Msabato na Ex...

Mpendwa dada Dinah. Pole sana na kazi nyingi na kutoa ushauri kwa watu wenye ishu mbalimbali kama sisi.


Niliandika muda mrefu kumbe attachment kwako ikawa ngumu kufunguka. Huwa napenda kuingia katika page yako mara kwa mara kusoma mambo mbalimbali na  kupata mawili matatu.

Nilishawahi kuandika kwenye page hii na ukanishauri vyema, narudi tena nikiwa na tatizo jingine kabisa.


Mimi ni mdada nina miaka 28 sasa mwaka huu. Nimemaliza Chuo na nimebahatika kupata kazi nzuri kabisa.

Nilishawahi kudate mkaka enzi hizo nasoma Degree chuoni na tulikuwa na uhusiano kwa miaka mitano na tukabahatika kupata mtoto wa kike ambae kwa sasa ana miaka 3 na zaidi.


Niliposhika mimba ya mtoto huyo mwanaume alishauri sana kuitoa lakini mimi nikagoma kufanya hivyo, na hapo ndipo matatizo yalipoanza kwani penzi lilianza kupungua.

Ila kwa msaada wa wazazi na ndugu zangu nilibahatika kujifungua salama. Tangu nijifungue hakuwa mtu wa kujali sana kuhusu mtoto. Awe mzima au mgonjwa na hakuwahi hata kuja kumwona mtoto hata mara moja.


Nilikuwa bado nambembeleza akae sawa, ikafika kipindi mtoto akiwa na miezi tisa nikasikia anatoka na mtu mwingine na anaishi nae.

Nikabeba mwanangu nikaenda hadi kwake Mwanza kuhakikisha hilo kwani mie naishi Mbeya. Sikubahatika kumfumania na nilikaa kwake kwa muda wa siku tatu.

Sikutaka kuamini kuwa ni yule mwanaume ambae mie niliwahi kudate nae kwani namfahamu jinsi gani alikuwa anapenda na kubembeleza ngono hadi analia.


Lakini kwa siku tatu nilizokaa kwake hakunigusa wala hakuomba ngono na kwa kuwa nilikuwa nishasikia mengi sikuhangaika nae kutaka mapenzi.

Hapo nikajua kweli hana hisia tena kwangu, siku ya 3 nikijua kesho yake ndio naondoka niliamua kumuuliza juu ya jambo nililosikia la kuwa anadate mtu mwingine, alikuwa muwazi kusema kweli anadate mtu na kuwa mimi na yeye basi.


Niliichukulia kiume japo ni mwanamke niliondoka nikaenda kulala Hotel na kesho yake kugeuza safari. Nami mahusiano yakaishia hapo.


Nikaanza maisha mapya yangu na mtoto japo kwa tabu ila nikaja kuzoea. Cha kushangaza hata ndugu zake wakajitenga si Mama, Madada, wala Kaka zake hamna aneuliza hadi leo mtoto anaendeleaje tangu kipindi hicho akiwa na miezi tisa hadi sasa miaka mitatu na kashaanza na shule hamna anejua mtoto anafanana vipi.

Maisha yangu yaliendelea huku nikiwa sina mawasiliano nae. Baada ya mwaka hivi akaanza kupiga simu. Mwanzoni nikawa sipokei ila baada ya muda nikawa napokea na kumuuliza shida nini akawa anasema anataka kuongea na mwanae.


Nikawa nampa simu mwanae aongee makorokocho yake kwa sababu bado alikuwa haongei vizuri sana alichelewa kupanga maneno.

Akawa anapiga simu hivyo hivyo siku ananiomba tuzungumze na ukiongea nae anakuambia nimekumis, namis kila kitu kwako mara hiki hiki anaanza kutaja vitu tulivyofanya pamoja enzi hizo.

Sikutaka kumweka akilini sana na nikaacha kupokea simu zake maana akawa akipiga simu ni kuongea habari za kumisiana tu.


Maisha yakaendelea hatimae nikaamua kumove on kimahusiano baada ya miaka 2 ya kukaa single nikilea mtoto wangu kwanza.

Nikampata mkaka mwingine ambae tulianza mahusiano  na sasa tuna mwaka mzima na zaidi katika mahusiano.

Nakumbuka tulianza mahusiano hata mie sikuwa sawa kiakili, kihisia kwa kuwa bado nilikuwa nawaza sana Ex wangu na kila kitu nilichozoea kufanya nae.

Kiukweli nilimpenda sana na huyu Mkaka wa pili nae alikuwa katoka kusalitiwa na mpenzie ikawa tumekutana Ofisini kama marafiki hadi tukaanza kudate.

