Can't marry me lakini anataka mtoto nami-Ushauri!

"Hakika wewe ni mwanamke jasiri..
Mimi ni msichina wa umri wa miaka 28 nimekuwa ktk uhusiano wa kimapenzi huu mwaka wa tano sasa, lakini sielewi nini cha kufanya mpaka sasa. Mpenzi wangu ni mchanganyiko wa rangi kati ya mweusi na mwarabu kwa baba.


Tunapendana tena sana tu, wazazi wake wanamwambia kuwa muda wa kuoa umefika atafute msichana aoe lakini si msichana aliyekuwa nae, thats means mimi, Alipopata habari hizo aliniambia japo roho yangu iliniuma sana lakini sikuwa na la kufanya zaidi ya kumwachia yeye aamue..


Ndipo baada ya mwezi mmoja aliponiomba kuwa anataka kuwa na mtoto na mimi, nilifurahi kwani napenda niwe na mtoto naye pengine hata awe mume wangu, akadai kuwa tutakapokuwa na mtoto itakuwa rahisi yeye kuwa karibu na mimi siku zote na pengine kuwa wote kabisa na hata kama ataoa ni kwa kuwaridhisha wazazi wake tu kwani yeye chaguo lake hasa ni mimi. Nikamuambia naomba muda nifikirie kwanza ili kama kufanya maamuzi yawe sahihi

Dinah sasa hapo ndio sijui nini cha kufanya:

Nafikiri niachane naye tu lakini nampenda na roho inauma sana hata ukizingatia tumevumiliana kwa mengi na pia huwa sipendi kubadili mahusiano hadi hapo inapobidi. Nahofia pindi atakapo oa, je ni kweli ataweza kuwa karibu na mimi?

Hasa atakapokuwa na huyo mkewe? Au ndio nitaishia kupata tabu na mwanangu tu? Maana si unajua mtu akishakuwa na mke tena hasa hawa wenzetu waarabu bila shaka huyo mkewe atakuwa mwarabu pia. Naomba ushauri wako ambao utanitoa hapa kigazini nilipo."

Dinah anasema: Pole kwa unayokabiliana nayo. Haya hutokea sana kwenye jamii nyingi tu za Kiafrika na sio Waarabu peke yao. Kabla sijaendelea naomba nikuulize swali.....hao wazazi wake wanajua kuwa wewe ni mpenzi wake?

Unayokumbana husababisha wanaume wengi kuamua kuoa mara mbili, ndoa ya kwanza kulidhisha wazazi na ya pili ni kwa mapenzi yake na hufanya siri bila wazazi wao kujua. Hapo hutafuta visa kama vile kunyima tendo la ndoa, kutorudi nyumbani mapema, kutokua chakula kipikwacho nyumbani, kutoongea nao, kutotembea nao n.k.

Hali inayopelekea mke huyo aliyechaguliwa kuomba Talaka, na hili likitokea Bwana anakuwa huru kutangaza ndoa nyingine ambayo tayari alikuwa ameshafunga sambamba na ile ya mke wa "kutafutiwa" na wazazi.

Huyu bwana inaelekea hata yeye amechanganyikiwa kama wewe ulivyochanganyikiwa na kweli anakupenda ndio maana anatumia njia ya kuzaa na wewe ili usijekuwa na mtu mwingine na akakukosa. Lakini, pamoja na nia yake njema bado utakuwa umezaa nae nje ya ndoa pia utakuwa ni Kimada na sio Mke pamoja na kuwa wewe ndio ulikuwa wa kwanza kuwa nae ktk uhusiano wa imapenzi.

Wewe hukupaswa kumuachia mzigo wote yeye peke yake ili afanya uamuzi (kosa kubwa ulifanya hapa), Wote wawili mlipaswa kulijadili suala hilo zito na kufanya maamuzi ya busara hasa ukizingatia mmekuwa kwenye uhusiano kwa muda mrefu.


Kitendo ulichokifanya kimemrahisishia yeye kufanya uamuzi logically zaidi na si kihisia na ndio maana akaja na suala la kukumimba ili aendelee kuwakaribu na wewe bila kuangalia hiyo itakuathiri vipi wewe Kihisia, Kimwili na Kisaikolojia.


Natambua ulipomuachia jukumu hilo ulitegemea yeye kukuambia kuwa hajali wazazi wake wanataka nini, atakachofanya ni kufunga ndoa na wewe, hata ikiwezekana kuhama mahali hapo na kupotea kabisa lakini awe na wewe............mwanaume mwenye mapenzi ya dhati na mwenye kujali hisia za mpenzi wake hakika angefanya hivyo na sio kuja na suala la kuzaa na wewe lakini kuoa anaoa mtu mwingine.


Nakubaliana na ufikiriavyo, kwamba ni heri muachane tu. Ikiwa hili ndio utakalo basi fanya haraka iwezekanavyo kabla hujapoteza muda zaidi. Natambua inauma sana......maumivu hayo ni ya kawaida kwa yeyote anaeachana na mpenzi wake ampendae, iwe kwa kugombana au kwa kuelewana bado maumivu ni yale yale lakini kutokana na tofauti zenu kubwa inabidi iwe hivyo.

Kuzaa nae ni sawa sawa na kuzuia baraka na bahati kutoka kwa wanaume wengine wazuri out there, sio wanaume wote watakuwa tayari kulea mtoto wa mwanaume mwingine na si dhani kama huyo bwana ataendelea kuwa karibu nawe the way anaahidi sasa. Kama kweli anataka kuzaa na wewe basi mfunge ndoa as simple as that!

Ukimuacha kabla yeye hajafanya hivyo itakuwa vema kwani utamuonyesha kuwa wewe ni mwanamke mwenye msimamo, unajiamini na unajua unataka nini maishani mwako. Unataka kuendesha maisha yenye amani na furaha, unataka kuthaminiwa, kushehimiwa, kupendwa na siku moja kuolewa na kuwa mama, sio kuwa mama na wakati huo huo Kimada.

Miaka 28 bado unamuda mzuri tu wa kukutana mwanaume mwenye kujali hisia zako, atakaepigana kwa ajili yako bila kujali ni nani hasa anataka kujiingiza kwenye maisha yenu ya kimapenzi.

Mungu akujaalie ktk maisha yako na siku moja utafunga ndoa na mwanaume mwenye kufuata Moyo na kufanya uamuzi yeye kama mwanaume kamili na sio kuamuliwa na Wazazi wake.......
Kila la kheri!

Comments

Anonymous said…
dada kwanza pole kwa yote yaliyokupata, mimi nachoweza sema ni kwamba huyo jamaa yako hana msimamo kabisa, kama angekuwa na msimamo angekutetea kwa familia yake kwa moyo wake wote. pili familia hiyo ni ya wabaguzi,hata ukijidanganya uzae nae hutapendwa ng'o kisa rangi yako na huyo mwanao, hutathaminiwa wewe kwa lolote, tatu si vizur kuiba mume wa mtu hata vitabu vitakatifu zinasema, usione watu wanaishi uke wenza lkn hawafurahii kabisa.mwisho achana na huyo mwanamme yasije kupata makubwa waweza rogwa wewe kisa unang'ang'ania mume wa mtu.sasa faida iko wapi uwe chizi bure mtoto wa kike kubali tu wako yupo Mungu kakupangia.
Anonymous said…
kama anaoa mwingine haina haja ya kuzaa nae ili iweje?
jaribu kusahau chukua mda wako mwingi kufanya mambo mengine yatakayo kuweka bize na kumsahau, ni kitendo cha uamuzi tu wala si kigumu.pia omba Mungu akupe alie wako na usiwe king'ang'anizi.
Anonymous said…
Ikiwa wewe unamwamini Mungu, na una malengo na maisha ya baadaye basi fuata dini yako inasema nini. Kama dini yako unayotumia kumwabudu Mola wako inasema kuzaa nje ya ndoa au kabla ya ndoa ni ruksa basi zaa tu, na kama hairuhusu basi jibu unalo kwamba ndoa ndio chanzo cha mapenzi ya kweli.
Nimekubainishia ipi ni pumba na upi ni mchele ni juu yako kufuata!!
Kumbuka umri wako ni mkubwa sasa, usitake kupoteza bahati ya kupata mahabuba wako ambaye Mungu amekuandali kwa kuzaa.
Mara nyingi sisi wanaume hatupendi kuoa mwanamke aliyezaa. Tazama ninavyo kubainishia ukweli, Sasa wewe hata ukizaa huyo mwarabu wake akipata mtu anayempenda kuliko wewe si ndo atakuacha uking'aza sharubu na mtoto wako? Nakwambia hatathubutu kutia hata pua yake kwako. Mi nakushauri utulie na acha umalaya wa kutiwa tiwa kabla ya ndoa! Wee unafikiri nani hapendi kutomba au kutombwa!? Wote tunapenda ila tunavumilia tu, usitake kujifanya wewe ndo mama huruma sana kumbe unamaindi tu mboo. Tunza thamani ya mwili wako ili upate mchumba mwenye kukuthamini na hatimaye kufunga ndoa nawe haraka sana.
Enyi mabinti acheni tabia za kuiga maisha ya tamthilia na maigizo yaonyeshwayo kwenye Tv , na wakati ukija kwenye real situation hali ya maisha haipo hivyo. Wengi walijifanya wanajua kupenda lakini mwisho wao ulikuwa ni vilio vya kusaga meno. Please think analytically and conceptually. Usiufanye mwili wako kuwa jalala la kumwagia shahawa za mtu ambaye hafikiri na hana mpango wa kuishi na wewe.
Kwanza alie kudanganya kuwa upendo unaunganishwa kwa kuzaa mtoto nani?
Watu wa namna hyo watakuja kuwamwagia virus halafu muanze kutoa hadithi za 'SITASAHAU MPENZI WANGU WA KIARABU ALIPONIAMBUKIZA UKIMWI NA KUNITELEKEZA NA MTOTO' kwenye magazeti ya udaku.
Mwatima
Anonymous said…
Kumbe dada yangu una bahati sana kwamba huyo mpenzi wako kakuakmbia ukweli kabisa kwamba wazazi hawakuhitaji wewe uolewe naye. Sasa unafikiri utakuwa ndugu wa nani hata kama huyo jamaa atakuzalisha au utaoana naye wakati anashinikizo kali sana kutoka kwa wazazi wake?

