Samhani! Lakini hii imeniuma sana.


Well, mimi binafsi sijawahi kuona haya mambo yakukeketwa mpaka asubuhi hii; Jamani kuna mila za kutokomeza.....huu ni ukatili wa hali ya juu.




Inaudhunisha sana.


Nitaendelea na somo la mwisho la matiti, pole kwa usumbufu.

Comments

Anonymous said…
Mtume! Yaani wakawaaachia wazungu kwenda kushuhudia ukatili wao. Alafu mbaya zaidi aliye kuwa na ujasili wa kupost hii ni mwanaume.

Wanawake tuamke sasa jamani heee.
KKMie said…
Yaani inasikitisha na kuudhi sana. Hii yote ni ubinafsi wa wanaume uliopandikizwa miaka ilee ambayo ndio utamaduni.

Akyanani kama hawa jamaa wapo bado wanafanya hii kitu kule Umasaini, Musoma, Mikoa yakati pale tafadhalini wekeni sheria ya kukabiliana nao....huo ni unyama!
Anonymous said…
ni sifa ya mwanamke ktk tamaduni zao,bila ya kukeketwa anakuwa bado hajakamilika.lakini si kitendo kizuri kwa ustarabu wa sasa.
Anonymous said…
uyo mtu aliyebuni iyo kitu?
Anonymous said…
yaani wewe Dinnah ulifikiri kukeketa ni kama kukata kucha? hadi uone youtube ndio unajua? ama kweli una mengi ya kujifunza. usiwe kama tomaso bana yaani hadi uone. Mbona mie nimeeenda kaujaribisha staili ya kusigida na sulutani bila ya kuone kwenye youtube? yaani nilifuata malelekezo yako tu.

Nyie hao wazungu achaneni nao sio ajabu hao kina mama hawakujua hio ilikuwa kamera au labda ilikuwa hiden camera pia inaeza kuwa jamaa wametengeza animesheni, kwani hujaona bahari inagawanyika ktk muvi ya teni komandimenti wakati musa anawaongoza wana iziraeli toka misri kwenda kanani?
Simon Kitururu said…
Inasikitisha sana hasa kuona jinsi jamii inavyoweza kuhalalisha kitu kama hiki na kufanya baadhi ya waathiriwao(wanawake, wako wengi tu) wateteao kwa nguvu zote mila kama hizi.Wanaume ni wakulaumiwa kwa kuanzisha jambo hili , lakini imefika muda wa wanawake pia kustukia swala na kutokubali mila kama hizi ziwe ndio kigezo cha kukubalika katika jamii.
Anonymous said…
what about extreme xxx, sexbondage, child prono,peodophilia na kutiana na mafarasi mbwa na vigunguti vyengine vimachine nakuzibana pumzi kukojoleana mkijo nakunyeana mavi wanafanya hao walioenedelea...ni sawa?
KKMie said…
Anony wa 28 saa 06:22
Tomaso ndio nini?
Ni wazi kuwa uelewa wako ni mdogo kwa vile umenijibu mimi kama Dinah badala ya kutoa maelezo kuhsu mada husika (kukeketwa) pia umeweka mfano ambao ni wa kufurahia na unakupa raha TOFAUTI kabisa na kukeketwa hali inayoashiria hujaelewa au huji madhara au adha ya kukeketwa.

Hakika nina mengi ya kujifunza kama ilivyo kwa yeyote kuwa tunajifunza kila siku, ila sitarajii kujifunza jinsi ya kukeketa mtu.

Swala la ukeketeji linasikika na tunaelezwa inavyokuwa na matatizo wanayoyapata wanawake hao lakini unapoonda mtu anafanyiwa ktk hali halisi unapata hisia nyingine ambayo ni tofauti na kusikia sio?

Jifunze kuelewa sio unakurupuka na maelezo ya kipuuzi yaliyojaa chuki.
KKMie said…
Simon naungana na wewe kuwa Wanaume ni wa kulaumiwa kwa vile bila wao wanawake wasingekeketwa ili kuondolewa hamu ya kufanya ngono na wanaume wengine ikiwa waume zao hawapo majumbani.

Ni ubinafsi wa hali ya juu na tunahitaji mabadiliko kama hili bado linaendelea huko vijijini ndani ya Bongo.
KKMie said…
Anony wa tarehe 28 saa 12:33, hao wanaofanya hayo mambo sio Waafrika au niseme waTz, hata kama wanafanya haiwapatii maumivu kama ya kukeketwa.

