Mkwe anataka nimuache mwanae ni Hanithi, lakini tumesha-do mara kibao na yuko sawa-Nifanyeje?

"Habari Aunt? Mimi ni mwanamke wa miaka 24,nina boyfriend wangu ambae tumedumu kwa miaka mitatu na plan yetu ni kufunga ndoa. Alipanga kuleta Posa baada ya Mwezi wa Ramadhan lakini cha ajabu mama yake aliwafuata mama zangu wakubwa na kuwaambia kuwa huyo boyfriend wangu si mwanaume, kwamba ni hanithi.

Pia mama yake alinifuata mimi na kunambia kuwa mwanae hana uwezo wa kiume. Lakini mimi na boyfriend wangu tayari tumekutana kimwili mara kadhaa na mimi namuona yuko sawa ila huwa anapiz nje kwa kuwa tulipanga tusizae nje ya ndoa.

Siku nyingine Mama yake kanambia kama siamini basi nijarbu kumtega kwa kumwambia kuwa anipe mimba, nilipomwambia boyfriend wangu anipe mimba alinijibu kuwa yeye yuko tayari. To be honest nampenda kutoka moyoni na yeye ananipenda pia.

Hivi sasa niko njia panda kwani pande zote mbili wanataka niachane nae lakini mimi sijaona tatizo au mapungufu ya mpenzi wangu yako wapi. Kwangu mimi ngumu kuachana nae kwa kuwa tunapendana na tuna plans nyingi tulizopanga na ni za muda mrefu.

Naomba watanzania wenzangu mnisaidie kwa hilo niko njia panda.

Asante."

Dinah anasema:Habari ni njema tu lovey, asante sana kwa ushirikiano. Pole kwa misukosuko ya soon to be mother in law, hapo ni sawa na kujitukana na kujidhalilisha mbele ya wazazi wenzie. Yeye amejuaje kama mwanae hawezi au hana uwezo wa kuzaa? Hata kama huo ni ukweli yeye anahusika vipi na maisha yenu ya ndani ninyi wawili kama wapenzi?

Anyway, Kama walivyo akina mama wengi wenye watoto wa kiume hupenda sana kupata mjukuu pale wanapotaka wao, wengine hutumia neno "sitaki kufa kabla sijaona mjukuu) hivyo hufanya kila jambo ili mtoto wa kiume kuzaa iwe kabla au baada ya ndoa.

Utagundua kuwa, kuna baadhi ya kina mama wakishajua mtoto wao wa kiume anauhusiano utasikia anataka kijana huyo afunge ndoa (hata kama hayuko tayari) na ikitokea akafunga ndoa kutokana na matakwa ya mama, soon baada ya ndoa mama mkwe ataanza kudai mjukuu, akipata wa kike, atataka wa kiume n.k yaani ni kama vile wana-control maisha ya watoto wao wa kiume.

Huyu mama anaposema mwanae ni Hanithi anamaanisha mwanae ni Tasa (hana uwezo wa kuzaa), labda kwa vile kila msichana alietoka nae kabla yako hakushika mimba kwa vile Mwanae alikuwa mwangalifu au hakutaka kuzaa kabla ya ndoa.

Vilevile inawezekana Mama mkwe huyo anadhani wewe ni Tasa kwani umekuwa na mwanae kwa muda mrefu bila kushika mimba (si unajua wazazi wetu wao walitumia Majira na hivyo waume zao walikuwa wanamwaga ndani tu hakuna cha nje wala Condoms)huenda anajiuliza "kulikoni hawa watu hawapeani mimba miaka yote hii" hivyo anataka ushike mimba kabla mwanae hajakuoa.

Sasa huyu mama anachojaribu kukifanya hapa ni kutaka wewe uwe forced na wazazi wako kushika mimba kabla ya ndoa ili ukifunga ndoa baada ya muda mfupi wewe na mumeo mmpatie mjukuu. Kumbuka amekuambia kama "huamini mwambie akupe mimba".

Alafu kwanini wazazi wako wakatae kupokea posa wakati sio wao wanaokwenda kuolewa na huyo Kijana, kwa kawaida binti ndio huwa na uamuzi huo. Kwamba mtu akija kuchumbia kwenu wazazi wanasema watamjibu baada ya muda fulani, then unaitwa alafu unaambia kinachoendelea na wewe kukubali au kukataa (kizamani).

Kisasa wengi tunakuwa tunawajua wachumba (vishwa Pete) kabla ya posa hivyo hata posa ikipelekwa wewe unakuwa wa kwanza kujua na huenda ukawaambia wazazi kuwa wazee wa kadhaa wa kadhaa watakuja kuposa n.k. hivyo wazazi kukataa Posa kwa sababu ya majungu ya mzazi mwenzao sio haki.

Nini cha kufanya:
Hebu kaa chini na mama yako mazazi na uwaambie ukweli kuwa Mchumba wako anauwezo wa kufanya mapenzi kwani tayari mmekwisha fanya mara kadhaa ndani ya miaka 3.

Mwambie "tunapendana na niko tayari kufunga nae ndoa. Sielewi mama mkwe(sijui unamuitaje) anataka nini kutoka kwetu kwani hivi majuzi (itaje siku) alinifuata na kuniambia nimtege mchumba wangu ili anipe mimba, inamaana huyu mama anadhani ukoo wetu ni Tasa?!!"

"Mimi sitaki kushika mimba kabla ya ndoa na ndio maana nimekuwa mwangalifu na kujikinga kwa miaka yote mitatu" (hii trick ya kujifanya victim huku unatoa CHOZI siku zote hufanya miujiza).

Enedelea "Mama naomba mkubali posa ya mpenzi wangu kwani ni mwanaume pekee ninae mpenda na tumepanga kufanya mambo mengi kwa ajili ya maisha yetu na familia zetu, nisingependa kumpoteza mwanaume anaenijali, mwenye nia njema nami na mwenye upendo wa dhati".

Mama yako anakupenda, hakika atakuelewa na atafikisha ujumbe kwa Baba. Ikiwa bado wanashupalia uachane nae basi uamuzi ni wako, Funga ndoa na Mchumba wako bila ya kuwaharifu wazazi wenu na baada ya ndoa ndio wapewe taarifa.

Fanyia kazi maelezo ya wachangiaji wengine pia,
Kila la kheri!

Comments

Amos Bwire said…
Duh, hicho ni kituko cha karne!
Swali: kwanini usimwambie mama mkwe na hao ndugu zako ya kwamba jamaa anasukuma nyama vizuri kabisa? Mbona hiyo ingerahisisha mambo? Au huyo mama anakuhisi we mgonjwa nini? Maana huenda anajua utamuulia mwanae kwa hiyo anakutishia ili umwache mwanae. Si unajua wamama wanavyokuwa sensitive kwa wakwe zao wasiowaelewa vizuri kitabia?
Anyway, kama matatizo ni ya huyo mama kikwelikweli, basi yangu ni haya:
1. Yawezekana huyo mama anachanganya kati ya "msenge" na "hanithi." I mean, maybe huyo mama kashuhudia mara kadhaa huko nyuma jamaa akilawitiwa. Kwa hiyo mama akahisi kuwa ndio imetoka hiyo.
2. Wamama wa kiswahili wana imani flani za kipuuzi. Hawaishi kuwachunguza-chunguza na kuwatega watoto wao wa kiume, tokea utotoni. Sasa huenda huyu mama kajaribu vile vimchezo alivyofundishwa na bibi na shoga zake, vyote vimefeli, kwa hiyo kaibuka na conclusion hiyo.
3. Yawezekana huyo mama kishalala na huyo mwanae mara kadhaa na kujaribu kufanya naye ngono. Lakini kwa kuwa jamaa hamfeel kabisa mamaake, huenda mboo imegoma kusimama. Kwa hiyo mama akajua jamaa si rizki.

