Mpenzi ni Mbabe, kosa lake mimi ndio niombe radhi-Ushauri

"Habari dada dinah,
Pole na hongera kwa kazi yako nzuri kwani tunajifunza mengi.

Dada dinah, mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 28 na nina BoyFriend wangu ambaye niko nae takribani miaka 6 japo hatujaoana kwani yeye bado anasoma. Kwa ufupi tulisoma wote ila kutokana na sababu mbali mbali nimemtagulia na sasa nafanya kazi.

Mahusiano yetu yamekuwa ya vuta nikuvute kutokana na sababu mbali mbali za hapa na pale japo tatizo kubwa ni WIVU na UBABE alionao BoyFriend wangu, mara nyingi amekuwa mgumu sana yeye kuomba hata samahani pale anaponikosea badala yake hugeuza kosa kuwa la kwangu.

Ili kuepuka ugomvi na mambo yaishe naishia kuomba mimi samahani. Niseme ukweli tunapendana na ktk upelelezi wangu sijawahi kusikia hana mtu nje zaidi yangu japo siwezi jua mambo ya wanaume.


Mara kwa mara amekuwa akidiriki kusema maneno ya fedhea na hata kunitukana. Pia mkipanga appointment muda fulani tukutane yeye anachelewa sana na anaweza akafika baada ya masaa hata 3. Kwakweli huwa nashindwa kuzificha hasira zangu na kujikuta nachukia (kununa). Nimuulizapo hunigeuzia kitabu lakini hawezi kusema samahani, Mimi hiki kitu kinanikera sana.

Siku moja alikuja chumbani akitaka mambo fulani, kama kawaida ya wapenzi kutaniana basi alitaka kufunga pazia nikamkataza na baadae aliporudi kitandnani nikamwambia kafunge. Kwa hasira alinyanyuka na kutaka kuondoka.

Nilipoona hivyo nikamvuta nikamwamia "hutaniwi"! Cha ajabu alinisukuma na kuniburuza nikiwa NAKED huku akielekea kufungua mlango wa nje na kisha akaondoka zake. Kwa kweli iliniuma sana n akuaibika kama pale nje kungekuwa na mtu.

Baada ya muda nilimtumia msg kuwa ktk mahusiano yetu amenionyesha picha halisi yeye ni mtu namna gani. Wadau hakujibu na tulichuniana takribani wiki 2 mpaka pale mimi nilipomwambia aje home. Tukiirudia topic ile lakini kama kawaida yake hakuomba samahani na kuniuzia kesi mimi.

Siku nyingine tulikubaliana tukutane Town ili nichukuwe pesa fulani kwani yeye alinisisitiza kuwa anashughuli nyingi hivyo niwahi. Ni kweli nilijihimu mida ya saa moja nikawa nimefika. Nilipompigia simu alidai bado amelala. Honestly niliumia na kwa hasira niliondoka nikarudi home. Wadau huyu mpenzi hakusema lolote wala samahani mpaka leo, baadae alinipigia simu mida ya saa 6 akiuliza niko wapi. Nilimjibu niko home.

Kutokana na tabia hii, nipatapo nafasi ambapo tukio kama lake linaweza kufanyika basi na mimi humlipiza ili aone uchungu wake. Huwezi amini huja juu na kulalamika kuwa ni kwanini nafanya vile, hapo ndipo ninapopata nafasi ya kumuliza je ni vibaya? Na je wewe uliponifanyia hivi uliona ni sawa?

Dada dinah, yeye huishia kusema niache kulipiza kisasi, Hata mimi humwabia kama hutaki kutendewa basi jirekebisha. Niliamua kuliweka hili suala mezani na tukalijadili kwa kina kama wapenzi lakini alihishia kusema atabadilika japo mpaka leo sioni mafanikio.


Nimechoshwa na hii tabia, yaani nimekuwa mtu wa kulia na kuumwa vidonda vya tumbo sababu ya hasira. Imefikia hatua anatoa maneno yake ya kejeli eti mimi na yeye nani mwanaume?anadai tutashindana mpaka lini?

Kununa nuna ndio haswaa, kwani hasione nina marafiki wakiume hata akiwa mfanyakzi mwenzangu. Kafanya juu chini niachane na nabest zangu wanaume ila nimegoma. Imefikia hata hatua tukienda kwenye fuction yoyote kama harusi basi mambo huko hayaendi tutanuniana mpaka tunarudi nyumbani, kisa watu wamenihug.

Dada dinah na wadau wote nisaidieni kwani nimechoka, mara nyingine nawaza kuachana nae ila naogopa magonjwa na kutengeneza CV za wanaume. Nifanye nini jamani? Naamini hakuna kitu kizuri kama kubembelezana na kuombana msamaaha pale mwenzi wako anapokukosea. Pia nimechoka kuona natendewa mimi na nishiwa mimi kupiga magoti kuomba samahani.

Nishaurini wadau kwani hayo ni machache tu."

Dinah anasema: Asante sana mpendwa kwa kuniandikia na kwa ushirikiano, kutokana na maelezo yako nadhani huyo jamaa hakulelewa kwenye mazingira ya nidhamu kwamba hajui kusema asante wala samahani.

Watu waliokulia kwenye mazigira hayo ni vigumu sana kwako kujua umuhimu wa shukrani na kuomba radhi, vilevile jinsi wanavyokuwa na kuwa na wapenzi huwa ni wagumu sana kusema "nakuepnda", "nimekukumbuka" "ninafuraha sana kuwa nawe" na wengine kuwa wabinafsi linapokuja suala la ngono.

Miaka sita kama wapenzi bila ndoa ni mingi mno yaani mmezoeana kupita kiasi na hivyo kulichukulia uhusiano wenu kama kitu mlichokizoea na mnashindwa kujitoa pamoja na kuwa wakati mwingine mnahisi kabisa kuwa " sasa basi, huyu mtu hanifai" lakini mnashindwa kufanya uamuzi na kusonga mbele kila mmoja wenu na maisha yake. Hilo moja.

Pili, mpenzi wako bado ana-elements za Mfumo Dume, yeye kuwa shule na wewe kufanya kazi (kuwa na kipato) n wazi anatishika nakuhisi kuwa haeshimiwi kama mwanaume na ndio maana amekuwa na maneno ya kashfa na hata kukuuliza wewe na yeye mwanaume ni nani? hii inaonyesha ni kiasi gani anahofia kupoteza "Uanaume wake".

Nini cha kufanya: Tangu umechoshwa na tabia ya huyo Mpenzi wako ningependa uondoe hofu ya kutengeneza CV ya wanaume kwani ukijipa muda wa kutosha wa kupumzika kutoka kwenye uhusiano wa muda mrefu na huyu Kijana wa sasa ni wazi utakutana na kijana mwingine na mkapendana nakuishi vizuri tu kama wapenzi na hatimae mkafunga ndoa.

Uoga mwingine ulionao ni "ugeni" wa kuwa single tena baada ya kuwa kwenye uhusiano kwa muda mrefu, hujui namnagani ya kujichanganya na hata nini cha kujibu ikiwa mtu atakutokea n.k., lakini ukijipa muda wa kutosha hakika utakuwa ok na utafurahia maisha yako wewe kama wewe.

Bado binti mdogo, unajitegemea kiuchumi na unajua nini mapenzi (umeonyesha wazi kwa kuishi na mtu mmoja kwa muda wa miaka sita na kuvumilia yasiyovumilika).....you can do better than that baby Girl.

Kila la kheri.

Comments

Anonymous said…
YAANI WEWE MIMI NAONA UNANITIA HASIRA TU HAPA, YAANI NATAMANI NINGEKUWA KARIBU NAWEWE NIKUZABE HATA VIBAO.

HIVI NYIE WANAWAKE NI KWELI KUWA KIONGOZI WENU NI KIPOFU NA MWALIMU WENU ALISHAFARIKI KITAMBO? HIVI NI LINI MTAZINDUKA NA KUJITAMBUA KUWA NI WATU WA THAMANI SANA KULIKO KIUME CHOCHOTE DUNIANI? HIVI NI LINI MTAJITAMBUA KUWA KAMWE HAMSTAHILI KUNYANYASWA WALA KUNYANYASIKA?

MAPENZI GANI YA KIJINGA KIASI HICHO MPAKA USHINDWE KUJITAMBUA KUWA HAPO ULIPO UMEPOTEA SIYO SEHEMU SAHIHI KWAKO? KWANINI UKUBALI KUWA MTUMWA WA MAPENZI KWA JITU KAMA HILO LISILOKUWA NA USTAARABU HATA KIDOGO WALA KUJUA THAMANI YA MWANAMKE?

HIVI ANA NINI CHA ZAIDI ANACHOKUPA AMBACHO WANAUME WENGINE WENGI WASTAARABU WANAOJUA KUPENDA NA KUJUA THAMANI YA MWANAMKE HAWANA?
WEWE DADA UNATAFUTA KUFA MAPEMA SANA KABLA YA UMRI WAKO KWA SHINIKIZO LA DAMU KUTOKANA NA MAUDHI YA HUYO MPENZI WAKO ASIYEJUA NINI MAANA YA KUPENDWA WALA KUPENDA.

IMAGINE BADO WACHUMBA TU HAPO ANAKUNYANYASA KIASI HICHO NA KUKUONA HUNA THAMANI ISIPOKUWA YEYE ANAKUTUMIA TU, SASA UKIINGIA KWENYE NDOA NA MTU KAMA HUYO KWA KWELI CHAMOTO UTAKIONA HASAA UKISHAZAA.

FUMBUKA MACHO DADANGU, KIMBIA MAPEMA ACHANA NA HUYO MTU ATAKUUA KABLA YA WAKATI WAKO KWANI INAUMA SANA KUISHI NA MTU WA NAMNA HIYO KIUKWELI. NAJUA UTAUMIA LAKINI ITACHUKUA MUDA MFUPI SANA KUSAHAU. WANAUME WAPO WENGI WAZURI TENA WASTAARABU WANAOJUA KUPENDA, KUCARE, NA KUJUA THAMANI YA MWANAMKE.

HUYO MTU WAKO ANAMAUDHI SANA NA ATAENDELEA KUUDHI NA KUKUUMIZA MAISHA YOTE KWANI ANAROHO YA UKATILI SANA NA UKAIDI WA HALI JUU. HUYO WEWE UNAMPENDA BUT YEYE HAKUPENDI ILA ANAKUTUMIA TU, NA MAPENZI ANAYOONYESHA SASA NI UNAFIKI TU ILI AENDELEE KUKUTUMIA.

MIMI KWA LEO NAISHIA HAPO NIWAACHIE NA WENGINE WENYE BUSARA WAKUSAIDIE BUT USHAURI WANGU DADA NI HUO KUWA KIMBIA MAPEMA HAPO ULIPO SIYO MAMA UMEPOTEA, HUYO SIYO MTU WA KUBADILIKA NDIVYO ALIVYOZALIWA, NA TABIA KAMA HIYO KAMWE HAIVUMILIKI WALA KUREKEBISHIKA. KAA TULIA UTAPATA MWANAUME MZURI KULIKO HUYO MWENYE MAPENZI YA KWELI ATAKAYEKUPENDA NA KUKUJALI MILELE AMEN.
Anonymous said…
Huyo mpenzi wako ana mambo ya kitoto sio siri. Kwanza ni mnyamyasaji wa hali ya juu ukweli siamini kama umekuwa naye miaka 6. Mana wewe kuendelea kuwa naye umepalilia aone tabia yake ni sahihi na ya kawaida. Not to be mean huyo mwanamme atakuzeesha kabla ya umri wako na kukuharibia mahusiano yako muhimu yote. Mie nakushauri achana naye na wewe walijua hilo, he sounds gay id you ask me.
Anonymous said…
huyo hakufai mpenzi achana nae mara moja kwani ni mtu mkorofi na mkatili sana coz hawezi kukuburuza kisa umemtania asifunge pazia....tht is bullshit....dada yangu ni bora uwe na CV ya wanaume kuliko kukaa na mwanaume asiyekuheshimu wewe kama wewe na hisia zako...sasa hapo ni kwenye mambo ya uboyfriend n galfriend je akikuoa c ndio itakuwa balaa??ni bora ugombane na hilo janaume kuliko marafiki zako coz they will always be there for u come rain o sun....achana nae hana maana!!
Anonymous said…
U dnt deserve dat u certainly need to get out of dat relationship its not healthy at all. Mwanaume anayekupenda ni mwepesi wa kuomba samahani kwani hataki kukupoteza am not sure kama huyo mwanaume anakupenda u dnt have to stay katika uhusiano ambao haufai kisa unawoga wa kuongeza CV za wanaume umenichekesha kweli na kunisikitisha. Get out wala usiangalie nyuma huo uhisiano kwa jinsi ulivyouelezea ni one side huo kwani hapo naona wewe unampenda kuzidi maelezo na yeye tayari anajua kwake hupinduki. Two weeks amekaa kimya mpaka wewe ulivyomuanza en u endup apoligising aaah tafadhali jamani de guy is jst not into u!!! ushauri get out fast wanaume wapo kibao en worry not utampata mwanaume anayekupenda ambaye hata umekosa wewe anapologise yeye!!!
Anonymous said…
Katika Kiingereza kuna kitu kinaitwa "damage limitation" [PUNGUZA HASARA]. Achana naye, experience inaonyesha kuwa kuwang'ang'ania watu kama hao mwisho wake ni machozi na majuto. Yeye ndiye mwenye matatizo. Usijitwishe matatizo yake bure!!! Kama kweli unajiheshimu hata kidogo utaachane naye.
Anonymous said…
dalili za mvia ni mawingu mwanaume wivu dharau hana upendo full stop jiachie mama kama anakupenda atakuja kukuomba msamaha muanze upya mie mwanaume wa kibabe 24/7 ni hatari sana No way ufunge ndoa eti atabadilika utakoma shauri zako !!!
Anonymous said…
Pole sana dadangu, nafikiri unajua la kufanya ila sijui unaogopa kupoteza hiyo miaka yote uliyokuwa naye? Let me tell you something, siku zote mwanaume atakufanyia mambo depending on how much you let him. There's no respect and love hapo. Stop wasting your time, unakosa bahati zingine kwa kumng'ang'ania huyo. Is that the best you can get out of life kweli? Maana maisha ya siku hizi ni uamuzi wako. Ukitaka mwanaume wa kukuumiza kichwa utampata, ukijiwekea standards utampata pia anayekuheshimu na kukupenda. Most of the people end up in marriages full of complications kwasababu ya uoga na kujiwekea low expectations. Hata wanaume wana standards, don't expect to end up with a good man wakati wewe huna standards. Acha kujishusha dadangu, expect more and you'll get more.
Miaka 6 siyo ishu compared to a miserable marriage for the rest of your life. Na life yenyewe ni short. Is this the kind of man you want to be the father of your children? Hivi kweli watoto wakiona baba ana m treat mama yao in such a manner unategemea nini? Najua you know what is best for you, ila take it from me it's never too late move on! And sometimes people need to loose what they have to know it's worth. No woman can change a man, it's his choice and personality only he can change himself. Nakutakia kila la kheri kwenye maisha yako. Naomba ujithamini!
Anonymous said…
pole sana dada!hakuna kiti kizuri duani kwenye ulimwengu wa mapenzi kama kusema ASANTE,SAMAHANI,NAKUPENDA,POLE, ukisikia umpendae katamka haya basi hujiskia furaha.lakini kama haya hayafanyiki ni wazi ndoa au mahusiano yatakuwa machungu sana.ebu anagalia ni maisha gani ungependa kuishi wewe na mpenzi wako!je ni kero au amani na upendo?kama ni amani na upendo tafuta yule ambaye anaweza kukupatia hayo na siye wa kukukera na kukusababishia vidonda vya tumbo.hapo hujaingia kwenye ndoa nae!jiulize ukiingia kwenye ndoa itakuaje??dada kuwa na mahusiano mengine haimanishi wewe ni malaya.heri upate mtu ambaye atakupatia ile furaha ya mapenzi na kule kujiskia unapwendwa.
Paul Akwilini said…
DADA POLE NA MATATIZO. NIONAVYO MIMI NI KWAMBA HUYO MWENZAKO ANAE MWANAMKE MWINGINE AMBAE ANATAKA KUMUINGIZA KTK NAFASI YAKO. ANACHOTAKA YEYE ANAOGOPA KUKUELEZA KWAMBA MUACHANE,BADALA YAKE ANAKUCHOSHA TARATIBU ILI WEWE UMCHOKE NA HIZO TABIA ZAKE UMUACHE ILI IWE KISINGIZIO. KWA HIYO MCHUNGUZE KWA MAKINI UTAGUNDUA. HAIWEZEKANI MUINGIE CHUMBANI KISHA GAFLA ATOKE AKUACHE HUKO. INA MAANA ALIKUWA HANA SHIDA YA SEX NA WEWE.
Doctor wa mapenzi said…
Waswahili wanasema "msema pweke huwa mshindi" Siwezi kutoa uamuzi wa ushauri kwa kusikiliza upande mmoja wa maelezo! Kuna mengi huenda umeyaficha, na umeeleza upande mmoja tu. Na ili ni balance case, ngoja ni postulate yafuatayo;