Wengi wao wanafanya hivyo kutokana na sababu zao binafsi na hawalazimishwi (their choice) wanaamua kufanya hivyo tofauti na swala la kukeketwa.

Tumfikirie binti huyu mdogo, anakatwa kisimi na vinyama vingine kule ukeni, tena bila hata gazi kwaajili ya mwanaume au ili aolewe.

This one here isn't a choice, they've bn forced kufanya hivyo.

Binti huyu akiolewa anafanyishwa shughuli zote za ndani + kumliwaza mume kimapenzi/ngono bila yeye kufurahia/pata utamu/raha, anakuja kuzaa kwa taabu na maumivu makuu(acha yale ya uchungu) n.k.

Jamani mwanamke hana nafasi ktk jamii toka anakuwa ni mtoto wa...kukeketwa
anakuja kuwa mke wa....kuzaa kwa taabu
anakuja kuwa mama wa....malezi na shughuli zote za nyumbani
anamalizia na bibi wa....mkeketaji.

Nazungumzia mwanamke halisi wa kijijini sio ninyi wa mjini.....tuwasaidie wajikomboe ei?
Anonymous said…
lakini tunasahau kuwa wanaofanya kazi ya kukekete ni wanawake wenzetu na si wanaume.kumbuka mila ni imani aina tofauti na imani ya kidini.tuzidi kuelimishana ili kutokomeza hii tabia.mimi nakerwa na tabia ya sasa ya kujitoboa toboa hata sehemu nyeti,hii ni sawa na tohara
Anonymous said…
mimi ndio Anony wa 28 saa 06:22.

Dinnah ulikuwa huna haja ya kutukana wala kujibu kwa jaziba maelezo yangu, kwanza wewe hii bulogu ni ya kwako sasa ukianza kunambia ulewa wangu ni mdogo, maelezo ya kiupuuzi na vitu kama hivo huoni kwamba hata wewe unashindwa kujibu hoja badala yake unatukana?

Kama uliona maelezo yangu ayalikuwa si ya msingi ulikuwa na uhuru wa kuyatoa ulikuwa huna haja ya kutukana pale mtu anapokuwa na mawazo tofauti na wewe!

Mboni wewe umeeleza mambo kibao ya kiasherati humu lakini hakuna mtu amekujia juu? au unafikiri yoote unayoyaeleza humu ni ya maana kwa kila mtu hadi watoto wadogo?

Unavoelezea namna ya kufanya sex kwenye hii bulogu yako huoni kwamba unawafundisha watoto wadogo dunia nzima mambo ya watu wakubwa tu? huoni athari inayoweza kuletwa kwa jamii kuotkana na maelezo yako?

Huoni kwamba watoto wadogo wa kike na wakiume wataenda kufanyia kazi maelezo yako na wakaishia kupata ukimwi na mimba kabla ya wakati na hatimaye kuharibikiwa kimaisha na hata kufa?

Tuvumiliane tu Dada dinnah, wana adamu tuko tofauti, tunafikiri tofauti na tunatafsiri mambo tofauti ndio mana unaandika hapa kwene bulogo na sizania kama unategemea kila kitu unaandika basi kila mtu akubaliane nacho, pale panapokuwa na tofauti just bite the bullet and move on huna haja ya kutukana na name calling.

Haya ukitaka iwachi hii post ukita bandua, bulogu yako una uhuru wa kufanya utakalo na usitegemee wasomaji wako watakuabaliana na wewe kila kitu.
Anonymous said…
Swala la kukeketwa wengi wanaolipinga inaonekana hawajui background yake. Kuna uhusiano gani wa kukeketwa na kuongeza uchungu wakati wa kuzaa? nini hasa kinacho mafanya mtu aliyekeketwa kuzaaa kwa taabu? Ukifanya utafiti wa kina utagundua kwamba ktk jamii zinazokeketwa kuna asilimia ndogo ya wamamama wanaozaa kwa matatizo.

Unapotaka kuelimisha kuwa ukeketwaji sio mzuri toa validi reasons sio vitu vya kutunga tu. Ukiwaambia wamasaiau wagogo au wakurya eti acheni mila zenu kwa sababu ukikeketwa unakuwa na maumivu na kuzaa kwa tabu wanakuwa hawakuelewi.

Hivi unafikiri mila za kufanyiwa plastiki sajare ni nzuri zaidi kuliko kukeketertwa? unafikiri hakuna uchungu kufanyiwa plastiki sajare? hivi kufanyiwa tomi taki hio ni mila poa? hazisababishi matatizo hapo baadaye na hata vifo?
Anonymous said…
Oooh dinah nilisahau kukuambia tomaso ni nini/nani. tomaso ndio yule ambaye hakuamini kama yesu alikuwa amefufuka hadi alipomkagua na kuhakikisha ana vile vidonda alivopigiliwa misumari msalabani
KKMie said…
Anony wa 30 saa 06:48, sidhani kama kunamtu anapinga mila hiyo bali wanasikitika kuonakuwa mwanamke anaonewa kwa manufaa ya mwanaume.

Sidhani kama unahitaji utafiti kuhusiana na ugubu wa kuzaa kwa wanawake waliokeketwa, huenda sio wote lakini wale ambao huojiwa (ndani ya Tz) walikuwa wakilalamika kuwa hupata maumivu makali na wengine kuchanika au kupelekea kuongezewa njia ili mtoto atoke vema.

Swala la kujirekebisha ulivyooumbwa kunakofanywa na wazungu hakuhusiani kabisa na swal ala ukeketaji, hao jamaa wanafanya hivyo kama choice sio mila wa desruri ladba tuite utamaduni wa watu wakisasa ktk nchizilizoendela na sidhani kama kuna mbongo wa kaiwada anaweza kumudu kufanya hivyo wakati senti ya kulisha familia hana.

Nazungumzia wale walioko kijijini ambao ndio wanakeketwa.

Kuna kesi tofauti nimewahi kupata kutoka kwa wanawake waliokeketwa ni wazi kuwa hawapati raha wanapofany amapenzi na hawa nadhani ni wale ambao hawawezi kufurahi tendo hilo uume ukiwa ndani nahivyo wangepara utamu huo japo kidogo kwenye kisimi.

Usibishe na kuwa mkali kwa vile ulikeketwa maiaka ile, kuna tamaduni/mila zimepitwa na wakati nahatunabuni kuwashawishi watu waache tuishi kawaida tu kama wanawake wengine ktk mikoa mingine ya Tz.

Acheni kuwakandamiza wanawake, wapeni elimu ya Dunia acheni mila za kipuuzi za kupeana maumivu au niseme kilema.
KKMie said…
Asante kwa kunielewesha kuhusu Tomaso, hahahaha kumbe!
KKMie said…
Anony wa tarehe 30 saa 06:48, asante kwa maelezo yako lakini sikumbuki kama nimetukana mahali popote ktk maelezo yangu na wala sijajibu kwa jazba(mimi ni mtu wa kufurahi @ all times).

Napenda kupata/soma maelezo tofauti kutokana issue husika ili watu waweze kujifunza zaidi, lakini huoni kuwa ulikuwa kama unani-attack badala ya kuchangia swala nililoliweka hapa?

Soma vema maelezo yako ya awali utagundua kwanini nimetumia sentensi ya "uelewa wako mdogo".

Kuhusu swala la ngono, ngono inafanyika na inafanywa na watoto wa dogo kabla hata mimi sijaanza kuandika haya mambo hapa last May.

Ninayoyazungumza hapa sio mambo yakishetani ni mammbo matakatifu kabisa nakila mtu anapenda nakufurahia kufanya/fanywa.

Wakati nikiwa darasa la nne mwaka 1987 kulikuwa na mabinti wanafanya ngono na wakati huo mimi nilikuwa sijui kitu hivyo sidhani kama mimi nasaidia au kushawishi watoto wa jifunze ngono isitoshe si watoto wengi wa kibongo wenye uwezo wa kuwa na mtandao hilo moja.

Wengi wanajifunza, ikiwa wewe unaona ni ya kishetani basi tembelea blog za mambo ya Dini, ziko nyingi tu.

Asante kwa ushirikiano wako na kuweka wazi yaliyoujaza moyo wako.
KKMie said…
Anony wa 29 saa 14:43, ni kweli wanaofanya hivyo ni wanawake hao-waho kwa vile wao walifanyiwa ila baadhi walio-ondoa mavumbi (pata elimu)hukataa kuwafanyia binti zao tohara.

kama ulivyosema utamaduni wa watu wa magharibi wa kujitoboa hadi ukeni si mzuri lakini kumbuka kuwa mwanamke huyo anajifanya hivyo akiwa mkubwa na ni choice yake halazimishwi au kufungwa na mila/utamaduni wa kwao.

Tofauti kabisa na Binti mdogo wengine ni chini ya miaka miwili....masikini hajui hana choice ya kukataa wala kukubali wanamkwangua tu alafu akijakuwa mkubwa anapata matatizo, yaani anakuwa na uke kwa ajili ya mwaume kufurahia na yeye hapati raha yoyote...kwa kweli Elimu inahitajika sana tu huko kwa wahusika.

Nakumbuka miaka ya 2000 mwanzoni kuna mama mmoja alikuwa kwenye chama cha wanawake Tz alikuwa akiitwa Laila Shah (kama nakumbuka vema) alikuwa akiendesha kampeni yakutokomeza tohara, sijui sasa wamefikia wapi.

Pelekeni watoto shule,wafunzeni maswala muhimu yatakayowakomboa kama wanawake na sio kuwakokoloa huko chini bila ridhaa yao.

Tuenzi mila nzuri kama zile za mwanamke kuwa mwanamke(tuache kiburi cha usawa), desturi ya mwanmke kuwa mlezi mkuu (watotow anaharibika sikuhizi kwa vile mama na baba wote wako busy) hizo ndio desturi sijui mila za kuendeleza kwani zinamanufaa sio kupeana vilema vya nyuchi mweee!
Anonymous said…
Dinnah mie hapa hunibandui wala nini, shukurani zangu ziende kwa Simon Kitururu kwa kuweka link ya bulogu yako pale kwake.

Afu wewe husomi vizuri unakurupuka tu kujibu (kumbuka kukurupuka ni neno lako) Mie sijasema kishetani nilisema kiasherati. eneweiz. Nilichotaka kukuambia ni kwamba habari ya namna ya kufanya matusi inaeza isiwe nzuri kwa watoto wadogo pamoja na kwamba unasema tayari wanafanya matusi enewei.

sijui kama una wawatoto au la, lakini kama mtoto akifanya kosa sizani kama una muinkareji kwa kumuonesha namna nzuri ya kuendelea kufanya kosa hilo. kwa wewe kuweka hii kitu wazi wazi ivi ni kwamba unawaambia hao watoto heeeei endeleeni kufanya matusi na ili mfaudu zaidi hebu fanya sigina na sulutani n.k. By the way I tried sigina and I kinda liked it! Thanks to you.

Turudi kwenye kukeketa, mie natokea kwene moja ya makabila yanayokeketa kusema kweli hio ni kalcha iwe nzuri au mbaya iko deep rooted kwenye hizo society na watu wengi wa huko wanaikubali tu kwa hivo jamani kutuelimisha ili tuwache hio kalcha sio kitu ya kuamka leo na kuanza kuwaambia ooolololo acheni sio vizuri.

Inabidi strategy iwepo na kitu mbadala kiwepo cha kuwashauri ili waachane na kalcha hiyo, huezi sema tu hio mbaya wacha. manake kwenye kukeketa ni parti tu ya the whole thing in other word ni part tu ya "jando na unyago" huko ndio vijana wanafundishwa kila kitu cha watu wazima, hio ndio transition kutoka utoto kwenda utu uzima. sasa unapo waaambia wawache kukeketa manake una waambia wabakie kuwa watoto siku zote.

Ni kweli kabisa kukeketa kwa wadada mie sipendi pamoja na kwamba natoke huko pia lakini sio kitu ya kuwaambia acheni bila validi reasons. Pia kitu mnatakiwa kujua ni kwamba hawakeketwi watu kwa ajili ya wanaume, wala sio wanaume wanaoshinikiza kukeketwa wa wanawake. the simple reason wanafanya ivo ni kastom endi kalcha na hio haitastopishwa kama gari kwa kushika breki hata gari ukishika breki ikiwa kwene hai speed haitasimama.

tena nikwambie nini Da dinnah bora watoto wasichana wakeketwe in ana organized way kwani kinachotokea sasa ivi baada ya serikali kupiga stop ni kwamba watoto wa kike wenyewe wanajikeketa na matokeo yake wanajikeketa vibaya kwa mana wao sio wataalam wa kukeketa!

Kumbuka Dinaah siongei ivi kwa shauri nimeona video naongea ivo kwa shauri nimeyaona hayo kwa mecho yangu. Unajua nini hata wanaume wanakeketwa kwa kutumia kisu tena bila ganzi wala nini na hiko kisu kina wakeketa zaidi ya mtu mmoja, hii ni hatari kwa maambukiza ya magonjwa ya kisasa.

