Simuelewi

Pole na kazi, nina mchumba anamiaka 35, ananipenda kwa dhati na anatabia nzuri, mcha mungu, mpole na ananiheshimu. Tumekuwa kwenye Uhusiano kwa miaka 6.


Tatizo lake hana future, hana malengo na hajishughulishi walau kuweka Miradi. Anategemea Mshahara ambao haukidhi mahitaji tangu tumejuana mpaka leo hana hata Kiwanja na soon tutaoana.


Nipo njia panda je anafaa? Nahisi tutaishi maisha magumu kutokana na yeye kutojishughulisha.

Nimejaribu kumsihi mara kadhaa anasema ataanza kwani bado anajiimarisha. Namuonea huruma kumuacha ila tatizo ndio hilo.


Kazi njema


**************

Dinah anasema: Nashukuru ahsante.

Tangu mmekuwa pamoja kwa miaka hiyo sita ni yeye ndio aliekuwa akitumia Mshahara wake kukuhudumia wewe sio?

Kama sasa anamiaka 35 ni wazi mmeanza uhusiano akiwa na miaka 28 which means ulikuwa mdogo kwake kwa miaka kadhaa na ni wazi kuwa alikuwa akitumia senti zake kwako.


Kama alikuwa akitumia Laki kwa mwaka(mfano tu) hivi sasa angekuwa na Laki Sita Bank kama angeamua kutunza....sasa calculate pesa zote he gave you for the past 6yrs.


Huoni wewe ni mchango mkubwa wa yeye kutokuwa na Kiwanja....Eti Mrembo?!!


Je, wewe una mchango gani kwenye uhusiano huo zaidi ya Ngono? Je, unafanya Kazi/Biashara/upo nyumbani unalea watoto wenu?


Kingine unachopaswa kujiuliza ni kuhusu familia yake, Je anategemewa kwenye familia yake?(Hasa kama yeye ni Mkubwa au mwanaume Pekee).


Mchumba wako anafanya kazi, huko ni kujishughulisha, anakwenda kazini kila siku...huko ni kujituma.


Atafunguaje mradi au kwa pesa/Mtaji gani ikiwa Mshahara wake kwa sasa hautoshi kukidhi mahitaji?

Hofu yako ni kuishi maisha magumu ikiwa mtafunga ndoa kitu ambacho nakielewa....lakini pia ukumbuke kwenye ndoa kuna mabadiliko je, mkifanikiwa sasa na kuishi maisha mazuri bila tatizo la pesa na mara pesa zikaisha(miradi hailipi) utamuacha?


Kwenye maelezo yako huonyeshi Mapenzi kwake na wala huonyeshi (hujasema) mchango wako kiuchumi.

Uhusiano sio kupokea tu, uhusiano ni kutoa pia. Kabla hujaanza kulalamika na kuweka hofu mbele na kumshutumu mwenzio kuwa "hajitumi" au "mzembe" wakati tayari anakazi.....unatakiwa kujiuliza maswali niliouliza hapo juu.


Kama yeye "hajitumi" lakini kila mwezi anakupa senti za Salon, Simu, Pombe na Nyama choma au kufanya manunuzi yako binafsi au chakula then bana matumizi na senti za salon na Pombe(kwa mfano) uzitunze ili zikitimia ufungue Mradi.


Kama umeweka mezani na yeye anakuambia bado hajakaa vizuri basi muonyeshe kwa vitendo. Mpenzi mwema hutumia akili na kujituma ili kusaidiana na mwenzie....


Mchumba wako inaonyesha kuwa anafaa na ni mwanaume mwema mwenye mapenzi kwako(kutokana na maelezo yako)....hastahili kuachwa kwasababu mshara wake hautoshi.


Anakwenda kazini na kufanya kazi zake peke yake na mwisho wa mwezi mnatumia Mshahara wake kwa pamoja kurekebisha mambo.

Tatizo sio yeye bali ni wewe kuwa tegemezi (unaweza kuwa na shughuli na bado ukawa tegemezi) kwasababu tayari anajituma.


Hakuna kanuni ya kufanikiwa maishani. Wengine hufanikiwa mapema na wengine hufanikiwa in their 50s, hivyo miaka 35 sio Tija.

Jitume kama mwanamke, piga kazi/buni na endeleza mradi/biashara na weka mchango wako Kiuchumi kwenye uhusiano wenu, mfunge Ndoa na kwa pamoja mshirikiane kununua Kiwanja na kuanza kujenga.


Kuna mchangiaji mmoja aliwahigusia "Heri pesa za kutafuta pamoja, kuliko zile unazozikuta".....mie naongezea....Heri kujenga pamoja kuliko nyumba uliyoikuta.


Kama nia yako ni kuachana nae basi tafuta sababu nyingine lakini sio hiyo ya "kutojituma".


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
hello dada Dinah, kwa mara nyingine tena natuma comment ya kukupongeza, ulichokiongea hapo juu ni ukweli mtupu usiopingika, huku kwetu TZ mchumba/mpenzi ni source of income kwa wapenzi wetu wa kike wanasahau kua ile ni relationship na sio employment opportunity