1. Huenda wewe mdada, sababu unafanya kazi, na huyo boy friend wako bado anasoma, basi kwa hivyo vi sent vyako vya mshahara una mnyanyasa huyo b.friend wako. Wanaume ukionesha dharau wao hukuonesha mara 2 yake. Ndo maana na yeye anaishi kuwa mkorofi kwako.

2. Huenda wewe una urafiki wa karibu sana na hao " best friend wakiume" kiasi kwamba inavuka mipaka, na inamvunjia heshima b-friend wako. Eti wani hug? Ndo upuuzi gani huo! Mbele ya b.friend wako aje mwanaume mwengine aku hug? Ndo kuiga western culture au? Si mila zetu kivile...lazima kuwe na mipaka ya salamu. Kwa hilo lazima uwe tayari kujirekebisha, si utumwa kufuata matakwa ya boy friend wako, so long hayakuvunjii utu wako. Anayo haki ya kukupangia yupi uongee nae kama wewe ulivyo na haki hiyo kwake (msikilize K-lyn ft J Mo na kibao chake ni kipata wangu remix).

3. Huenda huna staha na hujiheshimu in the name of kwenda na wakati (westernized). Kwa hali hiyo usitegee kama utapata mwanaume wa maana akakuendekeza. Kila mwanaume anahitaji secure and respect. Ukileta kujuwa wao wanajuwa zaidi. Mwisho wa siku Utageuka mama huruma, coz utamaliza dozen ya wanaume.

Ushauri: Kama kweli umeshamaliza yako, na umeamuwa kuwa katika mahusiano ya kudumu mpaka ndoa na kifo tu ndio kiwatenganishe. Basi kumbuka Mapenzi ni kuscrify, lazima ujuwe kwamba ukiingia kwenye mapenzi basi unapoteza kiasi cha uhuru wako, vivo unamnyang'anya mwenzio kiasi cha uhuru wake. Pia kwenye mapenzi ujuwe kwamba utatakiwa kufanya mengine ambayo wewe hayakufurahishi kihivyo, lkn mwenzio yanampendeza, vivo utataka kufanyiwa wewe yasivyomfurahisha mwenzio lkn wewe yanakupa raha na furaha. Mathali unyonyapo mboo hupati lolote wala hakuna ladha kwako, but ni fuuraha ya mwenzio, ni hivyo hivyo unaponyonywa KUMA hakuna utamu wowote kwa akunyonyaye zaidi ya ladha mbaya ya maji ya kuma, lkn kwako wewe unyonywaye ni raha na ladha ya ajabu. Huo mfano mdogo tu. So uwe tayari kuacha akukatazayo mpenziwo, ilimradi hayakuvunjii utu wala kukuondolea uhai, vile vile na wewe mkataze kwa usiopenda. Na mwisho mapenzi si upatu kwamba mnachanga kisha mgawane, achana na mambo ya kulipa visasi in the name ya kufundisha! Ni ujinga kufanya hivyo. Jirekebisha, mueleze, mrekebishe! Kama mumeishi miaka yote hiyo, basi huyo anakufaa! Usikurupuke kufanya maamuzi mazito. Kila mahusiano yana challenge zake! Muhimu ni kukubali makosa wewe kwanza kisha mrekebishe mwenzako.

Mimi Dr wa mapenzi
Anonymous said…
Wanaume wa mtindo huo wanateka wanawake kwa sentensi hii, nataka kukuoa. Nilishawahi kuwa na type ya mtu huyo, habadiliki kwa viboko wala kwa kupewa uchi, hata umpe tigo ndo kwanzaaaaaaaaaaaa atakuoa we changu, kashfa ndio kwao hapo, dharau usiseme ilimradi wakufanye ujione haufai.Ushauri wangu kimbia tena kwa miguu miwili kabla haijakatika, mie niko huru sahivi. Ukiachana naye achana kuwasiliana naye kabisaaa mana atakujia anakupenda lalalalala ukilegeza kamba yanarudi yale yale. Atakufanyia vimbwanga weeeee halafu atakujia mie nataka kuoa mwanamke bikira na awe hivi vile, so achana naye hafai huyooooo.
Anonymous said…
Pole kwa yoye mdogo wangu.... huyo mwanaume ana hulka mbaya kwanza ni kabila gani kwani kuna baadhi ya makabila wanapenda kunyanyasa wanawake...kifupi achana naye mungu yu pamoja nawe na humjaalia kila mja wake mwenye kumuomba yaliyo mema... huyo jamaa atakunyanyasa sana ikiwa mko katika uchumba ni manyanyaso kiasi hiki je ukiingia katika ndoa itakuwaje?? jaribu kupata picha kamili, kaza roho achana naye utampata mwingine, mwenye upendo na mapenzi ya dhati
Anonymous said…
KAMA HUTASIKIA NA KUFUATA USHAURI HUU MDOGO ULIOKWISHA PEWA NA WACHANGIAJI HAPO JUU, UTAKUJA KULIA NA KUSAGA MENO. PLEASE BE YOURSELF OTHERWISE NANI KAKUAMBIA KILA MWANAMKE NI LAZIMA AOLEWE?
Anonymous said…
kitu cha msingi, mkiwa na mtu hamuelewani wakati wa uchumba, ni afadhali muachene kuliko kuvumilia mpaka muoane, ndoa ndo watu wanavumilia, si uboyfriend/uchumba, jamani watu wakifika ktk ndoa huwa wanakuwa wabaya zaidi ya hapo, kama alikuwa ana tabia fulan mbaya ndo itazidi kama hakuwa nayo ndo ataanza, kwahiyo ukitegemea atabadilika mbele my dear, utajutia maisha yako, huyo mwanaume ni mbabe mno na hajui kubembeleza, kitu ambacho ndo raha ya mapenzi, mtu akujali na kukubembeleza na kukuona una thamani, kwa ubabe huo mnaoonyeshana ,hiyo ndoa mtalia, na mwanamke utalia zaidi, maana wanaume wao kupata replacement/nyumba ndogo simple kwao, lakini mwanamke uwa ni issue kidogo.
de'victorious said…
YANINA HASIR AHADI BASI HIVI MIJANAUME IKOJE....yani nahasiraaaaaaaaaaa
Anonymous said…
HUYO ANAYEJIITA DK WA MAPENZI SI LOLOTE WALA SI CHOCHOTE, USHAURI WAKE NI SAWA NA NGUVU ZA GIZA TU, MAPENZI GANI HAYO YAKUUMIZWA KILA SIKU? AU WEWE NI BEST FRIEND WAKE NA HUYO JAMAA NINI..?

ASIKUDANGANYE MTU DADANGU MAPENZI NI KUSHARE FURAHA, UPENDO NA HESHIMA KWA PANDE ZOTE MBILI, SASA KAMA UPANDE MMOJA UNAKUWA NI KULETA TU MAUMIVU BADALA YA FARAJA NA FURAHA HAKUNA MAPENZI HAPO, ETI KUJITOA KAFARA, KAFARA GANI YA KIJINGA HIYO KULIBEBA JITU LUSILOKUWA NA UTU KIASI HICHO? ACHENI KUTULETEA MAPENZI YENU YA KIZAMANI HAPA YA KUKANDAMIZA WANAWAKE NAKUWAONA KAMA WATUMWA WASIO NA THAMANI ISIPOKUWA NI VYOMBO TU VYA STAREHE..
Anonymous said…
Pole madame wit issues.Lakini sijapenda the way the guy mistreats you ,doesnt know your worth na bado unaendelea kumbembeleza.I know maybe you are so much in love with him but that should not be the reason for you to stay with him and be intimidated,Please wake up and smell the coffee this man is not into you and he is tired of you and that is why he is sending signals but you dont seem t realise.Always remember you are beautiful,believe me am sure if you leave that man you will find someone else who will treat you right and even be better that that hooligan anaekudhalilisha ovyo.i have been thru a lot and i learnt my lesson,DO NOT ENTERTAIN SUCH MEN,infact leave him as fast as you can before he kills you ooo.
Anonymous said…
Dada wenzangu washakwamia na wewe mwenyewe ushaona kuwa unanyanyaswa mpk una vidonda kwa sababu yake? akikuoa si ndo utakufa kabisa kwanza ACHANA NAYE haraka iwezekanavyo, yeye anakutumia tu na kukunyanya mpk anadiriki kukwambia kati yako na yeye mwanamumue nani inamaana kuwa mwanamume ndo unapata kibali cha kunyanyasika? naomba ulijue hili kuwa kila mtu ana mtu wake ambaye amepangiwa na MUngu na huyo sio wako aliyekupangia MUngu asingekunyanyasa hvo, unajicheleweshea bhati achana naye msubiri wa kutoka kwa MUngu.
Anonymous said…
Pole

my dear mimi nina mchumba mwenye tabia kama hiyo ya kunigeuzia kibao anapokosea yeye, ila in my case najua jinsi ya kum-handle.

that guy is only using ur body yaani anakuona kama chombo sio kama mwanamke anaepaswa kupendwa, kuheshimiwa.

haw wanaume wanatabia ya kupenda kutufanya kama mapunda but girl wake up yaani ingekuwa wewe ndo mimi yaani mbona angenikoma hivo vituko ambavo ningemfanyia ni mara kumi ya anavovifanya. ucruhusu mwanaume yeyote akakufanya punching bag!!!

Tena mwambie achape lapa mbaya tena fasta iwezekanavyo...mume utaletewa na mungu...lakini huyo mwambie atafue mwingine wa kumfanya msukule wake. kama alikusuma hvo atakuja kukuua cku moja kweli tena. hafai achana nae hangaika na kutafuta pesa. Yaani natamani nimuone huyo msenge nimpe vipande vyangu, u r the leader of ur lyf huyo ni kuma tu kwani amekuoa????????????? aaaggghhh

na ukiachana nae ucjeukajiroga ukarudiana nae shoga this time akirudi atatambaa mbona ili tu umsamehe ukibugi tu stepu umekwisha mwache asote kwani hapo alipo hajui anakitu gani na chenye thamani gani!! maama nauomba ucendelee kumuendekeza u deserve a man hu is sweet, loving, husband material, one hu will never ever lay a hand on u and one hu will love u unconditionally na ambaye hana wivu wa kipumbavu kama huyo mbwa.
Anonymous said…
zat not LOVE, zis is all i cn say
Unknown said…
we mdada unajua maana ya love? kwangu love ni kumfanya nimpendae happy mda wote,thats my definition.
Sasa huyu bwana hata hataki we ufurahi?=hakupendi,very simpo adage. Aisee hata mie nilipokua nimelose interest na mdada mmja in the past nilikuwa hivyo hivyo aisee duu alikuwa anaumia,anyway am sorry for that lakini kuikweli kama mie siwezi acha sweet wangu apate tabu hata kdg,haa haiwezekani kbs coz ha happiness is dwelling in me. Love means kumjali mtu awe na good mind set-up,mtu ambaye ukiwa na shida ndo anakutuliza na kukupa faraja,sasa huyu mshkaji dawa yake we amua kuwa nae mbali tu ukiona kawa kimya pia ndo ujue hana mpango na wewe. Usije shangaa eti miaka 6 sijui ndo mda mrefu so... hakuna kitu mie nimeachana na huyoo nimekupa story hapo juu after 8good years in serious relationship,ingekuwa shule ningekuwa na ka-pHD,hakuna kitu kuizuri kama kuwa na mtu wa kukupa faraja.
Afu CV ya wanaume kitu gani bwana? ah acha ushamba wewe. Ukicheki some(if not many)succesiful marriages come thru such CVs,unakuwa na hata kacertificate ka mapenzi,sa wewe una la7 in love(simaanishi watu wawe na GIGO relationships) na unatka kuendelea unadhani ndo mwisho wakat unaumia,pole mama anyway kila la kheri bibie ndo shule ya mapenzi,utagraduate tu.
Regards.Jer
Anonymous said…
Hello, huyo jamaa anataka kufanana na mimi kimsimamo ila sio sana maana mimi kumburuta mwanamke kiasi hicho siwezi, nina huruma sana. Lakini kwa swala la wivu kama kuhug na other boys I can't tolerate, yaani huwa naumia na kupata hasira sana hasa ikiwa nilishakwambia kwamba sipendi. Pia nadhani ni inategemea na lifestyle la mtu alikuwaje toka mwanzo maana kuna watu wengine wamekaa kiuanaume zaidi na hawezi kulegeza sana sometimes inabidi kuwa nae umvumilie unless uachana nae.
