Tumekutana mtandaoni,nahisi penzi la dhati-Ushauri

"Nimetokea kumpenda msichana ambaye yupo mbali nami, namaanisha yeye yupo Dar nami nipo Tanga. Nilikutana naye kwenye "chatting sites" na alinipatia nambari yake ya Simu pamoja na picha nami nikampa zangu.

Najua mapenzi ya mbali wakati mwingine hayana uaminifu, sasa nitafanyaje ili anianimi zaidi kuwa nampenda kwa dhati, ingawaje huwa namuambia sana avute subira tutakutana."

******Ufafanuzi***Unahisi kumpenda kwa dhati, huwezi kupenda mtu kwa dhati kabla hujajua mambo mengu juu yake ikiwa ni pamoja kasoro zake na kujifunza kuishi nazo/vumilia.

Jawabu: Asante kwa kuleta swali lako mahali hapa, Ni kweli kabisa mapenzi ya mbali huwa hayana uhaminifu hasa kama hamjuani, kwamba hamjawahi kuonana/kutana. Kumuamini mtu amabe unajua kwa picha na sauti sio rahisi.

Mtu anajifunza kukuamini baada ya kukujua/fahamu kwa karibu zaidi au niseme kwa ktk hali halisi unamuamini mtu kutokana na matendo yake na sio maelezo/maneno sasa ili mpenzi wako mtarajiwa aweze kukuamini ni vema ukaanza kuonyesha mapenzi yako kwa kumtembelea au kumualika Tanga na kuwa-spend sometime pamoja ili kufahamiana vema.

Wapo watu wengi wamefanikisha mapenzi na hatimae ndoa baada ya kukutana kwenye mtandao kama ilivyotokea kwenu ninyi, na mara nyingi umbali huwa ni mkubwa zaidi na unagharimu pesa nyingi (Mambo ya nauli).

Lakini kwa bahati nzuri ninyi mnaishi karibu na pia gharama za usafiri sio kubwa sana, kama kweli uko makini na maneno yako basi mfungie safari hali itakayomfanya ajifunza kukuamini kuwa unampenda kweli.

Kila lakheri!

Comments