Ni kweli Wanaume wanapenda "Saa sita" Kifuani?


Sina hakika ni kwanini wenzetu (wanaume) wanapenda Matiti wakati sisi (wanauwake) ndio tunaonyegeka ikiwa yatafanyiwa "kazi" vizuri na kwa utaalam. Ukiachilia mbali hilo, matiti hutufanya tuhisi kuwa ni "wanawake" pia ni Mwanzo mzuri wa maisha ya mtoto).

Nakumbuka mara ya kwanza kuvaa Sidiria ilikuwa 2003, sikuwa nahitaji lakini nilidhani kuwa kuvaa Sidilia ndio "uanamke", basi nikaenda kupima size ya Matiti ili kupata "Bra" itakayonitosha vema. Wahudumu wakanishangaa na kusema kuwa ninge-save pesa nyingi kwa kutovaa "Bra" kwani sihitaji, lakini kwa vile nilitaka kujihisi kuwa ni mwanamke nilisisitiza kupata "Bra" yangu ya kwanza....TMI i know, sorry hihihihi....


Katika hali halisi hakuna Mwanaume anaependa kukutana na mwanamke ambae matiti tayari yapo tumboni (inategemea na ukubwa), hiyo haimfanyi mwanaume huyo kuchukia matiti yaliyoanguka ila angependa yaanguke akiwa Mkewe na sababu  iwe ni kunyonyesha watoto wao.


Hebu badilishakibao wewe ndio uwe mwanaume etii....alafu unakutana na na titi zipo tumboni, hapo hajanyonyesha/Zaa, utakuwa hujui raha ya  matiti yaliyosimama na pengine siku moja ungependa kupata uzoefu huo....Hebu fikiri.


Kwa bahati mbaya wanawake wengi kwenye jamii rejea topic ya Jinsi ya kutunza, wengi hujiachia tu kipindi ambacho matiti hayo yanahitaji "support". Hakika Matiti kuanguka ni kutokana na kunyonyesha watoto wa Mumeo, lakini kumbuka kuwa sio Wanawake wote wenye matiti yaliyoanguka wamenyonyesha, Wamezaa, Wametoa mimba au wanawaume/wapenzi....kwamba matiti yao yalianguka kitambo kabla hawajanyonyesha kutokana na kutoyatunza vema.


Ikiwa mumeo alikukuta ukiwa na matiti Saa sita bila shaka ataendelea kuyapenda akijua kuwa wanae waliyatumia "early days of their lives", obviously atakuwa amekubali mabadiliko uyapatayo kutokana na Uzazi....lakini at least aliyakuta Wima na yeye ndio kachangia yatazame Chini (baada ya kunyonyesha watoto).


Ukweli wenye maumivu ni kuwa, Asilimia kubwa ya wanaume wangependa matiti ya wake zao au wapenzi wao yadondoke wakiwa nao na sio wayakute yakiwa hivyo (matiti yamedondoka). Hali inayofanya wengi wao kuzungumzia u-wima wa matiti na kucheka au kubatiza yale yaliyolala kuwa ni Malapa.


Mimi binafsi huwa sipendezwi na hilo na siku zote huwa nasema kabla hujamcheka mwanamke mwenye matiti yaliyolala hakikisha wanawake kwenye familia yako bado matiti yao yapo wima na muhimu kabisa ni je Matiti ya mama yako uliyonyonya bado yamesimama(saa sita)?


Ikiwa kwa bahati mbaya wewe ulichelewa ama ulikuwa hujui namna ya kutunza matiti wakati yananza kujitokeza hakikisha Wanao wa kike wanajua(wafundishe), pia hakikisha unayapa "support" yakutosha unapofanya Mazoezi, Unapo karibia hedhi, unapokuwa Hedhini, utakapo kuwa Mjamzito na wakati unanyonyesha.




Comments

D97 said…
Hellow,dina!habari za kazi,cjaelewa ulvyosema kuyatunza matiti,utayatunza vp kwa kuvaa bra au?Kazi njema
D said…
Hellow,dina.habar za kazi?cjaelewa jjns ya kuyatunza matiti,utayatunza kwa kuvaa bra au?kazi njema
AMINA said…
Ni kweli kabisa kwani saa sita ni nzuri kwa mwonekano. haya ni maoni yangu jamani. kila moja ana maoni yake