Atishia kuniacha kisa FB!

Hi dada Dinah natumai hujambo na mzima wa afya. Hongera sana na pole
kwa kazi ya kuelimisha na kuboresha mahusiyano ya jamii.

Nina shida dada yangu, nahitaji wazo lako. Nina b/f wangu wa mwaka na miezi kadhaa anasema anataka kunioa ila simpendi hata kidogo.


Nimekubali kuolewa nae
ikibidi, ila sasa naona anaanza kuwa mkali. Anataka eti nitoe
picha zangu zote facebook na ikiwezekana nifunge kabisa account yangu.


Mimi nimemwambia sintaongeza kuweka picha zingine ila hanielewi na kuhusu kufunga kabisa nimemwambia kuwa siwezi kwasababu inanirahisishia kuongea na ndugu, jamaa na marafiki maana niko nao mbali.

Baada ya kumwambia hayo yeye amenitishia kuniacha.

-Je nitekeleze anayotaka? au nikisha tekeleza ndio ataanza sasa na
maamuzi mengine ya kiajabu-ajabu?


Au niachane nae kama alivyonitishia?
*************

Dinah anasema: Ungekuwa unampenda au mnapendana hakika ningekushauri uzungumze nae tena na kumuelewesha umuhimu wa ubaki na facebook yako kwa sababu kuu ulizozitaja.

Lakini upunguze mazoea ya karibu na namna ya kuwasiliana "rafiki" zako ambao baadhi wanaweza kumfanya jamaa apate wivu au akwazike.


Lakini kwa vile humpendi ni vema kuendelea tu facebook yako na yeye akuache kama navyotaka kuliko kubaki kwenye uhusiano nae wakati humpendi(unampotezea muda na unajipotezea muda pia).

****************

-Je nikiolewa nae na simpendi tutaathirika/nitaathirika kivipi? Au nitamzoea na kupenda jisi siku zinavyokwenda?

**************

Dinah anasema: Hakuna athari mtazipata ikiwa mtafunga ndoa isipokuwa mtakuwa hamna furaha au amani na ni guarantee kwa mmoja wenu au wote kutoka nje ya ndoa kutafuta "kupendwa" au penzi.

Utamzoea lakini kwenye kumpenda siwezi kujua maana kama mmekuwa pamoja zaidi ya Mwaka na bado humpendi "hata kidogo" sidhani hilo litabadilika mkifunga ndoa.


Kama unafikiria kuolewa nae ukiamini utampenda nadhani ni vema kuendelea ku-date kwa muda mrefu zaidi ili uone kama hisia zako za mapenzi zitajitokea kwake.
**************


-Swali lingine, eti ni kweli kutia mabarafu ndani ya uke inapunguza upana wa uke? Nini kazi ya
barafu ukeni?

kila la heri dada dinah.

*************


Dinah anasema: Do'h! Logically...ukiweka barafu itapanua uke kulingana na ukubwa wa barafu hiyo....then barafu itayeyuka na uke kujirudi kama ulivyokuwa awali....Jibu? HAPANA...Barafu haipunguzi uke.


Uke umedizainiwa kupanuka kulingana na kinachoingia na kujirudi tena, hiyo ni kwasababu ya kuruhusu mtoto kuzaliwa.

Ikiwa Misuli ya Uke wako imepanuka kutokana na Mf; kuanza Ngono wakati mwili bado hauja-settle (kabla au wakati wa Balehe au chini ya miaka 21). Utakapozaa, uke utapanuka ku accommodate "safari" ya mtoto Duniani na baada ya hapo uke wako utajirudi kama ulivyokuwa kabla ya Uzazi.


Kwa maana hiyo, kama tayari uke wako ni mpana na baadae ukazaa, utajirudi kwenye "upana" wake na si kuwa mdogo.

Na ikiwa uke wako ni mdogo basi baada ya uzazi utajirudi na kuwa mdogo kama ulivyokuwa kabla ya uzazi.


Ahsante kwa ushirikiano na Kila la kheri!
Mapendo tele kwako...

Comments