Pamoja na kumpenda sana pamoja na kuwa naye katika mapenzi muda mrefu sana, siku ya siku imefika sasa kukupa facts kwamba huyo hatakufaa na umeishaambiwa na mhusika mwenyewe kuwa wazazi wamempa chaguo. Kumbuka kama huyo jamaa anakuja kukugereshaeresha ni ili usije kunywa sumu maana jamaa anajua jinzi mlivyohusiana na kutombana hasa, na pengine kufanya na mengine ya kifidhuri si unajua watu wakiwa katika mapenzi yakinoga hupitiliza hata utumiaji wa kawaida wa viungo husika.

Kuzaa mtoto naye usithubutu hata kidogo.Ukizaa unategemea nini dada?hujui kwamba utakuwaq umejiwekea doa zaidi la kukuchafua na kutotamanika na wanaume wengine?Mimi nilifikiri huo ni wasaa wako muafaka kuona mwanga na kuondoka katika eneo hilo tafuta la kwako maana mwenzio kishatafutiwa tayari.Usipotezxe muda kwa kusema eti unampenda na mumuvumiliana katika mengi!!! haya yalikuwa mapenzi tu dada, kitu ndoa bado hakina nafasi katia hilo hata kidogo. Usifikirie uhusiano wa kimapenzi unalingana na kitu kinaitwa ndoa.Huyo jamaa yako sasa hivi anazengea ulaji wa ngono tu kwako.lakini ni mstaarabu sana maana amekuambia ukweli wa hali halisi, machale yako kwako kama huoni kitu pole dada.Kama ni ngono mpeni maana umezoea lakini kataa kuzaa mtoto na akishaoa achana naye kabisa nawe endelea kusaka wa kwako.

Nakutakia kila la heri dada ujue kuwa mwarabu huyo kishakuponyoka hata ufanyeje usijeachawa kwenye mataa zinduka sasa kama ni utamu mumeishapeana na kkukiaiana.Yaani wewe hakuna wanaume wanakupenda kweli?hujui kwamba uhusiano ulio nao umefanya watu wasikusogelee kwa sababu wanajua una mtu.Lakini wakijua umeachana naye watamiminika haraka sana kukujulia hali.
Anonymous said…
Dear pole sana kwa hayo matatizo yaliyokukuta. Mimi pia ni Mwanamke wa kiarabu ngoja kwanza nikuubie siri yetu sisi waarabu,Hata sisi wanawake wa kiarabu wengi tulioachika hujiiba na kutembea na wanaume wetu means wa kiarabu na kujaribu kuwaboresha kwa vile tuna experiance za mapenzi. Hufanya hivyo kwa vile tumeachika na labda tuna watoto ili angalau tuolewe tena tustirike. Basi watatuchezea kufurahi ngono zetu na wakifikia kuoa wanaenda kutafuta wasichana bikra! Waarabu hadi leo bado wana mambo ya kufatilia bikra ndio wanaamini kuwa mwanamke bado muaminifu na hufurahia sana wengi wao nchi za kiarabu akikutwa hana bikra basi huachika mara moja lakini wazee wa mwanamke huwa hawasemi ukweli kuwa kaachika kukutwa wazi! Mara nyingi wanaume hao husema eti kwetu kwa vile ni ibadhi (dheheb mojawapo la kiislam) ni lazima nioe mwanamke ambaye sijatembea nae au nimelazimishwa nioe kazani wangu hizo ndio mbinu zao. Na dini inavyosema msiowe mliozini nao mtakaua daima kama tu mnazini hata mkioa mtakua mnajidanganya ndoa yenu Mungu haikubali kabisa!Na toba yao ya kuzini hukubalika ndio maana wanaacha na kuoa.

Sasa ukija kwa waliokua nchi zingine ndio kama hivyo ulivyoambiwa wewe mara nyingi huwa wenyewe hawapendi kuchanganya damu au kuamua kuifata dini na kutubu makosa yao na kweli wazee pia na ukiwa siyo muislam ndio kasheshe! Sasa ndugu yangu mimi nimezaliwa Tz na sasa naishi Uarabuni lakini najua mbinu zote za waarabu wenzangu na dini pia lakini mimi binafsti nimechanganya familia yangu nusu waarabu, nusu waafrica kwa hiyo kwangu ni sawa na hata ndugu zangu wa TZ nawaacha na uhuru wao na wote wameoa waafrika na mimi nipo nao wote poa tu muhimu wamechagua wasichana waliojitunza hivyo kuna uaminifu na usalama.

Kwa hiyo ndugu yangu wala usijaribu kuzaa nae huyo muarabu japo ni halfast mtoto wako atabaguliwa hadi atajichukia akikua.kwanza kabisa ataitwa mwana wa haramu!! Sisi tuliolewa nao na tulipoachana hata hawatujui tena na pia watoto wao wenyewe wanawabagua kwa ajili ya wake zao.

Nina mtoto wa kazani wangu mama yake ni mwafrika lakini baba yake ni Muarabu na alizaliwa nje ya ndoa mtoto alipenda familya ya baba yake na wao walimpenda na kumpa Education lakini baba alimbagua sana hakumthamini kama watoto wa muarabu mwenzie au wa ndoa basi mtoto alikua ana tabu hadi Mungu kamjalia kaaolewa. Kwa vile mafundisho alivyoyapata kwa mama yake mtoto alijitunza hadi ameolewa akakubwa bikra na sasa anafurahia maisha.

Mwingine mwanamke alizaa na murabu basi ni baba tu ndio anamthamini mtoto na mtoto katoka mweupe mzuri lakini hathaminiwi kabisa kwa family ya baba yake vile mtoto wa nje. Hata kama ni muarabu mwenzie lakini akiwa ni wa nje still anakua hana thaman! isitoshe mtoto wa nje kwa kiislam hana urith kwa baba kabisa labda baba ampe mwenyewe kabla hajafa!

Mimi naona hata kama unapenda waarabu wapo wengi waliochanganya na utampata atakaekupenda na asiykua na ubaguzi kwani dini yetu ya kiislam pia inakataza sana ubaguzi wa rangi muhim mtu awe na dini yake ndio aliembora zaidi kwa Mungu.

Jitunze utapata tu mume wa maana.
Huyo mwanamme hakupendi alitka tu kukuchezea na bado anataka kuendelea kukuchezea wakati yeye tayari atakua na maisha yake akupozee wewe,usijidanganye na pia dini yake kama anaifata kisawa sawa haimruhusu kuoa mtu aliezini nae!Hata kama umezini lakini ukiamua kuolewa olewa na mtu ambae hujazini nae kama wewe ni muislam na wakati huo umejitunza ndio nae atakuheshim.

