Umri gani sahihi kupishana kati ya Mume na Mke?

Salaam dada dinah, pole kwa shuhuli za kuelimisha jamii. Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 32, nimeolewa miaka kumi iliyopita na nimebarikiwa kupata  watoto wawili. Mume wangu ana umri wa miaka 48.

Naomba unisaidie suala moja, je ni umri gani sahihi wa  kupishana kati ya Mke na Mume?


Nauliza hivyo kwa sababu mimi na mume wangu tumepishana miaka 16. Hapo mwanzo sikuwahi kufikiria kuwa issue ya umri itakuja kuwa tatizo kwenye ndoa yangu ila kwa sasa ndio naona mapungufu mengi sana tena sana dada dinah.


*************


Dinah anasema: Kupishana miaka sio Tija na sidhani kuna umri sahihi as long as hakuna mtoto kati yenu(chini ya Miaka 18).

Pamoja na kusema hivyo ni vema kuepuka gap kubwa sana...Maana mnaweza kugongana kwenye kufanya maamuzi ndani ya uhusiano au ndoa. Mmoja akiwa mdogo sana (hajamaliza Ujana) mwingine Mkubwa sana (kamaliza ujana).

**************


Kwanza kabisa kwenye suala la mapenzi kifupi ni kwamba perfomance ya Mr imepungua sana, mpaka huwa namuonea yeye huruma na mimi pia najionea huruma sana.

Yaani sijui hata nisemeje, dada dinah si unajua umri wangu ndio kwanza nina moto wa hatari, mwanzoni  Mr alikua moto wa kuotea mbali ila kwa sasa  hakuna kitu.

Sasa sijui ni umri, sijui ni stress, sijui ni majukumu au ni nini? ila hakuna kilichobalika ktk suala zima la kazi zake za kila siku.

**************

Dinah anasema: Point hiyo, "hakuna kilichobadilika ktk suala zima la kazi zake za kila siku". Mumeo anakaribia kugonga Nusu Karne maisha yake kikazi hayajabadilika....hata mie ningepata stress na depression kabisa!!


Maisha yake yamebadilika, sasa ana mke na watoto ambao wanakua na mahitaji yao yanavyoongezeka lakini Kazi zake ni zilezile tangu mmefunga ndoa....huoni hii ni sababu kuu ya Mawazo, Hofu na Mashaka?

Pia, inawezekana ni uoga wa utu uzima, Miaka 50 inatisha ujue?!! inaweza kumtisha hasa kama hajafanikisha alichotaka kufanikisha kabla ya umri huo.

Kama issue ni hiyo basi utendaji wake kitandani na afya yake kwa ujumla inaweza kuathirika.

****************


Tulishawahi kulizungumzia hili suala na yeye anasema hajui kwa nini? ila hatujawahi kusema twende kwa Daktari au kusema atumie dawa.

Mwanzoni ilikuwa tunasex karibu mara nne kwa wiki na hapo unapata kitombo cha hatari mpaka K inawaka moto ila kwa sasa maskini sipati hata miezi miwili.


Hata haijaingia vizuri wakati huo mimi ndio naisubiri kuipokea daaah  tayari ameshapiz. Inaniumaga lakini ndio ivyo tena sina jinsi.

Namwambia asante, nampa pole basi!!! hapo ndio basi tena hata uimbe nyimbo zote haisimami tena!!! naomba unisaidie kwa hili kwani napata shida sana na minyege.

***************


Dinah anasema: Kwavile umesema wakati mwingine mnakaa hata miezi 2 bila Ngono huenda "ukame" ndio unamfanya acheke mapema.

Kama ilivyo kwa Wanawake, wanaume pia wanamatatizo yao ya afya. Yanaayosababisha mabadiliko ya huko "sirini"....yaweza kuwa mf: Kisukari, Saratani, n.k

Mimi kama mwanamke siwezi kukusaidia kwa kukupa jibu lenye uhakika kwasababu sijawahi kuwa na uzoefu huo (umri wa Mume wangu haujafika huko).

