Ningependa kuolewa ila naogopa...

Hello Dinah, Pole na majukumu ya kila siku. Samahani usiweke jina langu.

Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 28. Sijaolewa ila niliwahi kuwa na
uhusihano wa kimapenzi ambae alikuwa wa kwanza kwa muda wa miaka 3.

Mimi na Mpenzi tulipanga kufunga Ndoa nikiwa na miaka 25 na alikuwa
amejitambulisha nyumbani lakini kabla ya kufunga Ndoa alitaka
tushiriki tendo, nilikataa nikaomba tufunge Ndoa kwanza.


Chakushangaza alikataa katakata akasema hawezi kuoa mke
ambaye 'hamjui'. Baada ya kunipata ndiyo siku aliyoniacha.


Baada ya mwaka mmoja nilikutana na mwanaume mwingine niliyempenda
sana. Tulipoanza tu mahusiano akawa anataka ngono kwanza lakini Mimi
sikuwa tayari kutokana na mambo yaliyonitokea awali sikumweka wazi
kuwa sitaki ngono kabla ya Ndoa kwani pia tulikuwa na malengo ya kuoana.


Kadri siku zilivyoendelea aliacha kunigusia suala hilo la ngono na kuniambia anaheshimu maamuzi yangu.


Nilizidi kumpenda sana na hakuwahi kunibadilikia hata siku moja. Tukiwa kwenye harakati za kutambulishana, kukawa na send off ya rafiki yangu kwa Bahati nzuri nikakutana na mwanaume wangu akiwa na Mkewe


Tangu kipindi hicho nilichanganyikiwa na kujikuta nachukia wanaume na
sitamani kuolewa tena wala kuchumbiwa.


Nimeshatembelea Hospitali
nakufanyiwa councelling na kutumia dawa za kuondoa stress lakini Moyo
wangu umeshindwa kuamini wanaume tena!


Naomba unisaidie Dada Dinah maana umri unazidi kwenda na hili janga linanizidi kila nikisikia mwanaume anagusia Ndoa kwangu.

**************

Dinah anasema: Hi! Ahsante na shukurani kwa ushirikiano, usitie shaka kwa kawaida huwa sitoi majina.


Sikuwahi kutendwa bali nilikuwa nachukia au niseme NAOGOPA Ndoa.....yaani mtu akigusia tu na Uhusiano unaishia hapo (natoka mbio na siangalii nyuma) nadhani nilikuwa too "academic" a.k.a Msongo....anyway!

Nadhani tatizo hapo ni Muda(Akili/Moyo bado haujapona), ulitoka kwenye uhusiano wa kwanza na ulikuwa wa muda mrefu na mwisho wake ulikuwa wa "kudhalilishwa" na maumivu....in which ulikupa maswali mengi yasiyo na majibu.

Tatizo lingine ni Imani yako juu ya Ndoa na hofu ya kuzeeka bila kuolewa, jiulize; Kwani nini umuhimu wa Ndoa maishani? Na Je hata nikiwa kwenye ndoa siwezi kutendwa ikiwa mume atakaenioa si mwaminifu?


Ndoa sio guarantee ya kufurahia maisha yako.....kwenye maisha kuna mengi ya kufurahia zaidi ya Ndoa, enjoy maisha yako, jiweke sawa Kiuchumi alafu ukifika 30s huko ndio uolewe.

"Maumivu ya Moyo hayapoi kwa Ganzi", maana yake hayahitaji Hospitali wala Dawa za kupunguza stress (ukizoea utakuwa mtumwa wa dawa hizo) na zitakupa wehu.


Unahitaji Muda nje ya mahusiano ya kimapenzi, Familia (watu wakaribu wanaokupenda na kukujali) aka support system.

Pia, Unahitaji kukaa mwenyewe kwa muda mrefu zaidi ya Mwaka mmoja, piga miaka miwili au mitatu ya "single, happy and free", kula na furahia maisha yako kama mwanamke.

Alafu baada ya hapo anza tena kutoka au kujenga uhusiano wa kimapenzi wa "kurudisha imani"....kwamba mpo serious na penzi lenu na mnafurahia bila kupeana presha za kufunga Ndoa.

Mwaka mmoja kuingia tena kwenye uhusiano "serious" ilikuwa kosa, napengine hukuwa na mapenzi kwa huyo "Mfano wa mume" bali upweke, hali ya kupoteza kujiamini na ulikuwa "vulnerable" kihisia baada ya kuumizwa. Hali hiyo ndio ilikufanya UDHANI anakupenda na wewe unampenda.


Kumbuka sio kosa lako wanaume hao kuwa na tabia walizo nazo, chukulia kuwa wanamatatizo ya akili na wanahitaji matibabu au wamesahau kula dawa zao.


Songa mbele na ufurahie maisha yako bila kuhofia suala la Ndoa, muda ukifika (ukiponyeka) utapenda, utapendwa na mtafunga ndoa. Unamiaka mingine kama 40 hivi kabla hujazeeka.


Kila la kheri Mrembo.
Mapendo tele kwako...

Comments