All in all, kama jamaa yuko fresh kabisa na wewe unakerwa kiukweli na hizo stories, MWAMBIE jamaa. Lazima ataenda kumalizana na mamaake na hautamsikia tena huyo mama akikuletea huo ujinga!
emu-three said…
Hapo uamuzi mkubwa upo kwako, kwani umehakikisha kuwa wanayokuambia ni ya uongo,sasa ni wewe kusuka au kunyoa!
Mapenzi ni ya wawili wapendanao, na ukipenda, hakuna chochote utakachosikia kwani ukipenda chongo utaliita kengeza.
Cha muhimu, sijuii kwaninii mama mkwe wako huyo anataka kuwatenganisha, ila kama ingekuwa mimi ningempeleka boy friend wangu kwa dakitari athibitishe kitaalamu, halafu hivyo vipimo nampelekea huyo mama mkwe, na kumuomba anijulishe sababu kubwa za kutaka nisiwe na mwanae.
Nasema hivi kwasababu mkioana, ujue mama mkwe wakoo huyoo atakuwa mama yako, na muda mwingi mnaweza kuwa naye, sasa ni vyema kuondoa hiyo sintofahamu mapema, ili mbeleni muishi kwa raha!
Ni hayo tu
Anonymous said…
Hapo dada angu mi naona ni kitu rahisi na jibu unalo kabisa. Kwanza kabisa kitu cha aibu mama kumsema mwanae wa kiume ni hanithi bora angesema baba wa huyo mpenzi wako. Je akiwekwa kitimoto huyo mama na akiulizwa amejuaje kuwa mwanae ni hanithi atajibu nini?????? kama sio itakuwa matusi na aibu. In short usiumize kichwa wewe ndio umeshamjua vizuri mwanaume na umekiri yuko fit hata kama angekuwa hanithi kweli kama unampenda we endelea nae tu. huyo mama muweke mbali kabisa labda kama ana kitu kingine labda hataki uolewe na mwanae hapo taelewa lakini zaidi ya hapo we komaa na huyo mwanaume kama vipi mfunge ndoa mzae.Tabia chafu kabisa ya huyo mama looooooH!!!!!!!!
Anonymous said…
Dada, hujaeleza mambo ya msingi ambayo yatamwezesha mtu kukupa ushauri. Kwa mfano hujatuambia kama umeongea na huyo bf yeye anazungumziaje. Kama hujaongea naye, basi ongea naye. Pili hujasema huyo mama mkwe wako alijuaje kama mwanae ni hanisi. Nafikiri hili ndo lingekuwa swali la kumuuliza. Tatu umechanganya kuhusu u-hanisi na uwezo wa kumpa mtu mimba. Unamaanisha huyo jamaa anaweza kusimamisha lakini hana uwezo wa kuzalisha au vyote viwili. Hebu jaribu kuwa clear
Anonymous said…
Kifupi ni kwamba mama wa mumeo huenda hajakupenda. Au huenda kuna binti mwingine ambae wanataka kijana wao amuoe. Balaa, ama kweli inatisha. Pahala kama hapo mara nyingi ni hatari kwako na maisha yako na furaha yako. Mueleze bayana mpenzi wako na muombe muachane laa sivyo akupe hatma ya uchumba wenu. Kumbuka Uzinzi si katika mambo wafanyayo watu wema, ipo siku utakugharimu.
Anonymous said…
Binti inaelekea huyo mkwe hakupendi wewe na wala siyo suala analolieleza la boyfriend wako.

Kwa hiyo la muhimu maadamu ninyi mmemegena siku zote na kutoshelezana endelea na safari yako kama yuko fit katika agency hiyo usikubali kusikia chombezo la mama mkwe.

