Kwenda nje ya Ndoa/Uhusiano/ukware/Umalaya

KWA maana ya haraka haraka ni mtu asiye na adabu/heshima, huruma, utu, muharibifu, mkatili, mlafi, mshamba na ni muuaji vilevile.

Tatizo hili limekithiri katika jamii yetu na sasa limekuwa ni jambo la kawaida kwa baadhi ya watu au kwa maana nyingine wamefanya kuwa ni utamaduni wa kisasa (kwenda na wakati).

Tabia hii mbaya huathiri kwa kiasi kikubwa baadhi ya familia hasa ikiwa muhusika yuko ndani ya ndoa na amefanikiwa kupata Watoto.

Tabia hii haiko ndani ya ndoa pekee bali hata katika mahusiano ya kawaida ya kimapenzi tofauti ni kuwa ndani ya ndoa akina Baba ndio wako mstari wa mbele na walio nje ya ndoa baadhi hulipiziana visasi.

Wanawake walio katika ndoa hujitahidi kuwa wavumilivu wakiamini kuwa ndoa ni uvumilivu. Hapana! ndoa ni kuvumiliana (wote wawili) ikiwa mmoja wenu anamatatizo kiuchumi, kuugua, ajali n.k, lakini sio kwenye Uasherati jamani mwee!. Mimi wangu akitoka nje naua aisee!(hahahaha natania ila hatonipata tena)

Baadhi ya wanawake hushindwa kufanya uamuzi hasa ikiwa mwanaume ndiye “kitega uchumi” au wanafuata maadili mema ya mtanzani (utakufa kwa ngoma na maadili yako shaurilo). Wengine hung’ang’ania kubaki katika ndoa “for the sake of kids” na hii ni kutokana na kutokuwa na kipato kitakachomfanya amudu maisha yake na watoto ikiwa ataomba/kupewa Taraka.

Pamoja na mambo au sababu nyingine zinazopelekea tabia hii mbaya hizi zifuatazo hupelekea watu kutoka nje ya uhusiano wao wa kimapenzi/ndoa.

*Kutopata mapenzi ya kweli hasa ikiwa Kijana/Binti alilazimishwa kuoa/kuolewa na mtu ambaye hakumpenda “for the sake of Radhi ya Wazazi”, maadili, kuhofia umri n.k..

*Uchafu, kutojijali au kujipenda.-Wote mwanaumena mwanake.

*Kutoridhika au kutosheka na wakati mwingine uroho tu- Wanaume zaidi.

*Mmoja wenu kuwa na shughuli nyingi za kikazi/Biashara, kusafiri – Wote mwanamke na mwanaume..

*Tamaa ya kumiliki vitu Fulani –Wanawake zaidi.

*Kujaribu na kujifunza mambo mapya/mitindo lakini kutokana kufuata maadili unaogopa kuwa wazi kwa mpenzi wako-Wake kwa waume..

*Kukosa tendo la ndoa kwa muda mrefu ikiwa mwanamke ana Mimba kubwa /amejifungua n.k-Wanaume.

Kamanilivyowahi kusema kwenye makala moja iliyopita kwamba pamoja na mambo mengine mapenzi ni kuambizana ukweli, ikiwa mwenzi wako hakuridhishi, mchafu n.k ni vyema ukatafuta muda na ukamweleza taratibu tena kwa upendo, kumbuka hakuna Mwanadamu aliyekamilika hapa Duniani kila mmoja anakasoro zake.

Mpenzi wako (haijalishi mwanaume/mwanamke) ni kama mtoto anatakiwa kubembelezwa, kuelekezwa na ikiwezekana kufundishwa baadhi ya mambo ambayo hayajui.

Kama wewe ni mtu mzima na umepitia/unajua haya acha wenzako wanaoinukia maisha ya mapenzi wajifunze.

Asante na karibu tena.

Comments

Anonymous said…
Inatia moyo kuona mwanamke kajitokeza na kueleza maswala ya kutembea ovyo nje ya ndoa zao.

Wengi huwa tunasingizia wanawake wengine au kulalamika kuwa tabia za waume wetu mbaya kume wakati mwingine ni sisi wenyewe tunataka.

Dinah hongera sana na sisi tuko nyuma kukuunga mkono.

Kila lakheri bibie.
Anonymous said…
Dinah unataka kuniambia wewe hujawahi kulala na mwanaume mwingine na mpenzi wako hajui?

Mimi naona sikuhizi watu wote wanalala ovyo tu. Kama ulivyosema kwa wengine ni kama mtindo wao wa maisha.

Endelea nakazi yako nzuri ya kuelimisha jamii.
KKMie said…
Asanteni kwa ushirikiano wenu. Nikijibu swali la msomaji wangu hapo juu. Hapana sijawahi kulala na mtu nje ya uhusiano wangu (siwezi kujigawa), sikuzote nahakikisha siko kwenye uhusiano kabla sijalala/anza uhusiano mpya.

Karibu sana.
Anonymous said…
Dina mimi naomba contact yako plz kama vile number ya simu au email ya private, sina lengo lolote zaid nataka kukuuliza masuala but yawe private.

take care