Ndugu wa Mume wanataka watoto.

Dinah habari za kazi, Mimi ni mama mwenye watoto watatu wenye umri wa Miaka 16, 12 na Tisa.

Mimi na Baba yao tumeachana bila Talaka miaka miwili iliyopita na mwenzangu tayari anamwanamke mwingine kitu ambacho sio tatizo kwangu.

Kinachonisumbua kichwa ni yeye Mume wangu na ndugu zake kung'ang'ania kuchukua watoto. Mimi binasfi sipo tayari kuacha wanangu wakaishi na watu wengine kwa muda mrefu hata kama ni ndugu zao.

Pia naogopa wakienda huko watakataliwa kurudi kwangu na hivyo kuishi maisha ya unyonge na upweke.

Kama ni wewe ungekuwa kwenye viatu vyangu ungefanya nini?


Ushauri wako utanituliza Moyo na akili ili niweze kulea wanangu na kufanya kazi kwa amani. Asante.


**************

Dinah anasema: Njema kabisa, nashukuru kwa ushirikiano.

Hao ndugu nao wanakiherehere kama mama_______! Wakati unanema kuwapata hao watoto walikuwepo? Waambie walee watoto wao, wakuachie ulee wako.

Hakuna mama mwenye akili timamu anaeweza kuruhusu watoto aliowazaa wakakae na watu baki (hata kama ni baba ambae hawajamuona kwa miaka 2 anakuwa "baki" kimtindo).


Sina uhakika na Sheria za Ndoa na Familia za Tanzania zilivyo hivi sasa, ila natambua Mahakama na Ustawi wa Jamii hushirikiana kwenye kutoa msaada.


Kitu muhimu ni wewe kumtaliki Mumeo (kisheria), utaratibu wa sasa siujui ila ukienda Mahakama ya Wilaya hapo ulipo na kuomba kuonana na Hakimu wa masuala ya Familia atakusaidia kwa ushauri na nini cha kufanya (nadhani kuna Fomu unajaza kwanza kabla).


Hakimu anapitia kesi yako (ulivyojieleza kwenye fomu), kwa vile umetangena na Mumeo kwa miaka 2 na tayari anamtu mwingine itakuwa rahisi.

Baada ya hapo nadhani Mumeo atatumiwa Barua ya kuitwa Mahakamani kisha "Kesi" yenu kusikilizwa....weka wazi na kusisitiza kuwa unataka kumtaliki mumeo.


Usiwe na hasira na wala kuongea katika hali yeyote itakayoashiria bado unahisia nae au bado unamaumivu ya kuachwa (ili isionekana unataka kumkomoa).


Baada ya hapo Uamuzi utafanywa na nadhani utashauriwa uende Ustawi wa Jamii kwa ajili ya masuala ya Mgawanyo wa Mali zenu, Matuzo ya watoto....n.k.


Kisheria (kama hawajaibadilisha) kutokana na umri(zaidi ya miaka 6) wa watoto, watoto wana haki ya kuchagua wanataka kuishi na nani kati yako Mama au Baba yao.

Watoto wataulizwa mbele yenu wote(Wazazi) kuwa wanataka kwenda kuishi na nani na Ustawi wa jamii watatoa ripoti yao kuhusu "issue" yako ya watoto wakae na nani, mgawanyo wa mali + matunzo kutoka kwa Baba yao.

Baada ya hapo nadhani utarudi tena Mahakamani na Uamuzi kufanywa na Hakimu Mhusika.


Ndugu huwa hawahusiki kwenye stage hii unless otherwise mmoja wenu afariki Dunia wakati wa process.

Kazi kwako kuwashawishi watoto wagome kwenda kuishi kwa Baba yao, tumbia mbinu zote za chini ya jua(sina maana uchawi, bali ushawishi kama Mama yao) kama unaweza ili wasikubali kwenda kwa Baba yao (ambae atawapeleka kwa Ndugu zake).


Fanya hayo kabla hujaanza shughuli za kupelekana Mahakamani, kwani kibongo-bongo inaweza kuchumua muda mrefu.


Baada ya uamuzi, hakikisha watoto wanauhusiano mzuri na Baba yao, usiwajaze maneno kutokana na hasira zako au hisia zako kwa baba yao ili wamchukie baba yao.


Kama watamchukia iwe kwa vile aliwaacha wao wakiwa wadogo (they will hate him for that naturally) bila wewe kusema lolote kwao.


Hivi hakuna Blog za Wanasheria wa Familia na Watoto za Kibongo? Ingesaidia sana kwa update za sheria hizi muhimu.


Mie sio mtaalamu wa sheria + naishi nje hivyo sizijui sheria za Ndoa na familia za sasa za Tanzania.

Najua hayo niliyoyaelezea kwasababu mtu wangu wa karibu alipitia humo na alifanikiwa. Ni kitambo thought.


Nakutakia kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

alphonceambonisye@gmail.com said…
Dina umeeleza vema sana, japo nataka niongeze kitu. Mie ni mwanasheria na katika hili, ndugu hawana chao kwan wao sio wahusika halali kwenye hili swala. Na pia hata kama mume anahitaji watoto kuna taratibu za kufuata na Mahakama ndo inaamua hivo. Katika hali halisi ndugu hawana haki ya kuchukua watoto wala Baba kuwachukua akalee na mke mwingine, maana mama mzazi yupo na anaishi nao vizuri. Vilevile kama ni ndoa ya kikristo ukitaka kuvunja nenda kanisan mlipofungishwa au kanisa lolote la namna hiyo kama mlihama mkoa. Kama Muislam nenda kwenye baraza la waislam, ukienda sehem hizo mtasuluhishwa na ikishindikana mtapewa document ya kwamba imeshindikana ( hii ni lazma kisheria kufanyika hata kama mme wako anaishi na mwanamke mwingine) baada ya hapo mahakamani. Dada anaushahidi wa kutosha kwanza mme wake amezini, pili amemtelekeza. So dada pole sana na mambo ni mengi, kwa ushauri zaid unaweza kuniandikia kwa alphonceambonisye@gmail.com
Anonymous said…
Dina maakili mengi