shida sana kuanzisha mahusiano ya kimapenzi.


Am not sure whether my standards are very high or else. Currently nakaribia kumaliza my Masters Degree probably this december. Nina kikazi though hakilipi vizuri lakini siku zinaenda.

Natamani kuwa na mahusiano ya kimapenzi ambayo ni serious. Am not very outgoing person, ni mkimya sio muongeaji sana labda hiki ndicho kinachonifanya nisipate ninachokitaka.


Natumaini utanisaidia njia rahisi ninazoweza kutumia ili kuwa interactive mostly with girls. Hope you can keep my email private, thanks for your time.


***********

Dinah anasema: Ahsante sana na shukurani kwa ushirikiano (for being my follower....najihisi ka' Yesu vile hihihihi natania). Yeah nilipotea kwa muda mrefu sana, sikuwa na Muda wa ziada wa ku-blog.

Inawezekana standard zako zipo sky high lakini kutokana na maelezo yako nahisi kama vile ulikuwa/upo busy na Masomo + Kazi. Sasa unakaribia kumaliza unahisi presha imepungua na unaona umuhimu wa kuwa na mtu maishani mwako.

Wengi wetu kwenye umri huo kushuka chini huwa tunajiwekea "standard" na "quality" za watu ambao tungependa wawe wapenzi wetu.

Hivyo "Viwango" na "Ubora" hutusaidia kuvuta muda bila kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi.....kwasababu kila unaekutana nae unahisi hafikii Viwango na Ubora unaoutaka kwa Mpenzi.

Basi unaendelea kusubiri au kungojea hali inayosaidia kuzingatia Masomo/Kazi au chochote unachokifanya kwa wakati huo bila "Can we meet tonight, I miss you" sort of usumbufu.

Lakini katika hali halisi(in reality) mambo hayaendi hivyo unless otherwise uumbe mwanamke/mwanaume wako vile utakavyo nje na ndani.

Sasa unapofikia umri fulani kuanzia miaka 25(kwa wanawake) hivi unaanza ku-settle kiakili unagudua kuwa Viwango na Ubora unaoutaka hauwezi kupatikana kwa mtu mmoja hivyo unaanza kushusha/kupunguza.

Wengine hugoma kushusha/punguza na badala yake hufikia mahali wanakata tamaa(muda umeenda) na kuwa desperate na hivyo kujitolea Mhanga na kujiambia "liwalo na liwe".....ndio maana unaweza kukuta mtu kafunga Ndoa au kazaa na mtu ambae hawaendani kabisa au hawapendani ila desperation imepelekea iwe hivyo....which is sad really!

Anyway....Muhimu ni kupunguza Ubora na kushusha Viwango utakavyo (ulivyojiwekea) kutoka kwa mpenzi mtarajiwa kwani huwezi kuvipata vyote....unaweza kupata 5 out of 12 au 3 out of 8.


Wakati mwingine unapata Viwango au Ubora ambao wewe hukuufikiria mara baada ya kujenga Mahusiano au kuishi pamoja na Mpenzi husika.


Muonekano ni muhimu na kama anatick vibox 2 nje ya 5 sio mbaya vingine utakutana navyo huko huko na kujifunza kuvizoea au kumsaidia kubadilika.


Badili mtazamo kisha ujiulize ni nini hasa unataka au unadhani ni muhimu kutoka kwa Mpenzi....orodhesha vitu vitatu, Mf; (1)Iwe kwenye Muonekano (2)Iwe kwenye Mazingira na (3)iwe kweny Elimu.


Na je wewe uta-offer nini kwake na kwenye uhusiano wenu kwa ujumla ikiwa mtafikia hatua hiyo?.


Je unadhani ni kitu gani unacho(in terms of knowledge) na ukitumie hicho kukamata attention ya mwanamke husika.

Zingatia mazingira uliyokutana na mwanamke husika, anza kwa kupiga stori za kawaida tu bila kuhusisha mambo ya "kisomi"....unless mwanamke mwenyewe aanzishe.


Jaribu kuwa interesting, iwe kwa kucheza, mavazi, simulizi, tabasamu, unavyojiweka n.k.... inategemea na mazingira uliyopo na aina ya watu waliokuzunguuka.


Inaonyesha huna issue ya kujiamini (hivyo unaweza kushawishi mwanamke).....Upole/Ukimya, sio tatizo ni sehemu ya Character yako, inakufanya wewe kuwa wewe(tofauti na wengine).

Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
pole kaka kwa kutafuta mwanamke wa ndotoni!
Hawapatikanagi hao kwa kumwona tu halafu akawa perfect at first sight!

Lazima uingie nae ktk mausiano na jinsi utakavyoendelea naye kwa muda,utagundua kuwa ulipoteza muda mwingi ukihesabu nyota hadi mwezi ukakuponyoka!

Pata marafiki wa kike na kiume na jitose katika mahusiano ndipo utakapojuwa mbivu na mbichi!

Kama dada Dina alivyokushauri,vigezo vingi unavyoviweka kwa mpenzi unayemuhitaji;vilinganishe na viwango ulivyo navyo wewe ambavyo mwanamke pia anaweza kuvutiwa navyo.

all in all,UKICHAGUA SANA NAZI utaambulia kuchaguwa koroma na ukimchunguza sana nyuki,hutakaa uionje asali!
Anonymous said…
pole kaka naungana na dada dinah pia nashukuru kwa ushauri wake maana na pia nina tatizo hlo japo mi bado cjafika umri huo ila nawish kupata mwanaume aliye serious all the best katika kutafuta
Anonymous said…
Anoymous 4:36:00 mm nikoserious kupatyta mke alotulia, ila tatizo mm niko Mombasa (kenya). sijui tutaanzia wapi kazi nashukuru nipo nayo kipato chake cha wastani,na mm hutamani nijenipate mke mchapa kazi sio kukunja maguu,tusaidiane kuendesha gurudumu la maisha na tukijaaliwa kuwa nawenetu tuwape maisha bora na elimu bora...
anony 4:36:00 said…
Anony9:48:00 km uko serious endelea tufanye mawacliano ila cjui tutawacliana vp