Mzito kufunga Ndoa...

Habari Dada Dinah, pole na hongera kwa kazi ya kujitolea unayofanya kuelimisha jamii na kutoa ushauri huru hasa kwa vijana wanaotaraji na walio kwenye mahusiano.

Mimi ni Baba wa watoto wawili niliozaa na mwanamke ninayeishi nae sasa. Tulianza mahusiano toka mwishoni mwa mwaka 2008 baada ya mimi kumaliza Chuo Kikuu na kuanza Kazi ilihali yeye alikua anamalizia masomo yake ya A'level (form six).

Mwaka 2009, alipata Ujauzito wa mtoto wetu wa kwanza hivyo ilinilazimu kwenda kwao kufanya Utambulisho rasmi na kuona nini "way forward". Wazazi wake walinipokea vizuri na wakahitaji tulipe baadhi ya "mali" na tukafanya hivyo na kulipa Mahari kwa kama asilimia 85 hivi.

Kwa sababu alikua amefanya vizuri katika Mitihani yake ya Kidato cha Sita, alipangiwa chuo cha Ardhi hapo Dar es salaam, Wazazi wake walisema hawataruhusu tufunge hadi amalize Masomo ya Chuo Kikuu.

Uamuzi wa Wazazi wake uliniumiza sana. Hata hivyo walimruhusu aishi kwangu bila Ndoa na wakatoa sharti la kuhakikisha anaendelea na masomo bila kuyakatisha. Kwa sababu hata mimi nilipenda asome,niliwaahidi wazazi wake kwamba sitamkatisha masomo.


Wakati akiwa masomoni huku analea mtoto wetu, Nilijitahidi kuona anapata huduma za msingi kumuwezesha kusoma vyema. Hivyo nilimpangia chumba karibu na Chuo, nikampatia Msichana wa kazi na mahitaji mengine muhimu ikiwa ni pamoja na kumtembelea kila mwisho wa mwezi nikitokea Arusha.


Hata hivyo baada ya mwaka wa kwanza, niligundua kuwa alianza Mahusiano ya Kimapenzi na kijana ambaye alikua ni mwanafunzi wa Chuo hicho wa mwaka uliotangulia. Niliumia sana kwa sababu sikujua kwanini anafanya hivo ilihali yeye ni mpenzi wangu na ninajitahidi kumtimizia mahitaji yake kwa kadiri nilivyoweza


Muda wa kufanya field (2010) aliomba na akapangiwa huko kwao Bukoba, hivyo alienda huko kwa ajili ya Field na mwanetu na mdada wa kazi. Nilimshauri aombe mafunzo hayo aje kufanyia Arusha akadai amesha-omba so haiwezekani kubadilishwa.

Masikini kumbe yeye na huyo kijana walikua wamepanga wakafanye Field pamoja ili wapate muda wa kua wote kwa kipindi chote cha Field huko.

Niliona mabadiliko kwenye mawasiliano na ikanibidi kumtumia rafiki yangu wa huko Bukoba ndipo akanieleza kwamba anamuona na huyo kijana most of time.


Fied ilipoisha alikuja Arusha, huku mtoto akiwa na hali mbaya sana na msichana wa kazi aliondoka bila kuaga na aliacha barua kwa moja ya marafiki zangu akiniasa niwe makini na mke wangu kwa maana sio muaminifu na ameondoka kwa sababu hajapenda kuishi na familia yenye hali ya udanganyifu.

Kwa sababu sikujua ameenda wapi yule binti na hakuacha namba ya simu hivyo sikuweza kumpata hadi leo.

Ilibidi nimuweke chini nimuulize kuhusu yale yote na baada ya kum-bana sana alikiri kuwa na rafiki ambae ni mwanafunzi mwenzake lakini alikataa kabisa kwamba hakuwa na Mahusiano naye ya kimapenzi.