Kwa ivo jamani kinachotakiwa sio kuwashambulia/kutushambulia na kutuambia tuache mila na desturi zetu bali tuelimishane kistaarabu tu. Kumbuka kila wakati mtu akifanya kitu kibaya siku izi utaskia watu wanasema huo sio utamaduni wetu sisi watz, sasa sisi tukifanya utamaduni wetu pia mnatushambulia! sasa je utamaduni wa mTanzania ni nini hasa?

ndimi anon mwenye uwezo mdogowa kufikiria na mkurupukaji according to Dinnah. lol
Anonymous said…
dada dinah hakika wewe ni mwelevu na umejaa hekima....
nakupenda sana
Stela
Anonymous said…
Kusema kweli Dinah hata mie uliniudhi jinsi ulivyomjibu huyo anony wa 28 August 2007 06:22. Sikupenda kabisa, tambua kuwa wanadamu tu tofauti na mitazamo yetu ni tofauti. Huo ulikuwa ni mtazamo wake kwako, sasa mwenzetu wewe dinah inaonekana hupendi kukosolewa! Kuna siku za nyuma mie nilishawahi kukutolea maoni kuhusu topik fulani, nadhani ulikuwa unataka kutusimulia jinsi ya kujisafisha ukeni. Nikakwambia dinah unatuboa mbona maelezo huleti? Ukanijibu kuwa eti silazimishwi kuingia bloguni kwako, Sawa.. nakubali. Lakini kumbuka sisi ndio tunafanya hii blog yako iwepo. Kama hutapata msomaji/mtoa maoni, sidhani kama wewe mwenyewe utapenda. Manake itakuwa inaonekana kama unaandikia watu hewa!

Mdogo wangu jaribu kuwa na busara kidogo. Jifunze kujitambua mwenyewe ili iwe rahisi kuwatambua wengine pia.

Ni hayo tu. Zaidi ya hapo nakutakia kazi njema, uzidi kutuelimisha.
KKMie said…
Anonye wa 31 saa 05:55 asante kwa maelezo yako ya kina kuhusu ukeketaji, sasa kwanini pale mwanzo hukuja na hayo badala ya kuni-attack mimi?

Well, huenda hukuelewa vema nia na madhumuni ya mimi kuweka hiyo Vid hapo.

Natambuwa huwezi kukataza mtu kuacha mila yake bali unaweza kumelimisha kwa kuweka wazi madhara ya kufanya hivyo na faida za kutokufanya hivyo.

Asante kwa suhirikiano wako.
KKMie said…
Asante Stella hata mimi nakupenda wewe na wanawake wote wa Kibongo.

Karibu sana.
KKMie said…
Hahahahaha sasa wewe uliponiambia kuwa naku-bore ulitegemea mimi nikwambie nini? Hakuna mtu analazimishwa kuja kusoma/tembelea hapa, ni choice ei?

Anony wa tarehe 31, saa 12:38 kuna tofauti kati ya ustaarabu/busara/ujinga na uoga, mtu hawezi kuni-attack mimi nikabaki na ustaarabu wangu tu.

Kilicho wekwa hapa ni Vid ya tohara, inakuwaje mtu atoe maoni/mtazamo wake kuhusu mimi badala ya swala lililokuwa linazungumziwa? (huo ni uswahili a.k.a kutokuwa mstaarabu).

Napenda kukosolewa na ninakaribisha kukosolewa kwani ndio kujifunza kwenyewe lakini pale sikukosolewa nili-attack-iwa.

Mimi sijui kujivunga ili kufurahisha kila mtu, huwa naongea-type even kile kinachonijia kichwani kwa wakati huo kutokana na nilichokielewa kwa wakati huo.
KKMie said…
This comment has been removed by the author.
KKMie said…
Nasikitika kusema kuwa sitokuwa nikitoa maelezo ya wasomaji yenye asili ya malumbano yaliyo nje ya kile ninachozungumzia (somo a.k.a mada).

Nachukua nafasi hii kuwahabarisha wasomaji wachache wenye kupenda malumbano na labda kutofurahia kile ninachokiandika hapa, kwamba naandika kwenye blog hii kwa kujitolea kwa vile napenda kuandika na kuzungumzia mambo kuhusu wanawake, ngono, mapenzi na mahusiano.

Sifuati nani anafanya nini kwenye blog yake bali nafuata kile ninachotaka kukifanya kwenye blog yangu kama Dinah.

Unafurahia karibu tushirikiane....
Ikiwa hufurahii na unakuja hapa kulumbana na mimi badala ya kuchangia au kutoa maoni kuhusu somo husika nakushauri utafute kitu kingine cha kufanya.

Asanteni kwa ushirikiano wenu.