Uhusiano wa Kimapenzi na Binamu...

Hi dinah natumai umzima na unaendelea vyema na majukumu ya kazi.

Mimi ni msichana ambae nilijikuta nime fall in love na Binamu yangu ambae kiukweli ni wa mbali kidogo ktk ukoo wetu hivyo sikuwa na mjua kwa sura ila kwa jina tu.


Ikatokea kama bahati tukawa na mawasiliano as sister and brother at the end tukajifunika shuka moja baada ya miezi sita ya uhusiano wetu.

Yeye ndio wa kwanza kwangu nami kwake ni wa kwanza. Tukawa tunaendelea na maisha kama kawaida lakini ikatokea Udhuru na akateuliwa yeye kuendesha familia.


Mwanzo alikua anaiendesha sawa lakini mwisho akawa anafanya ilimradi tu. Katika kuchunguza kwangu nikagundua kuwa ana msichana ambae alikua anauhusiano nae kwasababu alikuwa anaongea nae maneno ya sita kwa sita.


Baada ya kugundua hilo nikamueleza na yeye kunijibu kuwa hana uhusiano nae ila anafanya hivyo kuficha uhusiano wetu wa miaka minne sasa ambao bado hatujauweka wazi.

Cha kushangaza sasa akawa kila akirudi kutoka kazini anakuwa kakasirika, mfano nikiingia chumbani kwake anakasirika kiufupi akawa kabadili tabia tukawa hatuna mapenzi kama yale ya awali ya kusaidiana kazi za ndani.

Yeye anadai hakuwahi sex nae lakini mwanamke alimtumia mpenzi wangu (Binamu) picha zake kwa whatsap.

Hivi sasa yupo mbali nami anasema eti ananipenda na hajawahi nisaliti huko alipo. Anasema kuwa anapanga maisha vyema hivyo nijichunge kwasababu mimi ndio nitakaekuwa mke wake.


Je? ananipenda kweli au he wants to waste my time?


*************

Dinah anasema: Ah! Mie bukheri wa afya namshukuru Mungu.


Atakupotezeaje muda wakati ni Binamu yako tena kapewa jukumu la kuendesha familia eti....hihihihi natania mwaya.


Hata kama angekuwa Binamu wa karibu upande wa Mama au Mjomba nisingeshangaa maana Chemistry inaweza unganisha mambo ukashindwa kuelewa (kwa vile huwa hakuna strong connection kama Ndugu) sema Waafrika tunapenda kulazimisha tu Undugu.


Siwezi kusema au kumdhania kuwa anakupotezea muda kwasababu uhusiano wenu ni wa kuibia kwa Miaka minne.

Kwenye kuongea masuala ya mapenzi na kupokea/tunza picha za mwanamke husika kunatia mashaka kiasi.


Mwanaume mwaminifu na committed kwa mpenzi wake hapaswi kuwa na picha za mwanamke mwingine ambae sio ndugu yake wa karibu au kuongea masuala ya kimapenzi na mwanamke mwingine....hakuna kisingizio.


Kwasababu wewe ulikuwa wa kwanza kwake ni wazi hukuwa na uzoefu na hakupata uzoefu wowote kutoka kwako.

Nasema hivyo kwa sababu wanaume wengi hupenda kupata uzoefu kabla hawaja-settle(kuoa) so kwa dunia ilivyo sasa mmmmh! sidhani kuwa ni mkweli au muaminifu kwako.


Kama mpo serious na uhusiano wenu basi wote kwa pamoja mliweke hilo wazi kwenye familia zenu ili mjue nini mtakabiliana nacho huko mbeleni.

Mf: Kususwa na familia zenu, kuachanishwa kwa lazima, kuondolewa kwenye Mirathi au mmoja wenu kuozwa kwa lazima ili kutunza "siri ya familia".

Msimamo wake kwenye hayo niliyogusia ungeninifanya nijaji kuwa hakupotezei muda na yupo serious na committed kwako na uhusiano wenu.


Miaka minne ni mingi sana, zungumza nae na useme yaliyoujaza moyo wako na kuwa upo tayari kwenda hatua ya mbele kwenye uhusiano wenu.


Mwambie ungependa na upo tayari kuweka wazi uhusiano wenu ujulikane kwenye familia zenu.

Majibu yake ndio yatakayokufanya ujue msimamo wake kwako au kwenye uhusiano wenu kwa ujumla.

Akisita kutoa jibu au kuomba muda zaidi basi ujue kuwa ni mpitaji tu huyo.....sababu kama ni muda wa kufikiria mwisho Miaka miwili.


Kwa miaka minne amekuwa akijua kuwa analala na "Binamu yake" kwa maana hiyo alikuwa anajua kama ni kosa au si kosa mbele ya Familia/Ukoo wenu.


Huombi kuolewa au Mahari bali unaomba uhusioano ujulikane so hakuna cha kusita hapo ni NDIO au HAPANA! hilo moja.

Pili, akikataa na kusema familia ita-whatever then mnapotezeana mida.

Tatu, akikubali lakini kudai muda zaidi wa kusubiri basi rudisha muda nyuma kwamba akisema msubiri hadi July, mwambie unataka May. Jibu lake hapa litakufanya ujue msimamo wake.

Ukiona anakuyeyusha, sahau miaka minne, sahau tena tupa kule "mie wa kwanza kwake".....

Toka nje ya "Ukoo" ili uone zaidi ya "Binamu" namaanisha usafishe macho kwa ku-date sio ukafanye ngono ovyo-ovyo.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments