Betty!

Mpendwa Betty pole kwa kutokujibu kwa wakati, hii ni kutokana na wingi wa shughuli. Kwanza kabisa napenda kukupongeza kwa uwazi ulionao wa kuzungumzia swala hili hapa, watu wengi huficha na kutoomba msaada wa kitibabu au hata ushauri tu wa kawaida kwa sababu ya uoga, kutokuelewa kama ni tatizo au aibu ya kujadili swala hili.

Kama nilivyosema kwenye maelezo yangu ya awali (wiki iliyopita) kuwa tatizo hilo huenda likawa limesababishwa na ulegevu wa misuli (pelvic floor) ambayo hufanya kibofu cha mkojo kufunga na kufunguka, ikiwa msiuli hii ikalegea basi tatito la kutokwa na mkojo ukicheka, hema kwa nguvu, kukohoa n.k. hujitokeza.

Tatizo hili linaweza kumpata mtu yeyote na sio wanawake pekee bali hata wanaume na watoto na husababishwa zaidi na unene kupita kiasi, uzee, Kuugua mara kwa mara, matatizo ya kupata choo, kuanza ngono mapema, matumizi ya madawa ya kuzuia mimba, na zaidi husababishwa na uzazi.

Ninachokushauri ni wewe kwenda kumuona Daktari wa magonjwa ya wanawake na atakusaidia ili kupunguza na kuondoa kabisa kero hiyo, huenda ikawa dawa, mazoezi vilevile anaweza kukushauri utumie bidhaa maalumu kwa ajili kuvuja mkojo bila kujitambua/kusudia.

Kila lakheri.

Comments

Anonymous said…
Asante Dina kwa ushauri wako,ubarikiwe!
KKMie said…
Tubarikiwe sote Betty. Nakutakia kila lililo jema ili kuondokana na karaha hiyo.