Mikono mikubwa kuliko mwili....nitapendeza gauni la Harusi?







"Pole kwa kwa ngumu dada Dinah.
Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 24 tatizo nililonalo ni kwamba, mikono yangu ni minene kuliko mwili.

Nina umbo zuri, sura nzuri lakini mikono imezidi. Nahofia siku ya harusi yangu sintapendeza, kwa kawaida huwa sivai nguo za mikono mifupi au midogo. Nimekaribia kufunga ndoa na wasi wais wangu ni mikono, je kuna namna yeyote ya kuipunguza au hata kama kuna dawa yoyote unayoijua ya kupaka naomba unisaidie au kama kuna mazoezi yoyote ya kupunguza mikono. Mpenzi wangu huwa ananiambia huna mikono minene basi mimi sipendi, wakati najua ni minene"



Dinah anasema: Hey mtarajiwa, hongera sana na kila la kheri ktk maandalizi ya kufunga ndoa. Hakika suala la kutafuta na kupata gauni litakalokupendeza kutokana na umbile lako sio kazi rahisi, hata hivyo shukrani kwa wabunifu wa mitindo yanguo za kufungia ndoa kwani wanabuni kutokana na maumbile ya watu.



Ukubwa wa mikono itakuwa ni sehemu ya umbile lako na hivyo sio rahisi kuifanya iwe midogo au miembamba, pamoja nakusema hivyo kuna aina ya mazoezi ya kuifanya mikono yako kuwa "firm" na hivyo kuonekana minene lakini haijajitokeza kwa nyuma au kwa chini (kama mbawa), tafadhali kama utakuwa tayari mimi kukuelekeza namna ya kuzoezika basi usisite kuniandikia.



Vinginevyo mimi nakushauri uchague Gauni ambalo litaficha mikono yako (angalia picha hapo juu), usifuate trend kwamba kila mtu anavaa gauni bila mikono basi na wewe utake hivyo (mara nyingi huwa too common) na badala yake nenda kwa a classic one lakini inayoendana na umbile lako.


Kila la kheri na furahia siku yako ya ndoa.

Comments

Anonymous said…
HEeeeeeeeeeee wewe mdada hayo ni maumbile yako tu na hakuna njia ya aina yoyote ya kupunguza unene huo.

Jambo ambalo lazima ulijue ni kwamba kama mwili wako wote umekaa vizuri na unaridhika nao kasoro mikono basi ujue ndivyo ulivyoumbwa na lazima kuna mtu amekurithisha kwenye ukoo wenu.Huo si ugonjwa na wala usijitese na harusi.Unaweza kujiumiza na kujiharibu bure kwa kufikiri kama vile una kasoro eti kisa harusi.tena una bahati mpenzio anakuona uko fit sasa unahangika na harusi ya masaa machache tena kwa ajili ya kuvaa shera?

Achana kabisa na mawazo potofu hayo.Hakuna mtu akanenepa mikono tu na sehemu za mwili zingine ziwe kawaida.Inaelekea wewe unajihisi tu.Mbona mchumbao haoni hivyo iweje wewe ujihisi hivyo na nuanze kuhangaika hivyo?Tulia anza maandalizi yako ya harusi.