Nimechoka Kugombana...

Za majukumu dada natumai hujambo na unaendelea na majukumu ya kila siku. Dada dinah niko kwenye mahusiano ambayo mpaka sasa naona hakuna ukweli maana kila wakati ni ugomvi.


Mimi na mpenzi wangu ambae kiumri amenizidi kama miaka 5 na yeye ndio mwanaume wa kwanza kwangu kuwa nae.

Mara nyingi tunagombana ikiwa yeye anataka tufanye mapenzi na mimi nikikataa tu atasusa hata siku tatu hataki mawasiliano na mimi.


Mpaka nimmbembeleze ndio awe tena kawaida na kuna wakati ananiambia maneno makali mno kuna siku dada dinah aliniambia "kwani mimi kaka yako unakataa kunipa penzi" seriously nilikaa nikafikiria hiyo kauli nikaona nafanya vibaya nikamwambia sawa ila itakuwaje nikapata mimba?


Akaniambia yeye sio mtoto mdogo awezi kufanya ujinga huo, nikamwambia sawa ila twende tukapime basi hapo tena ikawa ni shida tulikaa wiki bila kuongea akanitafuta akaniambia niende nikapime yeye tayari kapima.


Nikamwambia nataka nirudi Dar tukapime wote, kweli nilirudi Dar tukaenda kupima na Majibu yakaja wote tupo salama sasa ikawa bado kutimiza alichotaka.


Siku ilifika tukawa tumekutana ilikuwa mara ya kwanza dada dinah na sikujua naanza vipi na nilitetemeka mwili mzima ila siku hiyo alishindwa kuingia hadi ndani.


Dada dinah sikukaa muda sana akataka tena turudie ili apite mpaka ndani but hiyo siku ilifika tuko Lodge akaniudhi kweli nikamuuliza kwanini anakuwa mkorofi muda wote?

Akasusa kwanini nimemuuliza vile, akaniacha mule chumbani mwenyewe akaondoka zake. Nililia sana nikaamua niachane nae.

Kila siku matatizo, nilikaa peke yangu muda mrefu bila kumtafuta na yeye hakunitafuta mpaka Christmas mwaka jana ndio akanitafuta, nikamchunia.


Mwaka mpya pia akaniambia tuwe tunawasiliana kwanini nakataa kuwasiliana nae au kwasababu nishapata bwana mwingine? nikamwambia sawa tutawasiliana.


Usiku akawa akituma msg ya usiku mwema anaanza nakupenda sijui nini mambo mengi tu. Kuna siku nyingine ananiambia Leo nimekuota mara nimekumiss, nashidwa kumuelewa analengo gani na mimi.


Maana tumekaa miezi mingi hajanitafuta wala kuuliza siku alivyoniacha Lodge kama nilifika nyumbani salama au laa.


Mwezi wa tatu ameniaga anaenda jeshini na atarudi mwezi wa 9 na siku ananiambia anaondoka eti alikuwa anataka nikamuage nyumbani kwake.


Kanilazimisha kweli ila mpaka sasa hivi simuelewi yuko vipi dada dinah nisaidieni kumuelewa napata shida nimempenda ila nashindwa kumuamini ..kazi njema


**********

Dinah anasema: Ahsante na shukurani kwa ushirikiano.

Huyo Kijana inaonyesha akili yake bado haijakua, yote anayoyafanya ni kama Mtoto wa miaka 20.


Muache aende Jeshini salama, na wewe focus kwenye issue nyingine za kujikomboa kama mwanamke.


Bado Binti mdogo, huitaji kupewa hekaheka za akili mtu asiejielewa kama huyo....umri wako (ulionitajia) ndio pekee wa kuanza kujiweka sawa ama kielimu au kikazi/kibiashara/kimaendeleo.


Kwavile tu alikuwa wa kwanza sio sababu ya wewe kuendelea kuwa nae hata kama inaonyesha wazi anachokitaka kwako ni Ngono.


Mwanaume huyo hana Utu na wala hajali Hisia na Matakwa yako....alikuacha peke yako mahali pageni (Lodge) kwasababu hukutaka Ngono au hukuwa tayari.


Mwanaume mwenye Utu, Heshima na kujali Hisia zako angetaka kujua kwanini hutaki na ange heshimu matwaka yako au angekubembeleza ili ukubali lakini sio kususa na kukuacha peke yako.


Huyo Kijana hakufai, inaonyesha hana mapenzi na anakutumia kwavile anauhakika huna maambukizo kwa sababu yeye ni wa kwanza kwako.


Uamuzi wako wa kumchunia ulikuwa sahihi na sioni sababu ya wewe kwenda kumuaga(atataka Ngono) kabla hajaenda Jeshini.


Najua (kutokana na umri wako) huelewi au umechanganyikiwa as hujui nini hasa ni Mapenzi au Uhusiano wa Kimapenzi.....je Mapenzi ni Ngono kama atakavyo yeye au Mapenzi ni kumpenda mtu na kuwa nae karibu kwa ajili ya maongezi na romance kama unavyotaka wewe?


The "wangu wa kwanza" thing haina maana yeyote kwa mwanaume bali kumuongezea "Ego" kuwa hakuna mwingine kabla yake....Haina guarantee kuwa atakupenda, atakuheshimu au atakuwa mwaminifu kwako.


Bikira inamaana kwa mwanamke husika, ni sifa kwako kuwa umejitahidi kushinda vishawishi kwa muda wote huo uliokuwa Bikira.....


Kwa mabinti wengine ambao bado Bikira, tafadhali itunze kwa ajili yako na sio kwa ajili ya kupata heshima au kupendwa au kuolewa na atakaekua wa kwanza.

Na ikitokea umeolewa ukiwa Bikira usitegemee sana kuwa Mumeo atakuwa mwaminifu kwa ajili hiyo, kama sio mwaminifu atabaki kuwa hivyo daima milele hata kama yeye ni wa kwanza kwako.

Furahia maisha yako bila stress na ukiwa tayari utafurahia uhusiano na Mkaka mwingine na hakika utafurahia Ngono kwenye umri mkubwa zaidi ya ulionitajia.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments