Tarehe za kuzuia Mimba

Dinah! Mambo? I hope mzima wa afya, unaendelea na majukumu ya hapa na pale.


Mimi mmoja wa fans wako katika blog yako. Samahani, na swali moja nahitaji kufahamu. Nilikutana na mpenzi wangu kimwili na siku hiyo nakutana nae kama tarehe 15.


Yeye alikuwa anaingia Hedhi tarehe 24, na hatukutumia kinga. Then kuna siku nilikuwa napitia blogs nikakutana na kitu kuhusu mwanamke anaweza kutambua siku zake na kujikinga na Mimba.

Ilikuw hivi; kabla ya mwanamke hajaingia hedhi kuna siku 8 za hatari kabla ya tarehe yake ya kuiona hedhi, na kuna siku 8 baada ya hedhi ni za hatari.

Basi nilivyo soma hivyo nikamtext na akanielewa kuwa ni kwel ikabidi tusubiri tuone kama ataingia hedhi tena coz alikuwa anaelekea kuingia tena.

Ilipofika tarehe 24 hakuiona hedhi kwamba atakuwa amepata ujauzito, nilimwambia akapime na jibu aliloniletea aliniambia kuwa ni mjamzito.

Sorry Dinah kuna ukweli wowote juu ya hili? Au ananidanganya coz siko nae karibu.

Thanks.


**************

Dinah anasema: Namshukuru Mungu, ahsante kwa ushirikiano.

Asa wewe sijui nikucheke au nikutukane? Hakika atakuwa na Mimba.....unafanya bila kinga then unaenda kusoma maelezo kwenye blog kisha unajipa Moyo kuwa hatoshika mimba! Who does that?!!....Only Dumbs...KINGA 1st mengine yanafuata dogo!


Huyo alieandika siku 8 kabla na siku 8 baada ya Hedhi bila shaka atakuwa Mwanaume.....ndio hao hao wanaodai kilele kwa mwanamke ni kama kutaka kukojoa mkojo wa kawaida!!!

Ndio, ni kweli kuna siku kwenye mzunguuko wa hedhi ambazo ni Salama (Humimbiki) na Hatari (Unamimbika) lakini tarehe hizi hutoa matokeo yenye uhakika kama Mzunguuko wa mhusika ni wa siku 28 kwamba haubadiliki.

Mzunguuko wa Hedhi wa kawaida wa siku 28 ndio pekee (nadhani) unaaminika(kwasababu ni rahisi kukumbuka).

Siku ya kwanza ya Hedhi ndio siku ya kwanza ya Mzunguuko na Yai hupevuka siku ya 14 tangu Hedhi kuanza.



Siku ya kushika Mimba(Hatari) ni siku ya 10, 11, 12, 13, 14, 15 na 16 tangu Hedhi kuanza(sio tarehe kwani hubadilika).....siku Salama na zenye uhakika ni Siku ya kwanza ya Hedhi mpaka ya siku ya 7 ambapo kwa baadhi ya wanawake bado yuwa Hedhini....Siku zilizobaki sio Salama kivile.


Sitopiga mahesabu hapa (sina maelezo ya kutosha kuhusu mzunguuko wa huyo Binti) ila nitakupa maelezo ambayo yatasaidia ili wewe mwenyewe ufanye mahesabu.


Mwanamke anapoamua kutumia tarehe kama Kinga ya Mimba anatakiwa kufuatilia kwa karibu "mahesabu" ya tarehe zake angalau kwa miezi 3 kabla ya kuanza kungonoka bila Kinga.


Kutokana na uzoefu wangu siku kabla ya Hedhi huwa ni hatari kwasababu hakuna anaejua Manii husika zitakuwa hai ndani ya mwanamke kwa muda gani.

Inategemea na afya Manii hubaki hai kuanzia siku 3-7 hivyo unaweza ukapata Hedhi na ile umemaliza tu Mimba ikaingia.....


.....sidhani kama Hedhi inasafisha Manii na pia inategemea Upevukaji wa Yai linalofuata(sometimes hupevuka mapema).

Pole kwa kushtukiziwa Mimba, next time weka tumia Condom kama hutaki mtoto....

Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments