Umbali wetu memfanya atoke, je niendeleze?-Ushauri

Habari ya leo dada dinah, pole na kazi za kutuhabarisha mambo kadhaa wa kadhaa yanayokua yanajadiliwa hapa. wengi wetu tunafaidika sana na masomo yanayokua yanajadiliwa.

Mimi naomba ushauri wa swala hili linalonitatiza kwa mda mrefu sasa. nimekua na relation na bf wangu kwa mda usiopungua miaka 4 sasa. mwanzoni mapenzi yetu yalikua mazuri sana naeza sema kama romeo n juliet but baada ya mda nikaanza kuhisi mwenzangu alikua anacheat.

Nilipomuuliza alikana akasema hawezi fanya hiyo kitu, ukapita mda tena same thing ikatokea hadi hao aliokua anacheat nao wakaanza kunipigia simu na kunitukana na maneno kibao ya kunikashfu lakini mwenzangu still alikana kua na uhusiano naye nakusema anamfahamu huyo mtu lakini hawana relation yoyote.

Miezi michache iliiopita niligundua kitu tena kwamba they have relationship na nilipomuuliza tena akaomba msamaha na kujutia yote aliyoyafanya kwenye relationship yetu na kusema wameachana na huyo dada na kwamba yeye ananipenda mimi na anasema anataka kunioa mimi.

Kuna wakati nilisema labda anafanya hivyo(cheating) kwa sababu muda mwingi tumekua tukiishi miji tofauti kutokana na majukumu tulionayo na kazi tunazofanya.

Sasa naomba ushauri kweli niendelee kumuamini kama kweli hii relationship itafikia kwenye hiyo hatua ya kua mume na mke au itaishia huku tu na kupotezeana mda?

Kweli nampenda sana na najua kama nampenda na sikatai once tukiwa pamoja i feel his love na hata nikiwa sipo nae communication za hapa na pale zinakuwepo sana.

Dada dinah na wadau wengine naomben ushauri wenu kwenye hili suala."

Jawabu: Habari ni njema kabisa, karibu sana mahali hapa. Pole sana, na pia napenda kukupa hongera kwa kuwa mvumilivu, hapo ni Gf tu......wengine wala tusingefika hapo ulipo!

Nimepata matumaini baada ya kuona kuwa umefanyia uchunguzi na kugundua kuwa ni umbali ndio unaweza kusababisha mpenzi wako atoke nje ya uhusiano wako.

Lakini nimekereka na tabia ya mpenzi wako kutokuwa muaminifu, kutojiheshimu yeye na mwili wake, Kutokuwa mvumilivu mbaya zaidi ni kukosa adabu na heshima kwako na kuigawa nambari ya simu yako kwa mtu anae-cheat nae na kuruhusu mtu huyo kukudhihaki na kukutukana ili akukatishe tamaa umuachie mpenzi wako awe wake moja kwa moja.....wanawake wengine wanastahili kuuwawa taratibu kwa mateso makuu akyanani!

Nilichokigundua kutokana na maelezo yako ni kuwa Mpenzi wako anajua na anauhakika kabisa kuwa unampenda, tena sio unampenda tu bali unampenda kwa dhati.

Penzi lako la kweli na dhati kwake linamfanya aamini kuwa hata akifanya kosa gani hutom-buti kwa vile unampenda sana na kwa dhati, anajua na anauhakika kabisa lolote atakalofanya na kisha kuja jieleza utamsamehe na kuendelea na maisha kama kawaida.

Sasa mpendwa baada ya kudhani kuwa umbali ndio sababu ulipaswa kupunguza umbali huo ili kuangalia kama kweli ndio sababu ya yeye kuchoropoka/kutokuwa muaminifu, kwa vile kisheria hamjafnga ndoa ilikuwa rahisi kwa mpenzi wako kukufuata wewe huko uliko (Kuomba uhamisho) au wewe kuhamia huko aliko nakuishi pamoja au karibu zaidi.

Kwa vile hilo halijafanyika mapaka tunavyoongea hivi sasa basi hujachelewa linaweza kufanyika wakati wowote kuanzia leo(kama unapenda na yeye anakupenda) ili kuona kama kweli uhusiano wenu unamaisha marefu au la!

Kitu muhimu cha kuzingatia kabla hujachukua uamiuzi wa kuhama kumfuata au yeye kukufuata jaribu kuwakilisha hoja hiyo kwake uone atalichukuliaje, akija juu au kukupa jibu lisiloridhisha ujue hakufai huyo tena toka "nduki" usiangalie nyuma.

Akikubaliana na wewe basi endelea kuangalia mwenendo wake, akiendelea na tabia yake chafu wakati mko karibu kama sio kuishi pamoja kwa
mara nyingine nakwambia toka "baruti" na uangalie maisha yako na hakika utakutana na mpenzi atakae kuthamini, heshimu na kukupenda kwa dhati.

Natambua itakuuma sana tena sana, itachukua muda mrefu kuanza maisha yako ya kimapenzi au hata kuoenda tena lakini siku moja yataisha na utakuwa "fresh", mwenye kujiamini, mwenye kupendeza, mwenye kuvutia.....kama hili litatokea na unahitaji ushauri basi njoo tena mahali hapa tutakuwa na wewe kila hatua ya maisha yako ya kimapenzi.......au sio wadau?

Kila la kheri!

Comments

Anonymous said…
mdogo wangu,kwanza nakupa pole,naelewa unavyoumia.Mimi nakupa ukweli wangu,hata kama atakuoa hiyo tabia hataiacha,namimi nazidi kukuonea huruma ameianza hiyo tabia kabla hata hajakuoa,inamaana hana upendo wa dhati na wewe,asingewaruhusu hawo wasichan awengine wakupigie simu hata kidogo,hapo anafanya ili akuumize maana ameshajua weekness zako.mi nakushauri uongee naye ,na kweli kama anakupenda akuoe.nakutakia kil la kheri.
Anonymous said…
Kwa kweli nyie wanawake mliumbwa na moyo wa ajabu sana. Yaani eti bf wako anacheat then unasema eti unataka kumsamehe. JE ungecheat wewe yeye angekusamehe? Huyo hata akikuoa ataendelea kucheat , achana naye. Chukua time, anza maisha mengine. Huyo si wako tena.
Anonymous said…
Kwanza pole sana kwa masibu yaliyo kupata. lakini nakuomba uchukulie kama ni fundisho ambalo litakufanya uwe stronge.

baada ya kusema hayo maomba nikueleze. huyo Bf wako kwa ufupi ameshapunguza mapenzi kwako. mwanaume anayekupenda endapo atagundua kuwa unamuhisi kuwa na mahusiano nje ya mahusiano yenu atakatisha haraka mahusiano ya nje ili asikuumize (huyu BF wako hajafanya hivyo jiulize)

pili jiulize huyo mwanamke mwingine amepataje number yako ya simu mpaka akakupigia na kukutukana? ni lazima ameiona kwa BF wako sasa jiulize mahusiano yao yamefikia kiwango gani cha mpaka huyo mwanamke kuwa na uwezo wa kupata namba yako na kukutukana( jubu lipo wazi)

tatu hebu jaribu kupima hii hali sasa na uiproject kwa miaka kumi ijayo them utapata jibu kamili.sababu katika hali ya uBF na uGF mapenzi huwa ni motomoto sasa dosari kama hizi zikianza kujitokeza basi tambua miaka kumi ijayo mambo yatakuwa si mambo.

ushauri wa bure:

muache huyu kaka sababu utazidi kuumia sana maana umbali umeshawatenganisha hata akikuambia ameachana na huyo mwanamke utaaminije na wewe upo mbali nae? so utakuwa na mashaka na mahusiano ya kutoaminiana sio mazuri hata kidogo

trust is erned and once destroyed is difficult to build it back.

mshukuru mungu kwa kukufunulia hayo and move forward.

ila uamuzi wa mwisha ni wako.

nakutakia kila la kheri
Anonymous said…
Unajua mimi nikisema hakuna uhakika wa mapenzi yenu mpaka `ndoa' watu wengine watasema nashabikia ndoa, ilihali nyakati hizi zinahitaji watu `wapimane kwanza weee' ndio itangazwe ndoa.
Lakini u-bf au u-gf haumbani sana mtu hasa akiwa hana uaminifu wa kweli, kwasababu hamjaingia kwenye mkataba wowote wa kumfanya mtu huyo aogope kufanya lolote, ikizingatia sasa hivi watu hawamuogopi Mungu.
Nasema hivi, sio kwasababu napenda anachokifanya huyo b/f wako, ila kiuzoefu, wapenzi wengi wanakuwa hawajiamini, kuwa huyu ndiye atakayekuwa wangu wa milele, au huyu ndiye atakayenifaa mpaka ile hatua ya kuvikana pete.
Sehemu ya u-b/f na u-g/f huwa ina mitihani mingi, na ukifanikiwa kumpata ambaye kweli mumeshibana umshukuru sana Mungu. Tamaa na vikwazo viko vingi na hasa pale mnapokuwa mbalimbali sana.
Lamuhimu kama kweli mumejiandaa ni kutangaza uchumba, hapo mtakuwa mumeingia kwenye mkataba ambao utamlinda kila mmoja wenu. Na kama mmoja wenu akiiba nje, huyo atakuwa `haeleweki' na ni bora ukajiandaa kwa mabadiliko.
Miaka minne ya urafiki ni muda mrefu na kama mngekuwa mnaishi karibukaribu ungelishajua `tabia' ya mwenzako `nje na ndani' , lakini kwa vile mnakaa mbalimbali, huwezi ukahitimisha moja kwa moja kuwa mwenzako ni `mchepukaji'. Yakusikiwa yapo, na yanaweza yakawa na ukweli au ya uwongo.
Tabia ya mtu haijifichi, kama ni muaminifu utamjua mapema na kama ni wakueleweka utamjua mapema.
Jambo jema ni kukaa na kuliweka wazi. Dunia ya sasa hivi ni kuwekana wazi kwa kuambizana `ukweli' na mwisho wa yote ili kuhakikisha kweli mnapendana ni kuvikana pete/kualika uchumba.
Hayo ndiyo yangu kwa leo.
emu-three