Nadhani wanaume wanaweza kukusaidia zaidi kama wamewahi kuwa na tatizo linalofanana na hilo.

Suala la kuzidiwa na Nyege unapaswa kulijadili na Mumeo na kwa pamoja mkubaliane namna ya kusaidiana...maana kuna njia nyingi za kufurahia na kupunguza Nyege bila kuingiliwa.

*******************


Isitoshe alikua ameshanizoesha kufurahia Ngono kisawasawa,halafu hali inachange ghafla, naniuma sana.


****************

Dinah anasema: Maisha ya Ndoa hubadilika kama yalivyo maisha yetu sisi kama wanadamu, inabidi mmoja au wote m-adopt mabadiliko ili kufurahia ndoa yenu.

Hamuwezi kuishi maisha yale yale kwa miaka kumi na yaendelee kuwa hivyo kwa miaka mingine kumi.

*******************


Kwa ujumla hali hiyo imeanza kama miaka miwili iliyopita, kuna mabadiliko mengi sana achilia mbali hayo ya kitandani.


Hobbies zimechange, caring, outings hakuna tena na many many things. Hata suala la kushauriana kimaendeleo hakuna tena yeye anafanya mwenyewe bila hata kunishirikisha.

Nikimwambia vipi? anasema anafanya anachoweza yeye. Nimekaa nikajiuliza maswali bila majibu.

*************

Dinah anasema: Mdada mbona hapo hali inajieleza wazi! Ikiwa anafanya anachoweza ni ama hana pesa za outings au kuendeleza Hobi zenu za zamani.


Kama hayo mambo ni muhimu sana kwenye uhusiano wenu lakini yeye hawezi basi fanya wewe(kama una kipato), book mahali, toka na mumeo kwa ajili ya Mlo au kinywaji.

....kama huna kipato basi vumilia na utoe mawazo ya kuongeza kipato nje ya kazi zake ili maisha yawe vile upendavyo.


Kumbuka pamoja na mengine, maisha ya ndoa yanahitaji ushirikiano na kusaidiana.

************


Je ni kweli umri wake umeenda sana na haya yote yanaweza sababishwa na  umri huo?? au ni nini nisaidieni kuhusu hilo na pia unishauri kama anaweza tumia dawa.
Asante,


Kila jema kwako  dada dinah
naomba mobile namba yako dada dinah please, nitumie kwenye mail yangu.


***********


Dinah anasema: Sidhani kama ni Umri, miaka 48 mbona bado sana. Nadhani kuna issues nyingine zinamsumbua ama kichwani (hofu, mawazo) au mwilini(afya).


Ushauri wangu ni kumpa ushirikiano na support ya kutosha, zungumza nae kuhusu afya yake (kufuatia mabadiliko)....


Punguza ku-demand outings, shopping sijui Hobbies na badala yake toa ushirikiano katika kutafuta ufumbuzi wa chanzo cha mabadiliko unayoyaona kwa mumeo.

Kuna wanaume hutoa maelezo mazuri sana, natumaini wataliona hili na kutoa ushauri kama wanaume.

Nasikitika kuwa sina namba ya simu kwa ajili ya ninachokifanya hapa.

Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

Jay said…
Wanawake mnakimbilia kuolewa au kuzaa mapema mno. Mnatakiwa kuenjoy maisha na kufanya starehe zote kabla ya kuwa mke au mama. Huwezi kuwa mama na mke alafu uishi maisha kana ya watu ambao wapo single bila majukumu.Outings na hobbies sio muhimu mpaka watoto wajitegemee yaani wawe wamemaliza shule.

Ndio maana huwa tunasema maliza ujana wako kabla hujazaa au kuolewa kwani there is no go back untill the kids are at least 21yrs old and leave home then you and your hubby can start outings and add more hobbies in your life and enjoy getting old together.

Ushauri wangu ni wewe kumpa support mumeo na kumshawishi kwenda kumuona Daktari ili afanyiwe uchunguzi wa kina kuhusu afya yake kwa ujumla.