Funga moyo na funga kuma kama ulivyoambiwa hako kamchezo katamu hakuna asiyekapenda lakini inabidi uvumilie umpe anaestahili na pia utaepuka na wonders za mimba na maradhi mabaya!Tulie na jitunze wapo wengi wanatafuta mwanamke alijitunza utapata wa mapenzi ya dhati atakae kuwa mume na baba mzuri hopeful. Na ukizidiwa madam umechakaonja hako kamchezo jichue tu utaona raha hadi upate wa ngono ya halali na mumeo.

Goodlucky.
Anonymous said…
Kwangu mimi nashindwa kuelewa unaposema anataka mtoto lakini hakuna ndoa. Kwangu mimi naona mumejifikiria wenyewe zaidi, na hili mimi naona ni kosa kwa wapendwa wengi. Tujaribu kufikiria kama wewe ungezaliwa na kuishi na mzazi mmoja, hii ikiwa pamoja na haki ungejifikiriaje? Tunaona sasa hivi ni jambo la kawaida lakini linaathiri sana katika fikira za mtoto.
Sijui mpo katika imani gani, kwasababu imani nyingine mtoto nje ya ndoa hana haki ya kurithi, na sehemu nyingine anadharauliwa ndio maana yakatokea majina mabaya ya kuwaita watoto kama hawo ambao sio kosa lao, ni kosa la watu kujifikiria wenyewe, watu kuthamini matamanio yao bila kujali matokeo yake.
Nakuomba ufikirie kwanza kabla ya kujingiza kwenye huo mtego, mwambie kama wataka mtoto subiri tuoane kwanza ili huyo mtoto akipatikana awe na haki sawa na hawo wengine watakaopatikana kwa huyo mke atakayemuoa!
Pili ushauri wangu mwingine ni wewe kukaa na kutafakari nini lengo lako la baadaye, ndio unampenda je upo tayari kuishi mitala, kwasababu mitala ina masharti yake, na wewe hapo ndio umepewa nafasi ya kuamua, ukiamua usije ukaanza kulalama, unatakiwa uwe mke mwenza na mwenzako umtambue, nafikiri unalijua hilo!
Ngoja niwaachie wengine, najua hapa wanawake litakuwa limewagusa sana, changieni kwa wingi ili tusikie maoni yenu, wakati tunamsubiri dada Dinah arudi, manake naye kwa `kutoka toka...'
emu-three
Love said…
Kwanza nakupa pole sana dada kwa yote, mimi naunga mkono maoni ya mdau No. 1,
Nakushauri mdogo wangu achana na huyo mwarabu anakupotezea muda ndugu yangu, mwombe Mungu atakupa mme utazaa naye na kupata mtoto na kujenga familia yako. kaa mbali na huyo tapeli my dear. mwisho wewe ndio mwenye uamuzi wako mwenyewe. mwisho Zidi kumwomba Mungu.
Anonymous said…
dada mwanaume huyo achana naye kabisa kwasababu hana mapenzi ya kweli na kama ana mapenzi ya kweli asingekubaliana na wazazi wake kwamba aoe mtu wa aina ya kwao na badala yake asingekubaliana nao angewaambia kuwa ana mpenzi wake ambaye anampango wa kumuoa lakini nia yake ilikuwa ni kukuchezea tuu then akuache kama angekuwa na mpango nawe asingekubaliana na wazazi wake.

Na kuhusu kumzalia mtoto usije ukalogwa ukakubaliana naye kwasababu wanaume ni watu wa ajabu sana atakupenda pale unapokuwa hauja zaa nae lakini unapojaribu kumzalia tu ndiyo umepoteza ramani ya maisha kwasababu hato kujali tena na kama ndiyo hivyo yuko beneti na wazazi wake kwamba aoe mke wa kutoka kwao wewe unafikiri atakujali tena ataacha kmjali mtoto wa kiarabu aje akujali wewe ngozi nyeusi?

Hayo ni mapito tuu tulia na muombe Mungu atakupa wako ambaye hamtababaishana kwamwe mtaishi maisha mazuri mpaka utajutia kuchezewa na muarabu.

Asante Regina napatikana Arusha.
Kim from A town said…
Dinnah mambo?
Hivi hawa watu wanaojibu kihuni hivi wana matatizo gani? Mbona watu wanaishi kinadharia sana? Mimi nashauri watu wanapochangia hapa wajaribu kuangalia the practical part of it. Kwa mfano watu wanazungumzia kufanya ngono kabla ya ndoa hivi mseme ukweli kutoka katika roho zenu na kwa kumuogopa mungu wangapi hasa wanaume wamefunga ndoa wakiwa hawajawahi kabisa kufanya ngono? Au inakuwa rahisi kunyoosha kidole kwa wanawake kwa kuwa kutokana na maumbile tunajulikana kama tumefanya ngono? By the way tunafanya ngono na nani kama si hao wanaume. Huyo mwarabu ambaye amezini na huyu dada mliyemshambulia hivyo si ataenda kuoa ambaye ni bikira yeye bikira yake tunaipimaje.
Mie nasema hivi ifike wakati sasa tutoe ushauri ambao ni practical. Wengi tunafanya ngono hata kabla hatujapata wachumba hasa wanaume. Pia wanaume wengi na hata wanawake wanafanya ngono na wanaume ambao si wake au waume zao. Hiyo ina tofauti gani na huyu dada au kinadada wengine ambao wanafanya ngono kabla ya ndoa?
Mimi nakushauri kuwa kama una uhakika wa kumtunza mtoto bila kutetereka iwapo baba yake atakata mguu baada ya kuoa dada pata mimba yako zaa mwanao endelea na maisha. It's really good kuzaa na mtu unayempenda kuliko kuzaa na mwanaume yeyote kwa madai kuwa ndio mumeo. Kwani hao waume za watu wangapi wana uhakika kuwa watoto waliozaliwa na wake zao ndani ya ndoa ni wa kwao? Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia kubwa ya watoto waliozaliwa katika ndoa baba wanaoaminika kuwa ni wao si baba zao isipokuwa hawajui kwa kuwa wake zao wamezaa watoto hao wakiwa pamoja.
Lakini pili hawa wanaume wetu wa sasa wanakera sana kuanzia kitandani mpaka kila mahali hata hao watoto wanaowaita wa ndoa hawawatunzi. Hivyo kama mwarabu anakufanya vizuri dada endelea naye hakuna aliyebook mwanaume wa kuwa naye (yaani hakuna mwanamke aliyebook mwanaume kutoka kwa mama yake. Wanaume wote tumewakuta wakiwa na meno yao 32 kwa hiyo hamna mwenye wake). Niite malaya , muasherati, mhuni na vyovyote unavyotaka lakini nadhani tusiishi kinadharia. N a mtu anapoleta swala lake katika mtandao anahitaji kusaidiwa na si kukatishwa tamaa kwa maneno makali. Naamini katika kuishi kwa vitendo na si kwa kumfurahisha mtu au jamii wakati mimi ninaumia. Kitu ambacho nitakutaka uwe makini ni kutojiwekea mawazo kwamba siku moja utaolewa naye mtu ambaye tayari amelazimishwa kuoa mwanamke mwingine. Wewe ndiye pekee unayejua kuwa mwanaume huyo anakupenda au la ingawa ni ngumu kuusemea moyo wa mtu mwingine.
Anonymous said…
my dear the same things happen to me.mimi nimependana na halfcast nimeona dalili zote ndoa itakuwa ngumu mama yake ndo kikwazo hanitaki kwasababu ni mweusi. jamaa ananibembeleza tuzae nimemkatalia live kwasababu nataka nizae mtu moja ambaye atakuwa tayari kuja kwetu kunioa. ctaki mwanangu aitwe mwana wa haramu.always ndoa hupangwa na mola dont push kama aliweza kukuletea huyo katika maisha yako kwa nini ashindwe kukuletea bora zaidi ya huyo.ni maamuzi magumu najua huo ndo ukweli shukuru amekwambia ukweli carry on na maisha yako utaolewa tu dada yangu wako aliyekuandalia mola yupo njian don give up let him go be strong.mimi ndo hatua niliyoichukua na nimepata mtu mwingine tena bora zaidi hadi najiuliza nilikuwa nangangania nini? hakuna watu wabaguzi kama waarabu dada ucjitie jereha la maishan.unastahiki upate mtu mwengine anayejua thamani yako atakupenda na kukulinda hadi mwisho wa maisha yako.be strong
kijogoo said…
Ushauri wangu usitafute msiba wa pili. Unachotakiwa kufanya ni kuomba maghfira kwa mola wako na kuomba toba kwa kufanya zinna.na baadae umuombe YEYE akuonyeshe mwenye kheri na wewe na inshaALLAH utapata mwenye kheri na wewe.
MUNGU ANASEMEHE MAKOSA YOTE MADAMU UMETUBU KABLA YA KUONDOKA KWENYE MGONGO WA ARDHI.
Anonymous said…
Tumekupata vilivyo Kim from A town,ni kweli katika hali ya sasa hivi hakuna wa kumnyoshea kidole mwenzake kwani vidole vilivyobaki vinakunyoshea wewe, ila ningependa kukuuliza swali moja, je ukiwaona watu wanafanya uchafu, na huo uchafu umezoeleka kwa hiyo jamii na wewe unajua kuwa ni uchafu utakaa kimya tu eti kwasababu imezoeleka!
Nafikiri kiuungwana ni heri uwaambie, ingawaje watakubeza, watakudharau, lakini umeosha mikono yako. Hii ndio wengi wanajaribu kufanya,kuonyana ingawaje jamii imeshalowea kwenye hilo unaloonya.
Ni kweli katika jamii zetu ni wachache wanaoingia ndoani kabla hawajaonjana, na manake wengine wanafunga ndoa wakiwa wameshazaa, na bwana huyo au mke huyo au na mume mwingine au mke mwingine, hii imekuwa ni kawaida. Lakini hii kawaida kaianzisha nani, ni mimi na wewe, na wakuiondoa si mwingine ni mimina wewe. Jetukae kimya na kusema hewala jama...
Kuna kwenda na wakati na mabadiliko ya nyakati kama rafiki yangu mmoja alivyonielezea kipindi cha nyuma,lakini mimi bado nasema huko kwenda na wakati na mabadiliko ya nyakati muanzishaji ni nani? Ina maana inakuja tu kama mvua? Haya mabadiliko tunayaleta wenyewe,na mengi ni ya kuiga tu,na wanaosababisha hayo ni wale ambao kwabahati mbaya wamekumbwa nayo na ili kuondoa ile aibu wanayasambaza ili yaonekane ni kawaida, huo ndio ukweli jamani.
Naombeni,twendeni na wakati na tuukubali `unyakati'lakini tukumbuke kuwa,sisi tuliishi vizuri na maisha yetu yalijengwa kitabia ambayo tuliiona ni njema, nasisi tunatakiwa tuwajenge watoto wetu na jamii zetu ili wasiharibike, tujiulize haya mabadiliko yana wema ndani yake?. Kwa wenye imani za dini,kila mmoja ni mchunga na siku ya hukumu tutaulizwa yale tuliyokuwa tukiyachunga, mzazi ataulizwa kuhusu mwanae,kiongozi ataulizwa kuhusu wafuasi wake, na mke na mume mtaulizwa kuhusu mahusiano yenu. Na Dinah ataulizwa kuhusu wadau zake jinsi alivyokuwa akituasa. Ni hayo tukwasasa
emu-three
Anonymous said…
Pole sana dada,
Mimi nakushauri zaa naye huyo mwaarabu kwa kuwa unampenda na unataka labda kuzaa mtoto aliyechanganyikana na iwe kumbukumbu yake huyo mpenzi wako uliyependana naye muda mrefu.

Mimi mwenyewe nimezaa na mwanaume mmoja ambaye sio kabila langu tulipendana kwa muda wa miaka 3 wazazi wake wakamwambia aoe lakini iwe ni kabila lake. akaniomba nizae naye mtoto nimezaa naye mtoto mmmoja sasa hivi yupo form II, Mwanaume ameoa na mke wake ananijua ingawa atupangiani zamu lakini mwanaume anakuja kwangu anashinda na anamtunza mtoto wake vizuri sana kwa nguo, chakula, ada nk. Mimi niliamua kuzaa naye kwa kuwa nilijua hata akinikimbia nitaweza kumtunza mwanangu kwa kuwa nina kazi na mahali pa kuishi. Najua mtataka kujua kwa nini sijaolewa ! Mimi nilikuwa nimeishaolewa na nina mtoto mmoja lakini mume wangu akafa kwa ajali na kwa kuwa nilikuwa bado mdogo ndo nikampata huyo kijana ambaye alikuwa hajaoa. Ushauri wangu hapa si mambo ya kuoana ila nataka kumwambia kuwa kama ana uwezo wa kumtunza mtoto wake azae tu ikitokea mwaarabu akamkimbia aweze kuishi maisha mazuri na mwanae mie sioni kama kufunga ndoa ndo kitu cha muhimu sana duniani.
Anonymous said…
Husijali dada yangu:

