Kaikataa Mimba...Mie naitunza!

Shikamoo dada Dinah, hongera na kazi yako nzuri. Samahani dadangu mie ni binti nina miaka 22, nasoma College mwaka wa Tatu nategemea kumaliza Mwezi wa Nane.


Nilikuwa kwenye uhusiano na mwanaume kwa miezi kama mitatu. Siku tuliyosex kwa mara ya kwanza ndio siku nikapata Ujauzito, hiyo ni baada ya kupima ndani ya wiki Mbili.

Shida ni kuwa home Wazazi ni wakali ile mbaya na wakijua kifatacho ni
kunitimua nyumbani na mwanaume huyo ananambia kuwa hayuko tayari kuwa baba kwani hakujipanga.


Mwanzoni niliumia sana lakini nikajitahidi kulichukulia suala langu kawaida ili lisiniathiri katika masomo, hivi sasa nina Mimba ya wiki 4 na kila mara naambiwa kuwa kama ningetoa ingekuwa best.


Mie kutoa sipo tayari sababu naamini kiumbe hakina makosa, wenye makosa ni sisi, naomba mnishauri kitu kimoja kuhusu huyu mwanaume.


Yeye hajaukubali huu Ujauzito na hilo linamuathiri katika kazi zake na anasema mipango yake imevurugika. Nataka nimsaidie Kisaikologia ili aone ni tatizo dogo na aweze kufanya mambo yake hata kama hatonipa support mimi na mtoto.


Naombeni mnisaidie.

*************


Dinah anasema: Marhabaa Binti, Ahsante kwa ushirikiano.

Sasa na wewe ilikuaje ukangonoana na mtu kwa mara ya kwanza Bila kinga ukijua wazi utashika Mimba na hivyo kutimuliwa kwenu?


Ndani ya hiyo miezi mitatu ya "uhusiano" wenu mlikuwa mnafanya nini au mnazungumza kuhusu nini? Maana inaonyesha hamkulizungumzia suala la "je nikishika Mimba tutafanya nini?" na mengine Muhimu mkakimbilia kutiana tu....watoto wa leo MNATIA HASIRA! Anyway....limetokea hatuwezi kubadilisha but I had to say that.

Aliekuambia Mimba ni tatizo dogo alikudanganya. Mimba na baadae Mtoto ni Mabadiliko Makubwa sana kwenye Maisha ya mwanadamu na hakuna "going back".

MOSI....Wacha kupoteza muda na nguvu kumsaidia mwanaume aliekuwa TAYARI kufanya Ngono Bila kinga lakini HAYUPO TAYARI kuwa Baba. The shenzi kabisa.

Mimi pia sitopoteza Muda wangu kukushauri nini cha kufanya ili kumsaidia huyo Kijana wakati wewe ndie uliebeba Mzigo, Nyumbani kuna Utata na ndio utakae zaa kwa Uchungu.


Wachaa ateseke Kisaikolojia na ikiwezekana afukuzwe na kazi ili apate robo ya robo ya Machungu utakayokumbana nayo kama Single mother.

Au unadhani ukimsaidia atajirudi na kukubali Mimba ili muendelee na Uhusiano?! Tunza nguvu zako kwani utazihitaji sana ndani ya Wiki 8 zijazo na siku ya Kujifungua.

Sasa nakupa Ushauri ambao hujauomba! Focus....woman Focus....kama umeamua kuutunza Ujauzito usitegemee sana kuwa huyo Jinga siku moja atarudi na kukuoa (akirudi tutajua then)....kwasasa tengeneza Mazingira Mazuri kwa Wazazi wako na Mtoto utakae mzaa.

Anza na Mama yako na uanze kwa kuomba Msamaha kisha umpe picha kamili....Mama huwa na namna ya kuwaweka sawa Baba so atasaidia kukufikishia ujumbe.

Hakuna Mzazi atamchukia mwanae kwa kukosea (kosa Kubwa na la kijinga)....wazazi wanapokuwa wakali kwetu ni kwasababu wanatutakia Mema, hawataki tuwe na majukumu Magumu kabla ya Umri (chini ya Miaka 25).


Napenda nikuhakikishe, pamoja na ukali wa wazazi wako bado watakukubali na kukupa support(hasa Mama).


Pamoja na kusema hivyo tegemea kufokewa na kupokea kila aina ya matusi kisha huruma au kilio na huruma kisha kufokewa au kutukanwa.


Maliza Masomo yako salama, Lea Mimba yako, Omba Mungu akulinde na ujifungue salama kisha Tafuta kazi/shughuli ya kukuingizia Kipato....lea Mwanao.

Mwanao akikua atamtafuta Baba yake...

Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
mimi nina swali moaj kwako wewe binti, unatuambia kua jamaa amekataa mimba je ulimuambia kua uko kwenye tarehe hatari na bado akasisitiza mfanye? au ulimtegeshea ili iwe ni gia ya kuoana? mana kwa mtu ambae hakua tayari kua mzazi ukimueleza kua uko kwenye tarehe za hatari hua yuko radhi kuarisha au kutumia kinga