Nifuate ndoa nchi nyingine, niache ajira?-Ushauri

"Dada Dinah na wachangiaji wote, tafadhali naomba ushauri au mawazo kwani nipo kwenye kipindi cha kufanya maamuzi magumu.

Nina mchumba wangu ambae tunataka kufunga ndoa, lakini nitakapofunga ndoa nitalazimika kuhama kutoka Nchi moja kwenda nyingine na kuacha ajira yangu.

Kinachonichanganya hasa ni suala la kuacha kazi, yaani mawazo juu ya hilo hunipa maumivu ya tumbo na huonga huniingia.

Naomba ushauri kutoka kwa yeyote aliyepitia hii hali katika maisha yake, asanteni"

Comments

mainno13 said…
dada nakushauri usije kuacha kazi kwa ajili ya ndoa wapo wengi wamejuta.kati ya kaka yako na huyo jamaa anayetaka kukuoa nani ndugu yako?.usiwe mjinga maana mnaweza kuachana siku yoyote ukabaki huna kazi yeye akuiwa nayo.kwa hiyo angalia maisha yako ya baadae hakuna mwanaume anayependa mke tegemezi atakuchoka tu na kukunyanayasa.binafsi nilishawahi shuhudia dada yangu alifanya hivyo mpaka leo anajuta ndio maana nimeguswa kukushauri.
Anonymous said…
Tutajie nchi uliopo sasa na ajira yako, na tuambie nchi utakayohamia.Nimehitaji maelezo hayo kwa sababu wachangiaji wengi tuko nchi nje ya Tanzania hivyo itakuwa rahisi sana kujua kama nchi uliopo ikoje kiajira na nchi unayohamia ikoje kiajira.

Kuna nchi zingine ukienda utasota hata kama una madigrii na kuna nchi zingine ukienda utapata kazi hata isiyo ya fani ulionayo.Na pia kuna nchi zingine zina kipato kizuri zaidi kuliko zingine.Kuna nchi zingine maisha ni magumu sana hata kama ungekuwa na kazi pesa inaishia kula na kulipa pango.

Ukituambia kwa kinaga ubaga uko wapi na unatarajia kwenda wapi ukiolewa tutakupa msaada wenye manufaa zaidi kuliko hivi sasa tutakuwa tunaelea hewani bila real facts.
Hongera kwa kupata wa kuishi naye milele.
Anonymous said…
mi mwenyewe nilitaka kuuliza mana niliacha kazi yangu bongo ambayo ilikuwa inanilipa vizuri kukimbilia ulaya weeeeeeeeeeee najuta kuja ulaya yani usikie ivyoivyo nimekuwa mama wanyumbani full kukaa ndani tu na kwenda supermarketi kazi niliyopata uku ni yakusafisha can u imagine alafu hamna ata sehemu ambayo unaenda uka enjoy kama bongo ulaya full stress ivi natarajia mume anipe msingi nirudi home nifanye biashara uku najitafutia ajira polepole
Anonymous said…
mi mwenyewe nilitaka kuuliza mana niliacha kazi yangu bongo ambayo ilikuwa inanilipa vizuri kukimbilia ulaya weeeeeeeeeeee najuta kuja ulaya yani usikie ivyoivyo nimekuwa mama wanyumbani full kukaa ndani tu na kwenda supermarketi kazi niliyopata uku ni yakusafisha can u imagine alafu hamna ata sehemu ambayo unaenda uka enjoy kama bongo ulaya full stress ivi natarajia mume anipe msingi nirudi home nifanye biashara uku najitafutia ajira polepole
Anonymous said…
Mchangiaji namba 2 amemaliza yote. Toa maelezo kamili. Wengi tupo nje ya nchi wachangiaji, tutakushauri usitieshaka.
Anonymous said…
Jamani ahsanteni kwa ushauri wenu, mimi nataka nimfuate mume UK ila sasa hivi nipo Tanzania.