mimi ninachoona hapa dada, kama ulikua unampenda huyo mwalabu wako na kweli una uhakika nae anakupenda ingawa si lahisi kuusemea moyo wa mwenzio, lakini lazima utakua unajua huyo mwalabu wako anakupenda ama la, sasa basi kama anakupenda na wewe unaona moyo wako unampenda na unaona hakuna mwanaume mwingine ambaye anaweza kuchukua nafasi yake, basi wewe fanya maamuzi zaa nae ili na wewe uwe na raha ya kuwa na mtoto wake, maana hasikudanganye mtu raha ya kubeba mimba ni ubebe mimba na mtu unayempenda kutoka rohoni na utafurahia hiyo mimba yako na mtoto utakayemzaa, wasikukatishe tamaa eti subiri utapata wa kufunga nae ndoa, kwani ndoa vitu gani bwana!! wangapi tumewaona wemeolewa na hawana raha na hao waume zao ndani ya nyumba? na wamefunga ndoa baada ya mwezi mmoja ndoo imekua ndoano, hivyo kuolewa na kuzaa na kutoolewa na kuzaa yote ni sawa tu, watu wanapenda sana kufuata mkumbo kisa kaona naniii kaolewa basi na yyeye anataka kuolewa, ndoa ni tofauti ndugu zangu, kwa hiyo dada wasikukatishe tamaa, wewe kama umempenda huyo mwalabu wako na unaona kabisa roho yako inatamani kuwa na mtoto nae basi fuata moyo wako unavyokutuma ili ujifurahishe wewe mwenyewe sio ufurahishe moyo wa mtu mwingine, ukiamua kitu ni unaamua kwwa faida yako mwenyewe sio kwa faida ya mtu mwingine, kutafuta ushahuri sio kitu kibaya kwa wenzio au ndugu zako lakini ushauri wa kutoka kila kona utakuchanganya ndugu yangu, wewe lililopo ungemfuata mama yako mzazi au ndugu yako wa karibu sana akupe ushauri lakini sio kutafuta ushauri wa watu dunia nzima watakuchanganya ndugu yangu, maisha yenyewe haya kila mtu anafanya kile atakacho sio cha wengine watakacho, hivyo fuata roho yako inavyokutuma ufanye na ufanye uamuzi ambayo utakufurahisha wewe binafsi sio uhamzi wa kufurahisha jamii, hayo ni maisha yako tu utakapopata raha ya maisha yako akuna anayekujua ana utakapopata shida ya maisha yako hakuna atakayekujua, hivyo fanya maamuzi yako mwenyewe na ufuate moyo wako uanavyokutuma kuamua na kufanya kitakachokufurahisha maishani mwako na sio kufanya kitu kitakachomfurahisha mwingine, kama umempenda huyo mwalabu wewe zaa nae tu uwezi jua kwa nini aliamua uzae nae, kama alikua akupendi wala hasingepoteza muda wa kuanza kukwambia eti mzae, angeondoka tu na akapotea bila wewe kujua, lakini kama anataka mtoto na wewe unaona bado unampenda, wewe zaa nae tu na nina uhakika utaishi nae kwa amani tu ata kama ataoa mwanamke mwingine.
hashim258 said…
unafikiri vp wewe hata kuhitaji ushauri wa watu wengine?hujui kuwa kuzini mbali na ndoa ni machafu na matezo ktk dunia yako na ya hapo baadae>huyo mwanaume anaeye taka mtoto mbali na kukuoa ni mharibifu ktk maisha yako na ya mtoto wako.Mungu hakueka sheria ya ndoa kwa viumbe wake ila kuwa ni manufaa kwa wote mume na mke na yule atakae taka kuwa mbali na amri zake hupata majuto yasio na hali.Akili zenu nyie wanawake zipo ktk mikundu zenu mnajua kutombana tuu.Chunga na chekesha kabla hujachukuwa action....best man for best woman,the love which will live for long time.TAKE CARE/hashimalkaff@yahoo.com