1st Love, Unasahau vipi ili Usonge...

Pole na kazi dada. Mimi ni mwanaume nina miaka 25 nimewahi kuwa na mpenzi mmoja ambae nilianza nae mapenzi nikiwa Mwaka wa kwanza Chuoni.


Nilikuwa nakutana nae kila ninaporudi likizo tu nyumbani Morogoro maana yeye alikuwa Form 4 katika shule ya Wasichana hapa Morogoro.

Tulipendana sana kama hatutakuja achana.Tulikuja achana mwaka jana mwezi wa tatu wakati mimi namalizia Chuo nae anamaliza Form 6 sababu alidai kuwa tumezidi gombana.

Mimi huwa napenda tukubaliane kitu na tuishi kadri ya makubaliano yetu. Tuliacha kuwasiliana kabisa kama miezi 3 hivi. Nikiwa nyumbani baada ya kumaliza chuo, nawaza ntapata kazi lini na wapi nikaona sms yake ananisalimu. Kwavile nilikuwa na hasira nae sana niliishia kumtukana.


Alipo kuwa anakwenda Chuo Mwanza, tukawa tunawasiliana ambapo yeye ndio alikuwa akinitafuta. Kwasababu nampenda sana nikawa nami namtafuta. Tukawa kama tumerudiana maana alikubali kuja kunitembelea ninakofanyia kazi.

Alikuwa amenitambulisha na kwao japo sio rasmi ila nilikuwa nafahamika. Anadai hana mpenzi ila baadhi ya siku simu yake bisy sana nikimuuliza anasema anaongea na rafikize.

Nikiwasiliana nae akirespondi vibaya naumia hadi najilaumu kwanini nimemtafuta lakini kuacha nisimtafute kabisa nashindwa.

Nikiwaza kuwa na mwanamke mwingine nafsi inaniuma nashindwa kuwa na mahusiano na msichana mwingine.

Dada nisaidie, nifanyaje niweze kumsahau na niwe huru kupenda msichana mwingine? Maana nikiacha kuwasiliana nae kwa muda yeye hunitafuta.

Yaani dada dinah mimi hata simuelewi. Je alianza kuwasiliana nami kwa lengo la kifuta soo kwangu maana aliniacha kwa maneno mengi. Nilimtumia hadi watu wa kumbembeleza hakutaka kuwa nami.

Au ni kweli anataka turudiane harafu anakuwa muoga?

Au ananizugisha tu pengine kwa kuwa baada ya mimi kaona alikosea kwa maamuzi yake kwamba mimi ni bora kwake?


**************

Dinah anasema: Ahsante na shukurani kwa Ushirikiano.


Aah! Mambo ya 1st love halisahauliki, haliishi nini na nini....eti! Katika hali halisi uzoefu wowote unaupata kwa mara ya kwanza huwa hausahauliki....

....ilikuwa ni mara ya kwanza kupata au kuhisi hisia za kimapenzi....was magical.....tendo likawa very special (not really, it's because hatujui kitu kwa mara ya kwanza).

Utaendelea kukumbuka uzoefu huo kwa muda mrefu sana katika Maisha yako mpaka siku utakapokutana na mpenzi mwenye kukupenda kweli na mwenye kauzoefu....hiyo ndio itakuwa mwisho wa "first love never ends/dies".

Utamkubuka kama wa kwanza na atabaki kuwa hivyo, hakuna zaidi na hautokuwa na hisia nae na badala yake utatambua kuwa "ngono ya kwanza" ndio haisahauliki na sio Penzi.

Humuelewi: Nadhani utoto unamsumbua na bado hajui akitakacho kutoka kwa mwanaume, uhusiano au maisha yake kwa ujumla.

Kwasababu alikwisha kuacha hapo awali nadhani huwa anakutumia kama "kipoza Moyo" ikiwa kakorofishana na Boyfriend au kashindwa kukutana nae kwa mfano. Au anapokuwa Mpweke au down kwa sababu nyingine na anataka kuwa cheered up.


Hii huwa ni solution ya muda mfupi kwa wanawake wengi in 20s ambao hawawaelewi wapenzi wao, wapenzi hawatoi commitment kwenye uhusiano, hawana wapenzi lakini hawataki kuwa na an Ex wanasubiri Mr Right n.k....hukimbilia kwa an ex waliowaacha for comfort.....


Kwa kawaida huwa wanakeep mawasiliano au kusema bado wanaurafiki na Ex kwa sababu hiyo....kuwatumia in the future.


Wakati mwingine hali ikiwa mbaya na upo karibu basi na Ngono utapewa ilimradi tu ajisikie "kutakwa" tena...."Kutamaniwa" au "kujaaliwa" lakini hakuna mapenzi.


Nimejuaje? Well sikuzaliwa tu nikawa in my 30s....nimepita humo.

Kujaribu kutowasiliana nae kwa muda ni hatua nzuri lakini unashindwa kusonga mbele kwa vile yeye bado anawasiliana na wewe(hajafuta mawasiliano yako).


Badilisha namba au m-block kisha futa mawasiliano yake. Anza kufurahia company za wadada wengine kikawaida au kirafiki tu sio kimapenzi.

Taratibu utaanza kupata hali ya kujiamini tena na hisia kwa mwanamke mwingine kwenye mzunguuko wako au mbali zitajitokeza.

Just go out there....have fun, enjoy your life kwa uangalifu though maana Mjini kuna mengi.


Kila la kheri!
Mapendo tele kwako...

Comments