Nimerudi, samahani kwa kukutenga!

Habari za leo mpenzi msomaji, mtembeleaji na mchangiaji wa D'hicious, nafurahi kusema kuwa nimerudi tena mahali hapa baada ya kupotea kwa muda wa wiki chache kutokana na mishughuliko ya kikazi (safari za hapa na pale) ambazo zilininyima muda wa ku-publish post mpya na kujibu maswali yaliyokuwa published.

Naomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na kutokupatikana kwangu. Namshukuru Mungu nimemaliza salama na sasa nimepata muda wa kuwa nawe tena.

Vilevile napenda kukufahamisha kuwa sito-publish maswali yote yanayozungumzia au kugusia ngono kwa undani kwa muda (Mwezi huu Mtukufu) ili kuepusha vishawishi na pengine kuharibu Funga za wenzetu Waislamu.

Asante sana kwa ushirikiano wako.

Mwenye upendo na kujali,
Dinah.