Tatizo lililopo sasa ni kuwa huyu mpenzi mpya ni Msabato na mimi ni Mkatoliki. Yeye ana ishu nyingi za kidini ambazo anadai zinamrudisha nyuma katika kuamini kuwa nitakuja kuwa mke mzuri kwake kama unavyojua sheria za Kisabato.

Pia tuna interests tofauti mwenzangu anapenda kuimba miziki ya dini mimi si sana japo siichukii. Mwenzangu mchamungu zaidi yangu.


Tumekuwa tukiishi hivyo kwa mwaka na zaidi sasa bila sex ila romance na tunaishia hapo. Jambo ambalo mie naliona sawa tu ukizingatia nilishaharibu nyuma.


Kila kitu kinaenda sawa sasa hivi japo nilipata tabu sana mwanzoni kumzoea kwani hata hiyo kiss tu ilikuwa tabu kwa kuwaza Ex wangu kila nikiwa nae.

Ila nikaanza kuzoea na alijitahidi sana kwa kuwa nilimweleza ukweli nae alinieleza kuwa pia anajifunza kuwa sawa kwani aliumizwa vibaya na akasema hatopenda tena na kajikuta katika mahusiano.

Wote tuliingia katika mahusiano bila kupendana tofauti tu ni kuwa sasa nampenda kupita kiasi baada ya kuona ni mwanaume mzuri sana, ana moyo mzuri na anatoa nafasi ya mwanamke kuzungumza na kuchangia mambo.

Ni mkweli hanaga longolongo kitu kipo hivi anasema direct hata kama anajua kitakuumiza. Yaani dada dinah kama mume yeye ni zaidi ya mume anafaa.


Tatizo lipo kwake kwa sasa kuwa upendo wake kwangu unakuwa taratibu sana hadi napata wasiwasi na tushakaa tukazungumza na kuangalia possibility za kutengana ila wote tunaishia kulia na kubembelezana kuwa tuendelee kujipa muda.


Mie niko sawa sasa nampenda kiukweli baada ya kuhangaika kujifunza tatizo lipo kwake kwani anasema tusiachane atajifunza kunipenda ili afikie level ya kama nimpendavyo mimi.

Sio kwamba hanipendi kabisa ila anakuwa muwazi kusema upendo upo ila mdogo ukiringanisha na wangu kwake.

Kiukweli nampenda ndio na natamani kuwa na mume kama yeye mwenye hofu ya Mungu hasa kwa baada ya kuumizwa vibaya.

Upande mwingine Ex baba wa mtoto  nae anakuja kasi kwa kudai mimi simweshimu kwa kuwa simpi nafasi ya yeye kama baba wa mtoto. Kisa alisikia mtoto nimempeleka shule fulani bila kumtaharifu.

Kiukweli sikuona umuhimu wa kufanya hivyo kama hata centi hatumi na anaweza kukaa miezi hata 4 kimya hajui mtoto anakula nini, analala wapi na ada sh ngapi, anaumwa au mzima.


Anadai tukutane aniambie matatizo yangu kwani analaumu kuwa namtreat vibaya na simpi nafasi kama mwanaume na pia siwi kama wanawake wengine wanaoheshimu wanaume zao.


Nani mwenye matatizo kati yetu? maana ananilaumu kuwa si mama mzuri pia sasa sijui anataka niact vipi? na je kuhusu Msabato unaweza kuniambia kama dini ni kikwazo cha hayo yote?

Naomba pia nifahamu kwa mwanaume anaweza kujifunza kumpenda mwanamke na akaweza?

Na je muda gani anaweza kuchukua kujifunza? nifanyaje kwenye situation hii niendelee kuvumilia au nirudi nyuma?


NB:Kama ni kuchagua mwanaume ningemchagua Msabato ila tu simwelewi anaposema anahitaji kujifunza zaidi kupenda.

NAHITAJI MSAADAWAKO DADA DINAH KWANI NAONA UMRI WANGU UNASOGEA NAZEEKA SASA NA SINA MWELEKEO WA MWANAUME GANI SAHIHI KWANGU…

Wako katika mawazo.

*********

Dinah anasema: Salama kabisa Mpendwa na shukurani kwa kurudi tena baada ya Miaka.


Tuanze na huyo Ex king'ang'anizi asie na utu, heshima, adabu, haya wala aibu.

Fanya yote lakini usirudi kwa Ex, sana sana utakuwa "second best" na utaishia kujilaumu au kuumia zaidi. Kashindwa huko alikokuwa ndio anataka kurudi leo? Tena kwa lawama na kukufananisha....hana heshima kwako in what so ever!

Hana aibu wala haya kukulaumu kuwa wewe sio Mama mzuri wakati umelea Mimba peke yako, Umejifungua peke yako na unamelea mtoto mwenyewe.

Ukampa nafasi ya kuwa karibu na mtoto wake lakini hakuijali kwani alichokitaka yeye ni "kuipoteza" Mimba ili aendelee kula ujana......


Mtoto akikua na kusikia kuwa baba yake hakutaka azaliwe (alimkana alipokuwa Embryo) ndio atakapo jua nani Mzazi mzuri na nani useless.


Mbaya zaidi anakulinganisha na wanawake wengine, jinga kabisa na hafai kuwa baba wala mume....he's an example of a man. The shenzi kabisa tena akafie mbele kwa mbele huko na ukoo wake.(Huh! I hate Exes that's all)

Sasa onto Msabato Guy: Wasabato sana (Level ya Ulokole) nao bana, wengi wanapenda kuoa Bikira ka' Waarabu wakisha Oa wanaanza "kutumbukiza" nje ya ndoa ka' wameioa Dunia....

Pamoja na kuumizwa sana na Ex wake hali inayoweza kumfanya ashindwe kuamini mwanamke yeyote pia nadhani huyu Msabato wetu kashikiliwa zaidi na Jamii ya Kisabato (wanakaubaguzi fulani hivi ka Dini)....sasa nadhani hilo linaweza kuwa tatizo kuu.

Je, anachukuliaje suala zima la wewe kuwa na Mtoto kabla ya ndoa? Je umewahi kuhoji kama mtoto anaweza kuwa tatizo kwenye Usabato wake?

Kama mmewahi kujadili au "kutishia" kuachana na mkaishia kulia ni wazi kuwa mnapendana na mnahisi hamuwezi kuishi bila each other(how sweet).


Hakuna muda wa kujifunza kumpenda mtu, ni unampenda au humpendi....hisia za mapenzi huongezeka/hupungua jinsi mnavyozidi kuzoeana na kugundua kasoro, habits n.k....lakini kama umependa kiukweli utajifunza kuishi na Kasoro zake kwani hakuna aliekamilika.


Hawezi kukupenda wewe kama unavyompenda yeye kwasababu ninyi ni watu tofauti kwa kila kitu....kuanzia Jinsia mpaka interests.

Kwenye uhusiano wowote wa kimapenzi lazima kuna mmoja atampenda mwezie zaidi....kamwe hamuwezi kupendana kwa level sawa, ila naweza kupenda idea, vitu au jambo kwa kiwango sawa.


Inaonyesha pia Msabato wetu bado hajamaliza hisia za maumivu aliyopata kutoka kwa Ex, hali hiyo inamfanya ashindwe kuendelea.


Wanaume wengi hawapendi kuachwa na wakiachwa huamua kwenda kulala na wanawake tofauti tofauti na baadhi huchagua mmoja ili kujipoozea mpaka machungu yamuishe.


Sasa kwa vile Msabato wetu Usabato unamzuia kufanya kama wanavyofanya wanaume wengine inamchukua muda mrefu kupata "uponyevu". Kumbuka Mwaka mmoja sio muda mrefu kihivyo.


Hamuwezi kuwa na interest zinazofanana kwani ninyi ni watu tofauti muhimu ni kila mmoja wene ku-support interest za mwezie au ukishindwa basi unamuacha na interests zake na wee endeleza zako.


Mimi nakushauri uendelee na huyo Msabato, kwa vile ni muwazi basi ni vema na wewe kuwa wazi kwake....kama issue ni mtoto, wewe kubadili Dini, Mawasiliano na Ex, Jumuiya ya Wasabato kanisani kwake, Wazazi wake(wasabato) n.k.


Kumbuka wanaume hawapendi mwanamke aendeleze mawasiliano na Ex hata kama mtoto anahusika....hebu tafuta ukweli na ikitokea Ex anamkwaza (anahofia kuwa na wewe ni kuwa na Ex pia) basi "ua" mawasiliano nae.

Since Ex hakuwepo tangu mtoto kazaliwa na mtoto hamjui kama Baba yake huna haja ya kuwasiliana nae. Mtoto akikua atamtafuta baba yake (akitaka).

This is 2014, at 28 wee bado katoto kabisa....Uzee ni jinsi unavyojichukulia sio miaka (namba)....

Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments

Anonymous said…
Kushauri ni kipaji, huwa nafarijika sana ninaposoma blog yako na jinsi unavyowashauri walengwa, ubarikiwe sana dada DINNA.
Anonymous said…
Shogeer uyoo ex anakurudisha misri,i like the way u think,think like a man act like a lady songa kanani kwa ex ucjarib
Anonymous said…
Pole Sana dada