Kisirani sehemu ya Kwanza!

Shikamoo dada Dinah, Pole  na majukumu dada na asante sana kwa kutuelimisha kupitia blog yako hii.
    

Mimi ni msichana mwenye miaka 25 sasa nimeolewa miezi kadhaa imepita bado hatujapata mtoto, naifurahia sana ndoa yangu.
 


Tatizo dada Dinah ni mimi mwenyewe Mume wangu hana shida kabisa. Yaani sijielewi nimekuwaje maana  nina  katabia ka Kisirani.


Nakasirika bila sababu mume wangu anaweza akanisemesha kitu namjibu kwa hasira mpaka ananishangaa. Sio kwamba simpendi nampenda sana.


Sometimes nina Kisirani hadi kwa ndugu zangu, nanuna bila sababu sina furaha Moyoni sijui ni Wivu au ni nini?


Natamani kuacha hii tabia lakini najikuta nairudia tu. Halafu nina hasira za haraka sana mume akiniudhi tu kidogo nakuwa mkali sana.

Halafu uvivu usiseme kuamka asubuhi ni shida nashindwa kabisa na sina kazi nipo tu nyumbani nahisi nina mkera sana ila hasemi.


Nataka niishi kwa furaha kama wanawake wengine wanaojiamini maana mimi sijiamini kabisa kwa lolote then ni muoga sana hata kupita au kukaa mbele za watu ni shida.


Mume wangu ananishangaa sana kwa uoga nilionao natamani nibadilike lakini nashindwa. Naomba unishauri dada Dinah nianze wapi niachane na hizi tabia kwani zinamkera mume wangu sana.


Halafu msimamo ndio kabisa sina kabisa nipo nipo tu.Nashindwa kujisimamia mie mwenyewe nabaki kuiga na kutamani mambo ya watu.


Msaada wako dada Dinah utaokoa ndoa yangu changa kabisa na pia utanifanya niishi kwa amani bila mateso moyoni mwangu kwani ni mtu ninaetamani kubadilika.
    

Kusoma nimesoma na nina Elimu nzuri kabisa. Namshukuru Mungu kwa kweli mimi ni mrembo sijisifii ila ni ukweli hivyo tabia kama hizi mfano za wivu, chuki zisizo na sababu, pia kujali mambo ya watu sijui vinatoka wapi.

Ahsante dada Dinah.


**********


Dinah anasema: Marhabaa Binti, shukurani kwa ushirikiano.

Nahisi kama vile unatatizo la Kisaikolojia linalonifanya nipate maswali haya.....Je, umewahi kunyanyaswa/teswa kwa aina yeyote ile ulipokuwa Mtoto/Shuleni?

Je, uliwahi kuugua sana enzi za utoto wako?

Je, umelelewa na wazazi wako wote wawili au ulikulia/lelewa kwa ndugu au Mzazi mmoja ambae sio wa Damu?


Wewe ni wa ngapi/mmezaliwa wangapi ulipata attention sawa na wadogo/wakubwa zako au unahisi wao walipendelewa? Hebu rejea nyuma na ujitahidi kukumbuka kisha rudi tena kwangu.


Yote uliyoeleza ni tabia ambazo husababishwa na hisia zenye maumivu kutokana na maisha yako ya nyuma, kuna uwezekano mkubwa kabisa hukujua kama uliumizwa/umia na ulichukulia au bado unachukulia ilikuwa hali halisi.


Ukali na Kisirani ni dalili ya "kujilinda" kabla hujawa attacked.....Mf; ukiamka tu umenuna ni wazi kwamba Mumeo hatotaka kukuudhi kwani tayari umeudhika....hivyo kama alitaka kuzungumza na wewe kuhusu jambo lililopelekea "kisirani" chako, hapati nafasi hiyo.


Vilevile kwasababu unajijua ulivyo na hupendi kuwa hivyo lakini unashindwa kujizuia. Inaonyesha wazi kwamba unahofia au hutaki kuambiwa na watu wengine kuwa tabia yako ni mbaya....hivyo ili kuwapiga stop....unajihami kwa kuwa Mbogo (Mkali) so hakuna atakae sema chochote.

Suala la kutokuwa na Msimamo sina uhakika unamaana gani! Mf; "Msimamo wangu ni kuzaa baada ya kuolewa"...."Msimamo wetu ni kutotumia ovyo pesa mpaka nyumba iishe"....

Wanawake wengi hawana misimamo au kama wanayo basi huibadilisha mara kwa mara....ndio maana kuna msemo kuwa "I am a woman and I am allowed to change my mind".

Kutokana na maelezo yako ni kwamba unatamaa, unatamani kuishi kama watu wengine au kuwa na vitu kama fulani...!!


Suala la uvivu nikiliunganisha na maelezo yako ya awali nadhani linasababishwa na hali ya kutothamini au ridhika na Maisha uliyonayo.....hivyo huoni sababu au umuhimu wa kujituma na kufanya shughuli yeyote iwe ndogo au kubwa hapo nyumbani.


Pamoja na kusema hivyo haina maana utakuwa hivyo Daima milele. Kwavile upo tayari kubadilika basi itakuwa rahisi. Hautobadilika ndani ya wiki au mwezi lakini utabadilika tu kama nia unayo.


Kitu muhimu ni kutambua kuwa wewe ndio mwenye uwezo na Control ya kumbadilisha Wewe, hakuna mtu atakae control au kubadili msimamo wako, bali wewe.


Hakuna atakae kuondolea Kisirani, bali ni wewe mwenyewe. Hakuna mtu atakaekuondolea hali ya Uvivu bali ni wewe mwenyewe. Hakuna mtu atakaekupa amani Moyoni, bali ni wewe mwenyewe.

Nitarudi na sehemu ya Pili nikushauri ufanye nini ili kuondokana na tabia hiyo.
Mapendo tele kwako...

Comments