Mke ana Wivu, je nimtaliki?-Ushauri

Habari za kazi sister? Mie nina miaka sawa sawa na Chama Tawala. Nimeoa nimebahatika kupata watoto wawili, wa kwanza miaka minne na wapili Miezi Mitatu.

Mke wangu amekuwa na Wivu kupita kiasi, nimejaribu kumueleza anakokwenda siko lakini haelewi.

Nimemgawia nyumba 3, moja ya kuishi, gest na nyumba ya wapangaji na kumpatia Lorry Scania ajitegemee kwani nimechoshwa na tabia za wivu lakini hataki.


Ukweli mie sina mchepuko, nataka niachane nae niendelee na biashara zangu. Naomba ushauri wako nifanyeje? naomba usitoe jina langu.


****************


Dinah anasema: Njema kabisa Brother, nashukuru.


Sasa ndugu yangu biashara na familia si ndio zinapaswa kwenda sambamba....kwamba unatafuta kwa ajili ya familia yako eti?!!


Ukimuacha mkeo kwa sababu inayorekebishika(au ya muda) huoni kuwa utakuwa unawaonea yeye na kuwaumiza watoto wako pia? Umri wa watoto wako ndio umri ambao wanahitaji upendo na uwepo wa Baba na Mama.

Huo wivu wake umeanza au kuongezeka lini? Ni baada ya kushika mimba ya 2 au baada ya kujifungua?

Maana wakati mwingine Mabadiliko ya Homono wakati wa Mimba na baada ya Mimba yanaweza kusababisha makanganyiko wa hisia na tabia kwa ujumla.


Inawezekana sio Wivu bali ni uoga wa kuwa peke yake na watoto wawili, usikute anakuwa paranoid akiwa peke yake (Usiseme umemuwekea msaidizi, msaidizi sio mumewe....hana connection nae kama mpenzi).


Pia kuna Ugonjwa wa Akili unaowapata Wazazi baada ya kujifungua (Post-natal Depression)....isije kuwa mkeo anaugua bila yeye/wewe kujua.


Ni Ugonjwa unaowapata wanawake wengi (mimi mwenyewe mmoja wapo) na dalili zake wakati mwingine sio zile ambazo zinajulikana na kila mtu kwani watu tunatofautiana.


Siku mkeo ataja kujiua na pengine kuua watoto na wewe utasema "wivu ulimzidi" lakini ukweli sio Wivu bali ni tatizo la akili.


Mkeo bado ni Mama mpya, amejifungua miezi 3 iliyopita bado mwili na akili havijakaa vizuri then boom unatishia kumpa Talaka.


Haitaji stress zaidi kwenye akili na mwili ambao tayari umechoka. Kama mume wake Unahitaji kumuelewa (hata kama huelewi jifanye unamuelewa), kumuonyesha mapenzi na kumhakikishia kuwa unampenda.


Badilisha ratiba ya Shughuli zako ili utoe attention kwa mkeo, sio kila leo unarudi usiku wa manane.....tafuta siku 3 tofauti katika wiki ambapo unarudi mapema na kuwa pamoja kama familia.


Tatizo la mkeo linarekebishika/tibika kama mtashirikiana na kuboresha mawasiliano yenu kama wapenzi na sio Baba na Mama.

Pia ni vema kwa wote ku-share hofu zenu kwenye uhusiano wenu kwa mtu wa tatu ambae sio ndugu wala rafiki bali aliewafungisha ndoa au Mtaalam wa masuala ya Familia na Ndoa (sina hakika kama Tz wanapatikana), wao watawasaidia kwa ukaribu na ulevu kutoka pande zote mbili.

Mali na Pesa hazina maana kwake bali kuwa na wewe na kama ana Ugonjwa wa PD Mali na Pesa ndio hazionekani kabisa(haoni umuhimu wake)!


Ikiwa hana PD (Daktari wa Magonjwa ya Akili kathibitisha) then Mali na Pesa havina nafasi linapokuja Penzi lake kwako.


Sidhani kama Mkeo ana Wivu ule wa "kuchosha" nadhani huwa Paranoid (moja ya dalili ya PD) unapokuwa mbali....


Nashauri muende kumuona Daktari wa Magonjwa ya Akili ili kuwa na uhakika kuwa yupo salama (hii hali inaweza kujirudia au kujitokeza baada ya miezi michache hadi mwaka baada ya kujifungua).


Kama hana PD then kwa pamoja mfanyie kazi uhusiano wenu na mjaribu ku-compromise.


Kama Biashara zako haziruhusu kuwa na muda wa kuwa na mkeo kipindi hiki ambacho mimi nadhani ana issues kiakili ni vema kuomba msaada kutoka kwa Mkwe (mama yake) au ndugu yake ambae wanaelewana na aje hapo kuwa nae karibu.


Mtoto wa miezi 3 akifikisha Mwaka na mmefanya niliyogusia hapo juu lakini bado Mkeo ana "wivu wa kuchosha"...then err Vumilia....fanya uamuzi ambao hautoumiza hisia za watoto wako wala Mkeo.


Kwa umri wako huoni kuwa unakila sababu ya kuwa karibu na Familia yako? Jiulize ni Legacy gani utawaachia wanao? "Chuki" kwa kumuacha Mama yao bila kosa (Wivu sio kosa)....kuwapa mafunzo mema na mifano mizuri Kama baba?


Mali na Pesa haviwezi kuziba muda waliokosa kucheza na kujifunza kutoka kwako.


Mali na Pesa hazitojibu maswali yao na hazitoondoa "Chuki" watakayoijenga kwako kutokana na Sababu ya uliyoitaja ya kumuacha Mama yao.


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments