Hatukuzaliwa waaminifu, tumejifunza...

Umewahi kusikia mtu akimtetea "rafiki" au mtu anaefahamiana nae wa jinsia tofauti kuwa anamke/mume/Mpenzi hawezi kufanya chochote?


Walio kwenye Ndoa/Uhusiano ndio washenzi wa tabia kuliko wale ambao ni "single"....labda kwa vile mara nyingi (tumeaminishwa) kuwa mwanandoa/uhusiano akitoka nje ya ndoa yake na "m-single" mwenye kosa ni yule aliekuwa "single".

Wakati mwingine wanandoa kwa wanandoa wanakubaliana ku-switch "mahusiano" illegally....kwamba wote wanawatenda wenza wao.


Walio kwenye ndoa/uhusiano ndio mwenye jukumu la kulinda ndoa/uhusiano na sio yule aliekutokea/kubali ambae ni single, kataa kama kielelezo cha Heshima kwa Mwenza wako na Watoto.


Mimi binafsi siamini mtu yeyote iwe kaoa au kaolewa, haina maana kuwa simuamini Mume wangu la hasha, namuamini sana tu ila sio kwa asilimia zote(hihihihi Mjini hapa + hizi sosho media hizi, akuu...).


Hakuna mwanadamu kazaliwa na Tabia njema (Uaminifu unatokana na tabia njema ya mtu), sote tunajifunza/tumejifunza kutokana na mazingira tuliyokulia na Malezi kutoka kwa wazazi wetu.

Since hatukulelewa pamoja na hujui mwenzio alikulia mazingira gani, huna sababu ya kumuamini kwa asilimia zote....


Wale waliooa au kuolewa na hao ni wake/waume wao wa kwanza ndio huwa hatari zaidi baada ya miaka kadhaa ya Ndoa, maana hawajui "mwingine" zaidi ya huyo alienae.


Sina maana watu muanze Umalaya au u-Serial dating wa kutosha kabla ya ku-settle, hapana. Najaribu kusema pitisha angalau mmoja, kula nae maisha (ujue mwili wako) kabla hujafunga ndoa....kwa mfano.


Na huyo mmoja ujitahidi kujaribu nae as mambo mengi as possible ili ukijaku-settle usidhani wanaume/wanawake wote wako hivyo au hawako hivyo na huyo ulie nae ndio funga kazi.


Kumbe waaapi bana....siku ya siku unakutana na Blog hii(mfano tu, usipaniC) then unahisi "umepitwa" kweli....ukaanza kutamani kutoka ili "ujionee" na kuumiza mwenza wako na watoto.


Ni vema itambulike kuwa ili kuwa na uzoefu huitaji kuwa foleni ya Exes, Mmoja tu in your life anatosha...yaani wa Kwanza na atakaefuata (wa pili) ni Mumeo.


Muhimu ni kuwa makini kabla "hujajikita" kwenye uhusiano na mtu(ili kuepusha namba kubwa ya Exes....!


Sasa huyo wa kwanza jaribu yote ambayo unadhani ni muhimu (kuchelewa kuanza nako kunasaidia), jifunze as much as unaweza kabla hujaingia kwenye uhusiano (na kushiriki Ngono).

Hapo mwisho nimelenga zaidi wadogo zangu waliopo Early 20s....


Kila la kheri.
Mapendo tele kwako...

Comments