Tekinolojia ndani ya mahusiano yetu ya kimapenzi.

Kutokana na kukua kwa tekinolojia watu wengi tumekuwa tukitumia muda mwingi kwenye Komputa (Internet), simu za mikononi, Luninga na vifaa vya umeme (Gadgets) na kutumia muda kidogo na wapenzi wetu hali inayoweza au inayopelekea mtafaruku ambao huatarisha maisha yetu ya kimapenzi na wapenzi wetu.

Sasa basi leo nikirudi kutoka Kariakoo nitaelezea hilo kwa kina ili kutambua nini kinaendelea akilini mwa wapenzi wetu japokuwa wanaonekana hawajali wewe kukeshakwenye Komputa.

Karibu mida-mida tushirikiane ktk kuzungumzia hili.

Ty.

Comments

Anonymous said…
hapo umegusa penyewe,lakini naona unawalenga wasomaji wako.kule kilamba nyoka hata umeme hakuna,kazi kweli
Anonymous said…
Ujumbe ni ujumbe tu.

Lete vitu dada, maana kama ulivyosema, internet isipoangaliwa kwa macho matatu, inaweza kuleta vurugu na kutokuwepo kwa maelewano kwa wapenzi.

Anano wa juu hapo, ni kweli Dina anawalenga watumiaji wa internet ambao pia hupitia blog yake, maana wasio na internet hii habari haiwahusi. Wao kutakuwa na kitu kingine chenye kuchukua nafasi hiyo, labada TV au soga.

Kuna watu wengine hata kama anaumwa anaweza kuwasha computer kucheki email ila akashindwa kufanya kitu kingine chenye manufaa kwa mpenzi wake. Tena kamtindo haka kapo sana hapa Dar hasa kwa sasa kuwepo kwa mtandao kwenye kila kampuni ya simu na wenye computer zao nao ni wengi kuliko walioko mikoani.