Kutoa mimba ni sahihi?-Ushauri!

Bonyeza hapa kuona Picha inaonyesha kiumbe (mtoto) kilichotolewa, kilikuwa na umri wa wiki nane tumboni ambazo ni sawa na miezi miwili.
"Natoka nje ya mada kidogo naomba mitizamo yenu Dinah na wadau wengine katika suala la abortion/utoaji mimba je ni sahihi kwa wapenzi kutoa mimba baada ya kuingia bila kutarajiwa?kama hawajajiandaa na pia kuwa tayari kwa mtoto kifedha na hata kindoa-TEITEI".

Mtazamio wangu:Teitei nashukuru sana, hili swala bado ni nyeti sana kulizungumzia japo kuwa linafanyika sana ktk jamii nyingi hapa Duniani ikiwa ni pamoja na hapa nyumbani Bongo, ni kama ilivyo kwenye kuzungumzia ngono kwa uwazi/adharani.

Maelezo nitakayoyatoa ni ya wazi pia ni hali halisi, lakini kusema nitakacho sema sio kwamba naunga mkono swala zima la utoaji mimba. Mimi binafsi naamini kuwa utumiaji wa madawa ya kuzia mimba hasa ile "Morning after" ni utoaji mimba, lakini hili watu hawalioni au kulizingatia mpaka mimba ijengeke ndio wanaona "big issue", lakini katika hali halisi kuzuia mimba (unaruhusu iingie lakini isijengeke) na kutoa mimba (unaruhusu iingie na ijengeke kisha unatoa) kwangu mimi ni mauaji ya viumbe visivyo na hatia.


Kwa mujibu wa Imani zetu za kidini utoaji mimba sio sahihi na huesabika kama mauaji ambayo ni dhambi, lakini wakati huohuo mama anaweza kulazimika kutoa mimba kutokana na matatizo mbali mbali moja likiwa ni matatizo ya kiafya ambapo Daktari hupendekeza hilo, hili hufanyika kwa kufuata hatua za kisheria na vilevile kuzingatia maamuzi ya mama na baba wa mtoto, kwamba wako radhi mtoto afe mama abaki au wote wawe hatarini kufa ikiwa mimba haitotolewa.


Swala lingine ambalo ni la pili linaweza kufanya/sababisha pea/wenza watake kutoa mimba ni kutokuwa tayari kwa hilo kama ulivyosema hapo juu, kwamba mimba imeingia kwa bahati mbaya bila ninyi wawili kupanga, kwamba hamko tayari kuwa baba/mama au mnajua wazi kuwa hamtomudu malezi ya mtoto atakae zaliwa.

Natambua unataka kuuliza "kama ulijua hukua tayari kwanini sasa ulingonoka?" hebu tuwe wazi na nafsi zetu, ni wangapi hufikiria mimba au kuzaa pale tunapokwenda kufanya mpenzi au pale tunapovutiwa na wapenzi wetu? Mimba ni matokeo ya kungonoana na ni wajibu wetu (wake kwa waume kuwa waangalifu) lakini wakati huohuo tutambue kuwa kuna bahati mbaya ambayo husababishwa na watu kutojua kikamilifu kile wanachokifanya (ngono) kutokana na swala zima la ngono kuwa siri miongoni mwetu.

Tatu ni mwanamke "kumimbwa" na mwanaume aliyem-baka, kutokana na tendo lenyewe ambalo ni la kikatili na limefanywa na mtu ambae humjui, humfanya mwanamke kuathilika kisaikolojia na kiakili nakutaka kutokuwa na kumbu-kumbu ya mkatili huyo na njia pekee ya kuondokana na hilo ni kutozaa mtoto wake (m-bakaji) ambae akizaliwa ofcoz itakuwa kumbukumbu mbaya na ya maumivu makuu.