Akadai huyo kijana anatabia ya kujikweza anapokua na urafiki na msichana basi yeye anatangazia watu wengine kwamba yupo nae kimapenzi. Aliomba msamaaa na kusisitiza yaishe na ameelewa amekosea nini so atajirekebisha na kwamba hatakua na ukaribu wala mawasiliano na yule kijana tena.

Dada Dinah, mwaka wa Tatu (2012) kama kawaida nilienda kumtembelea mwezi wa kumi na mbili. Nilienda na ajenda ya kumuomba tufunge ndoa ya Serekali ili nipate attachments kwa ajili ya Records zangu kwani nilikua nimetoka Private na kuingia katika ajiara ya Serekali.

Mpenzi wangu alikataa kabisa na kusema anahitaji muda afikirie na awashirikishe Wazazi wake. Hivyo nilimuacha atafakari kwanza.


Nilipokuwa huko nilimnunulia simu mpya na tukakubaliana ile simu yake tumpe zawadi Mama yangu mzazi hata hivyo nilipoondoka nikawa nimeisahau kwa hiyo akaituma Arusha kama Parcel.

Kabla sijampa mama niliweka laini yangu ili niweze kufuta some text na kurestore settings ili isimpe shida mama kuitumia. Hapo nikakuta text za mapenzi na appointments zisizopungua 20 na nilipochunguza niligundua ni namba ya yule kijana.


Nilimpigia simu kumuuliza akashindwa kunikjibu, akadai zilikua ni za zamani sana na hata hivyo hana mawasiliano na huyo kaka siku hizi. Nilimpigia yule kijana kwa hali ya utulivu alinipokea simu yangu na kunitambua kabisa kama Baba____. Nilipoongea nae kwa kirefu akasema ni kweli alikua na mahusiano nae japo mwanzoni hakujua kama ana mwamaume because aliwahi kumwambia haishi na mwanaume.


Yule kijana alikiri kwa sasa hana mahusiano nae kimapenzi bali ni marafiki na yeye ameshamaliza Chuo na ameoa. Tuligombana sana lakini kwa kuwa ulikua ugomvi wa simu, niliona ni busara nimpe nafasi afanye mitihani yake ..then tutayaongea vyema baadae.

Mwaka Jana mwezi wa 8 alimaliza Chuo na ku-Graduate rasmi Novemba 2013 na akaja Arusha tukaanza kuishi pamoja. Nilitafuta muda nikamtoa ili nimuulize kuhusiana na yule kijana. Akasema hana mahusiano nae na zile meseji zilikua za zamani.

Nikamuonesha na tarehe na zille meseji zilivo, akasema hazikua za tarehe hizo, kwa sababu alizimove kwenye phone baada ya Sim Card kujaa so zimerecord tarehe ambazo zilikua moved.

Baada ya hapo ameanza kutaka tufunge Ndoa na ananikera sana na jambo hilo japo nimeshamwambia mie kwa sasa sipo tayari lakini bado ni msumbufu mno.

Wazazi wake wananiuliza pia kuhusu Ndoa? lakini ukweli ni kuwa Moyo wangu unakua mzito mno na naogopa kula kiapo na huyu mwanamke. Nimepoteza hata hamu ya tendo la ndoa kwake..

Dada Dinah naomba ushauri Tafadhali.


**************

Dinah anasema: Habari ni njema sana namshukuru Mungu, ahsante kwa ushirikiano.


Pole kwa yote uliyokabiliana nayo kwa miaka yote wakati Mwenza wako yupo Masomi. Huyo mwanamke nae mchafu wa tabia, hana utu wala shukurani.


Kutokana na matendo yake maovu ya kusaliti uhusiano wenu bila kujali hisia zako wala za watoto wenu ni wazi kuwa humuamini tena.


Uaminifu unapotoweka kwa mtu unaempenda kunakuwa hakuna umuhimu au faida ya kuwa na uhusiano mpaka Uaminifu urudi.