mama mkwe ana lake jambo.kaza kamba mdada.
Anonymous said…
Muulize mama yake amejuaje kuwa mtoto wake ni hanith. Huyu mamao hataki uolewe na mtoto wake anmekutafutia sababu tu
Anonymous said…
Du! hiyo kali sijawahi kusikia we kaza buti!
Edamo said…
Kama nimekuelewa vizuri hakuna haja ya kuumiza kichwa sana hapo kuna mambo mawili ya kufanya
1.Chunguza mahusiano kati ya kijana na mama yake maana inawezekana huyo mama hataki kijana wake aoe kwa sababu anazojua yy ndo akatafuta namna ya kukuepusha nae.
2.Inawezekana huyo mama hakupendi ndo maana akaamua kukuambia kijana wake si mzima.
Nimezungumzia hayo mambo mawili kwa kuwa hata kama huyo kijana ni hanithi mama yake angekuwa anampenda asingethubutu kusema maungufu ya kijana wake kwa mchumba wake na ndugu zake.Labda huyo mama ni mshirikina na ana masharti yasiyoruhusu huyo kijana kuoa au labda anatembea naye.Vilevile inawezekana hapendi uolewe na kijana wake.Utatuzi wa haya yote utapata kwa kumshirikisha mpenzi wako na muhoji kuhusu uhusiano wake na mama yake pamoja na historia yao yote kama familia zenu hazifahamiani.Usifanye uamuzi wa papara maana utaweza kukugharimu.Baada ya uchunguzi ndo ufanye uamuzi na ikitokea kuwa huyo mama anamsigizia mwanae ujue utahitajika kuwa makini naye sana katika maisha yako.
Edamo said…
Kama nimekuelewa vizuri hakuna haja ya kuumiza kichwa sana hapo kuna mambo mawili ya kufanya
1.Chunguza mahusiano kati ya kijana na mama yake maana inawezekana huyo mama hataki kijana wake aoe kwa sababu anazojua yy ndo akatafuta namna ya kukuepusha nae.
2.Inawezekana huyo mama hakupendi ndo maana akaamua kukuambia kijana wake si mzima.
Nimezungumzia hayo mambo mawili kwa kuwa hata kama huyo kijana ni hanithi mama yake angekuwa anampenda asingethubutu kusema maungufu ya kijana wake kwa mchumba wake na ndugu zake.Labda huyo mama ni mshirikina na ana masharti yasiyoruhusu huyo kijana kuoa au labda anatembea naye.Vilevile inawezekana hapendi uolewe na kijana wake.Utatuzi wa haya yote utapata kwa kumshirikisha mpenzi wako na muhoji kuhusu uhusiano wake na mama yake pamoja na historia yao yote kama familia zenu hazifahamiani.Usifanye uamuzi wa papara maana utaweza kukugharimu.Baada ya uchunguzi ndo ufanye uamuzi na ikitokea kuwa huyo mama anamsigizia mwanae ujue utahitajika kuwa makini naye sana katika maisha yako.
Anonymous said…
Makubwa hayo. Ila mimi kama naona hapa kuna mambo mawili. Moja, uhanithi na pili kutokuwa na uwezo wa kusababisha mimba. Yawezekana huyo mama anachosemea ni kwamba huyo mwanae hana uwezo wa kusababisha mimba ila jogoo anasimama na kuwika kama kawaida.
Dada kaa karibu na mama mkwe wako muulize vizuri anamaanisha nini kusema mwanae hanithi? Mueleze kwamba nyie mnafanya ngono bila tatizo lolote.
Kama shida ni kutoweza kusababisha mimba ni tatizo linalotibika na mama kama mama hatakiwi kutoa siri za mwanae hivyo. hiyo ni siri, ingekuwa ni kwa ajili ya kila angekuwa amesema yeye mwenyewe.
Vinginevyo huyo mama hakutaki kwa sababu zake mwenyewe na ameamua kukutisha.
Anonymous said…
Rudi kwa huyo mama mkwe mwambie una maswali ya nyongeza,muulize kama kaona huyo mwanae akilawitiwa kama hapana muulize kajuaje mwanawe hadindi?,na pia imekuwaje ahisi mwanawe hawezi kumpa mimba mwanamke kama kasema hadindi? Majibu yake yatakupa mwanga ili uweze kuamua uendelee na huyo mwanae awe uachane nae.
Anonymous said…
MAKABILA TUNATOFUTIANA!! KWA BAADHI YA MAKABILA HUYO MAMA MKWE ANGEADHIBIWA KIFO KWA KULALANA NA MTOTO WAKE WA KIUME KWANI ANAWEZAJE YEYE KAMA MAMA KUJUA KWA UFASAHA NA UHAKIKA KUWA MWANAE NI HANITHI. MAMA LAANA SANA HUYU.KAMA MWANAE NI SHOGA HILO LIKO KATIKA UAMUZI WA MSICHANA AU MUOLEWA MWENYEWE
Anonymous said…
Kuzaa ni Majaliwa jamani Kama mmependana owaneni kama alivyosema mwengine huyo Mama aulizwe kajuwaje mwanae Hanithi? hata kama Hazai si anaweza na mmependana wangapi hawajazaa duniani? Kumbukeni mengine majaliwa angalau huyo hatafuti wanaume wenzake. MZ