Mimi ushauri wangu ni kwamba japokuwa almost wote wamekushauri uachane nae moja kwa moja lakini mi naamini wewe ndo unaemjua zaidi, jaribu kukaa nae chini kwanza mweleze yote uliyonayo usimfiche hata moja kisha mtangazie kwamba utaachana nae kama hatafuata yale unayoyategemea na akishindwa kufanya hivyo basi we unaweza kuachana nae sasa.
Nimekushauri hivi kwa kuzingatia kwamba huyu mwanaume ana wivu na wewe kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa sana kwamba anakupenda pia umesema hana tabia mbaya ya kutoka na wanawake wengine ni vigumu sana kumpata mwanaume kama huyo pia mwanaume anaweza kupenda sana bila kukuonyesha wazi.
Binafsi huwa ninaweza kufanya karibu na hayo anayoyafanya huyo lakini mwanamke ninampenda sana ila pia unajaribu kumwangalia je naye kweli yupo?
Kingine ni kwamba most of the boys huwa hawapendi dharau au kukosewa heshima na sometimes anatumia ubabe kama silaha ya kujilinda we just differ in terms of perceave things.
Just give him last chance, usikurupuke na ushauri unaopewa na wadau wachangiaji karibu wote wa mada hii wakati mwanaume ni wako na unayemjua ni wewe mwenyewe wala si wachangiaji na umeweza kusurvive naye kwa muda mrefu.
Anonymous said…
Hello, huyo jamaa anataka kufanana na mimi kimsimamo ila sio sana maana mimi kumburuta mwanamke kiasi hicho siwezi, nina huruma sana. Lakini kwa swala la wivu kama kuhug na other boys I can't tolerate, yaani huwa naumia na kupata hasira sana hasa ikiwa nilishakwambia kwamba sipendi. Pia nadhani ni inategemea na lifestyle la mtu alikuwaje toka mwanzo maana kuna watu wengine wamekaa kiuanaume zaidi na hawezi kulegeza sana sometimes inabidi kuwa nae umvumilie unless uachana nae.
Mimi ushauri wangu ni kwamba japokuwa almost wote wamekushauri uachane nae moja kwa moja lakini mi naamini wewe ndo unaemjua zaidi, jaribu kukaa nae chini kwanza mweleze yote uliyonayo usimfiche hata moja kisha mtangazie kwamba utaachana nae kama hatafuata yale unayoyategemea na akishindwa kufanya hivyo basi we unaweza kuachana nae sasa.
Nimekushauri hivi kwa kuzingatia kwamba huyu mwanaume ana wivu na wewe kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa sana kwamba anakupenda pia umesema hana tabia mbaya ya kutoka na wanawake wengine ni vigumu sana kumpata mwanaume kama huyo pia mwanaume anaweza kupenda sana bila kukuonyesha wazi.
Binafsi huwa ninaweza kufanya karibu na hayo anayoyafanya huyo lakini mwanamke ninampenda sana ila pia unajaribu kumwangalia je naye kweli yupo?
Kingine ni kwamba most of the boys huwa hawapendi dharau au kukosewa heshima na sometimes anatumia ubabe kama silaha ya kujilinda we just differ in terms of perceave things.
Just give him last chance, usikurupuke na ushauri unaopewa na wadau wachangiaji karibu wote wa mada hii wakati mwanaume ni wako na unayemjua ni wewe mwenyewe wala si wachangiaji na umeweza kusurvive naye kwa muda mrefu.
Anonymous said…
weweeempige chini huyo ii aelewe umuhimu wako.....unajinyima furaha ya nini?let go of.........