Kwa nchi zilizoendelea kunavituo vyakuwalea/angalia wanawake waliobakwa namimba zao na mara tu watakapijifungua watotow aliozaliwa huchukuliwa na kutafutiwa familia amabzo zinahitaji watoto, na kipindi chote hicho mwanamke huyo huenda kozi kali ya ushauri nasaha mapaka atakapo jifungua.

Kutokana na mfumo wa maisha tunayoishi sasa swala zima la utoaji mimba (kwa nchi zilizoendelea) limeachwa kwa mwanamke husika, kuwa yeye ndiye mwenye uamuzi wa nini kifanyike juu ya mwili wake na kabla hilo halijafanyika ni lazima mama huyo apatiwe ukweli wa athali/madhara na hatari za kutoa mimba, anatakiwa kufanya hivyo wakati gani, aina gani ya utoaji wa mimba anaitaka kisha wanakupa muda ukafikirie kabla hujaendelea na utoaji mimba.

Ukirudi baada ya muda waliokupa na ukawa na msimamo uleule wa kuendelea na uamuzi wako basi unapewa ushauri nasaha na unaelezwa tena nini kitafanyika, athari na matuzo baada ya huduma kukalimika alafu ndio wanaendelea....kutokana na maelezo yangu utatambua kuwa wenzetu wamelikubali na kuliweka wazi ili kuepusha utoaji mimba ambao sio wa kitaalam.

Asante.

Comments

Anonymous said…
Mimi kama mimi siungi mkono kabisa `utoaji wa mimba' labda, na tena labda `doctor' ashauri hivyo, kiusalama wako na kiumbe kilichopo tumboni, na sio maswala ya kifedha na ugumu wa maisha.
Kitu kikubwa, (hapa nazungumzia kama mimi)nikujiuliza wewe mwenyewe, mfano ungekuwa ni wewe upo tumboni kipindi hicho na `wazazi' wako waka-amua kukutoa, ungekuwepo sasa hivi? Wengi watasema hiyo ni `ngeli' tu, lakini kama wewe au mimi tusipoweka `ngeli' katika maisha yetu hatutajihisi `jinsi wenzetu wanavyojisikia'. Hatutakuwa na huruma katika nyoyo zetu.
`Unapomfanyia mwenzako kitu jiulize kwanza `kama ingelikuwa mimi nimefanyiwa hivyo ingekuwaje?'
Ndio utasema hicho ni kiumbe ambacho hakijakamilika, na unaogopa `maisha yake ya baadaye, au yako ya baadaye' Lakini wewe una uwezo gani wa kupima maisha yako ya baadaye, wewe unajuaje `huko baadaye kwako itakuwaje?' Huenda huyo unayemtoa ndiye pekee uliyekuwa umepangiwa?' Imani hiyo kweli hatuna?
Yapo maswali mengi yakujiuliza, hasa unapotaka kufanya jambo kama hilo, kwani kwa asilimia kubwa, matokeo ya baadaye hayapo ndani ya uwezo watu. Uwezo ulionao ni wa maaumizi ya busara tu. Na maaumizi mema nikutoitoa hiyo mimba, na ni vyema ukashauriana na mwenzako jinsi gani ya kuilea hiyo mimba na maisha ya baadaye mema tu.
Ngoja niwaachie wenzangu na Dada Dinah yupo kwa ajili yetu
mimi
emu-three
Anonymous said…
Dina please niko chini ya miguu yako naomba toa hiyo picha inanikumbusha kitu ambacho sitaki kukumbuka.
Anonymous said…
Mh dada dinah hiyo picha inatia uchungu sana itafanya watu kufikiria mara mbili swala la kutoa mimba.Lazima waliotoa mimba kubwa zaidi ya miezi miwili wajisikie vibaya baada ya kuona kiumbe hicho.
Anonymous said…
Kumbe miezi miwili mtoto anakuwa kamili kabisa?Jamani tukishika mimba na tuzitunze kwa dhiki na faraja na tuwapende watoto wetu
Anonymous said…
Wadau na Dina nimewapata na ninashukuru kwa michango yenu.
ITEITEI