Social Net na Mahusiano!

Social Network hazina tofauti na kuangalia Tv.....Unapokuwa mfuatiliaji wa karibu wa Tv programs na kuhisi umekuwa addicted nazo ndivyo ambavyo huwa kwenye "Shosho Netiwoku"....



.....Unajikuta unakolea huko mpaka unasahau kama una familia achilia mbali Mpenzi.




Miaka ya nyuma (Mwaka nilioanza kublog) niliandika kuhusu Technology na sikwenda moja kwa moja kwenye Sosho Media/Netiwoku kwani enzi hizo hazikuwa nyingi nadhani zilikuwa ni blogs, forums na facebook....




Soma topic hiyo http://dinahicious.blogspot.co.uk/2007/09/vishawishi-vinavyosababishwa-na.html?m=1



Miaka mitatu baadae nikakutana na topic kama yangu kwenye Magazines na Magazeti ya huku nikasema "heko to me, niliona mbele kabla yao".



Ingekuwa ni Magazine na Magazeti ya Tz ningesema wameiba sehemu ya maelezo yangu hihihihihi lakini ilikuwa ni Media za UK ambazo nina uhakika Waandishi wao hawasomi wala kupitia Blog yangu.



Anyway, sina mengi ya kusema zaidi ya kukumbushia tu kuwa hizi Technolojia za mawasiliano zimeanza kuchangia sana tena sana Uvunjikaji wa Ndoa na Mahusiano mengi kitambo.



Ukiachilia mbali ongezeko la matatizo ya Kisaikolojia na maovu mengine ya kutisha, Teknolojia imeingilia na kuharibu heshima miongoni mwetu na kuua Uoga wa kuumiza hisia za wenzetu tunaowapenda, pengine kwa makusudi au bila kujua.




Kuna faida gani kuwepo nyumbani mapema au kutoka na mwenza wako huku attention yote ipo kwenye Tv au Simu?!!!


Kama ilivyo kwenye kila kitu, moderation na kujua limit ni muhimu.
Mapendo tele kwako...

Comments