Ataka Ndoa, mie nasoma.

Mimi nikijana umri wangu miaka 24, ninamchumba wangu ninampenda sana na tumedumu kwenye uhusiano huu ni mwaka wa Nne but hatujawahi kukutana kimwili maana ndivyo alivyo niomba hadi ndoa.

Mimi bado niko Chuo ila mwenzangu hakufanikiwa kuendelea na Masomo sasa yuko nyumbani kwao. Juzi kamtuma rafiki yangu akidai anahitaji kuolewa kwani amechoka kunisubiri.

Kila nikimpigia simu anadai yuko bize yani kiufupi anaona kama ninamsumbua. Ninampenda sana ila mwenzangu ndio kashaanza vituko please nisaidie dada dinah.

*********


Dinah anasema: Unamiaka 24 na uhusiano wenu unamiaka Minne which means mlianza mkiwa watoto....tusema alikuwa 17 na wewe 20.


Well, sidhani kutopokea simu au kusema yupo busy ni vituko. Huenda kweli yupo busy akijipatia "uzoefu" wa maisha baada ya shule. Ila wewe unajishtukia ukidhani unamsumbua (huenda kweli ni msumbufu) sio kila mwanamke anapenda kuwa checked on kila saa.

Katika hali halisi, kama ni Mchumba wako ni wazi kuwa Unajulikana kwao na yeye anajulikana kwenu, umetoa Posa na seheme ya Mahari au Mahari yote si ndio?.


Sioni sababu ya kwanini Mchumba wako kumtuma rafiki yako kukufikishia ujumbe badala ya kutumia Wazazi/Mshenga wako via wazazi wake au kukuambia moja kwa moja. Unless mnaitana Muchumba kufurahisha nafsi zenu kuwa uhusiano wenu ni serious, kwamba hamjakamilisha taratibu za Kuchumbiana.

Binti atakuwa na miaka 24 au mdogo zaidi, akili yake na mtazamo wake na hisia zake hazifanyi kazi kama alivyokuwa miaka 4 iliyopita, amekuwa kwa kiasi fulani, si msichana tena bali ni Mwanamke.

Huenda sasa (since hasomi) anadhani ni wakati muafaka wa yeye kuolewa na tayari kuna "wachumba" wanataka kuoa leo-kesho.


Kutokana na maelezo yako ni wazi anakuambia mfunge Ndoa haraka au umuache aolewe na mtu mwingine kwani amechoka kukusubiri.


Kufunga ndoa kwavile unampenda mtu ni vizuri, lakini hamuwezi kulipa bills na kula penzi lenu, mtahitaji pesa kutimiza hayo.


Kutokana na umri wako na bado unasoma nisingekushauri ufunge Ndoa mpaka ujiweke sawa Kimaisha na Kiuchumi.


Kaeni chini mzungumze tena na ku-review options zenu (kama zipo) kiuchumi sasa na baada ya ndoa(kama mtaamua kufunga)....mkishindwa kuelewana pelekeni issue yenu kwa Wazazi wenu na kama vipi vunjeni Uchumba.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
Bwa mdogo,
pole kwa vitisho toka kwa 'mchumba' anayejali maslahi yake tu na si ya yule ampendaye!

kutokana na maelezo yako,mwenzio amepata 'ingizo jipya' hivyo anakupa presha ili ufanye haraka umuoe au umchukuwe muishi wote!hizo ni indiketa kuwa CHELEWA CHELEWA utakuta mwana si wako!

fanya mandingo umuoe mwenzio!