Kwa kawaida aliesababisha Uaminifu kupotea (asiaminiwe tena) ndio hupaswa kufanya jitihada za kurudisha uaminifu huo. Kurudisha uaminifu sio rahisi kama vile "najua nimekosa, sitorudia tena na sitofanya mawasiliano na whoever".


Baada ya hayo yote wala asingekuja kifua mbele kulazimisha Ndoa ambayo awali aliikataa. Nadhani anajua "udhaifu" wako ambayo nahisi ni Upole na huenda unashindwa kumconfront ukiwa firm kutokana na ushahidi ulionao....anacheza na Saikoloji yako.

Anafikiri kuwa amekupata, kwamba anakudanganya na unaamini Uongo wake na ndio maana baada tu ya kurudi kakimbilia kutaka kuolewa.


Nini cha kufanya: Ifanye issue uliyonayo iwe yenu na SIO yako, kwamba kaa na mwezio na uzungumze nae kwa uwazi jinsi unavyojisikia.

Mwambie kwa mf; "kwavile nanyamaza au kukubaliana na Uongo wako haina maana kuwa mimi ni mjinga na sijui nini kilikuwa kinaendelea".

Ongeza; "Kabla ya ushahidi niliokuonyesha unaodai kuwa ni wazamani which inaonyesha usaliti wako kwangu pia kuna watu walikuwa wananipa habari zako".


Mwambie..."Hayo yote yamenifanya nijiulize mara nyingi kama kweli unafaa kuwa mke wangu au la!"......Hayo yote yamenifanya nisikuamini tena na wala sitamani tendo na wewe, nahisi kinyaa...nikikuangalia na-imagine wewe na yule Kijana mnafanya mapenzi, so inani-put off".

Endele; "Nahitaji muda kukuamini tena na wewe unahitaji kunithibitishia kuwa na tabia njema na mapenzi ya dhati juu yangu ili nirudishe hali ya kukuamini na kuvutiwa nawe tena"

Malizia "Kila kitu kikienda vizuri na uaminifu kurudi basi tutaangalia uwezekano wa kufunga ndoa, lakini kwa sasa sipo tayari".


Weka kila kitu cheupe ili ajue unavyojisikia.....aache kujionda bingwa wa kudanganya na kuficha siri kumbe wee unaugulia na ukweli unaujua.

Wazazi wakiuliza kuhusu Ndoa, waambie kuwa wewe na huyo Bibie mna issue zenu mnajaribu kuzitafutia ufumbuzi kabla hamjafunga ndoa.

Wakitaka kujua ni issues gani then waeleze moja kwa moja au via Mshenga(hakikisha ni ana kwa ana, sio simu).


Tangu ulitoa Mali na sehemu ya Mahari na sasa mnawatoto wawili, hakika una haki kuwakilisha issue yenu kwa Wazazi kama wanandoa, japo sio rasmi..

Vyovyote mtakavyoamua kumbukeni kuna maisha ya watoto wawili ambao wanahitaji Mapenzi yenu kama wazazi. Umoja wenu usipofanikiwa basi hakikisheni watoto wenu hawateseki.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
Pole kwa yote kaka.nimejska uchungu a if ndo mimi!tulia fanya maamuzi sahihi usije ukakosa aman maisha yako yote yaliyobaki.kuwa na watoto sio tatizo au sababu yakukufanya ulazimike kufunga ndoa na mtu asiemwaminifu.na kama humuamini tena hata upendo utakua wakulazimisha.mm ilinitokea kwa mume wangu ila tayar nlikua tayar kwenye ndoa(bomani)seriously had leo simuamn na hata upendo wangu kwake niwakulazimisha.inanicost mno!!so kua makin.ndoa ni nzuri mkiwa wote waaminifu ila ni mbaya kama mwenzio sio.kila la kher ndugu. Mungu pia ni mwaminifu sa ukimshrikisha haja zako.lì